Naomba msaada simu bora

Naomba msaada simu bora

Silicon Valley

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2012
Posts
1,092
Reaction score
1,119
Chief-Mkwawa Naomba msaada SIMU BORA

Naomba unichagulie simu bora ya kununua bajeti yangu Tsh 0.8mln up to 1.2mln napendelea sana double line kwajili ya kupunguza uzito mfukoni.

History yangu na simu, niliwahi kutumia simu zifuatazo:

1. Samsung Grand Duos miaka 3 – Internet slow sn

2. Samsung S6 miezi 8 - Ttzo kuchemka saana wakati inatumika

3. Samsung A8 miezi ninayo – Tatizo KUPOTEZA network inabidi washa zima mara kwa mara

Naomba kwa uwelewa wako nichagulie simu nzuri ilioko sokoni ninunue

Napengelea sana ku surf mtandaoni sana, Whattsapp, email , JF, Ila sina tabia ya kutunza music au movie hapana labda pics na movies za whatsapp tu
 
Chief-Mkwawa Naomba msaada SIMU BORA

Naomba unichagulie simu bora ya kununua bajeti yangu Tsh 0.8mln up to 1.2mln napendelea sana double line kwajili ya kupunguza uzito mfukoni.

History yangu na simu, niliwahi kutumia simu zifuatazo:

1. Samsung Grand Duos miaka 3 – Internet slow sn

2. Samsung S6 miezi 8 - Ttzo kuchemka saana wakati inatumika

3. Samsung A8 miezi ninayo – Tatizo KUPOTEZA network inabidi washa zima mara kwa mara

Naomba kwa uwelewa wako nichagulie simu nzuri ilioko sokoni ninunue

Napengelea sana ku surf mtandaoni sana, Whattsapp, email , JF, Ila sina tabia ya kutunza music au movie hapana labda pics na movies za whatsapp tu
najua mi sio ila kukusaidia mawazo jaribu iphone 6s au kama ni android jarib oneplûs 3 ila ni oxygen os juu ya android
 
ninatumia Tecno boom j5 muda mrefu sasa lakini matatizo yote ya hizo Samsung uliyoorodhesha hapo sijawahi kuyapata kwenye tecno Yangu nilijifunza kutokununua majina Bali ubora wa bidhaa
 
Hiyo s6 itakua ilikua na tatizo ,yangu haina shida hiyo na nafanya yote hayo plus kusikiliza music .
 
mkuu siku nyengine usiandike jina langu kwenye kichwa cha habari kama ni message yangu tu tafadhali nitumie kama private msg sababu unazuia watu wengine kuchangia uzi huu.

kati ya hizo simu kuna hata moja unayo? haswa haswa hio galaxy s6 na A8 maana kwa muono wangu simu nyingi za around budget hio zinafanana na hizo, badala ya kukimbilia kununua simu mpya tunaweza tukazirekebisha hizo hizo. na zilipopata matatizo ulizipeleka samsung shop?

pia kuna jambo jengine muhimu unatakiwa ulijue, simu za maduka yetu kibongo bongo asilimia 90 sio mpya ni refurbished wanazitoa masoko ya korea, china na marekani kuja kuzitupa huku hivyo unaponunua simu Tanzania double check ni version ya Kimataifa ambayo huuzwa kwetu na pia utume imei yake kwenda namba ya samsung ili kuhakiki zaidi. mfano unakuta simu kainunua mzungu marekani huko ina tatizo kairudisha kwenye kampuni then inaenda kurekebishwa na kuja kuuzwa kwa bei nafuu, wafanya biashara wa bongo huzinunua zile simu nafuu na kuja kuziuza huku, kama unataka kuspend hela nyingi kama hivyo hakikisha ni version ya kimataifa, kuwa safe zaidi kanunue duka la samsung official.

kuhusu network, ikiwa ni simu ya nje ambayo wameunlock na sio iliotengenezwa kwa ajili ya Tanzania unaweza kupata Tatizo la network sababu modem yake ni Tofauti, pia simu za Alluminium hazishiki vizuri Network kutokana na material yake compare na za plastic, hivyo kama eneo lako lina shida ya network pendelea zaidi simu za plastic au kama zinakuwa na alluminium iwe ni frame tu na sio full body.

kuhusu ku overheart almost simu yoyote yenye perfomance kubwa itapata moto, unachotakiwa ni kufunga apps usipotumia au kuweka battery server ili kudownclock processor simu isipate moto.

kama hizo simu hapo juu huna tena unaweza subiri miezi kadhaa ikitoka s8 basi s7 zitashuka sana bei, samsung kuacha utengenezaji wa note 7 kumefanya thamani ya s7 isishuke hivyo itakuwa ngumu kuipata budget hio (japo inawezekana kuipata), sababu umeshatumia s6 sioni simu nyengine ya kukushauri zaidi ya s7 na flagship za mwaka 2016. sema kutokana na warranty za samsung Tanzania sioni maana ya kununua kampuni za brand nyengine ambazo hata service centre hawana, labda Huawei kidogo na simu kama Honor 8 kama wataileta itamake sense budget hio.
 
ninatumia Tecno boom j5 muda mrefu sasa lakini matatizo yote ya hizo Samsung uliyoorodhesha hapo sijawahi kuyapata kwenye tecno Yangu nilijifunza kutokununua majina Bali ubora wa bidhaa
Tatizo Lake ni haina h+ na ni auto haina manual
 
mkuu siku nyengine usiandike jina langu kwenye kichwa cha habari kama ni message yangu tu tafadhali nitumie kama private msg sababu unazuia watu wengine kuchangia uzi huu.

kati ya hizo simu kuna hata moja unayo? haswa haswa hio galaxy s6 na A8 maana kwa muono wangu simu nyingi za around budget hio zinafanana na hizo, badala ya kukimbilia kununua simu mpya tunaweza tukazirekebisha hizo hizo. na zilipopata matatizo ulizipeleka samsung shop?

pia kuna jambo jengine muhimu unatakiwa ulijue, simu za maduka yetu kibongo bongo asilimia 90 sio mpya ni refurbished wanazitoa masoko ya korea, china na marekani kuja kuzitupa huku hivyo unaponunua simu Tanzania double check ni version ya Kimataifa ambayo huuzwa kwetu na pia utume imei yake kwenda namba ya samsung ili kuhakiki zaidi. mfano unakuta simu kainunua mzungu marekani huko ina tatizo kairudisha kwenye kampuni then inaenda kurekebishwa na kuja kuuzwa kwa bei nafuu, wafanya biashara wa bongo huzinunua zile simu nafuu na kuja kuziuza huku, kama unataka kuspend hela nyingi kama hivyo hakikisha ni version ya kimataifa, kuwa safe zaidi kanunue duka la samsung official.

kuhusu network, ikiwa ni simu ya nje ambayo wameunlock na sio iliotengenezwa kwa ajili ya Tanzania unaweza kupata Tatizo la network sababu modem yake ni Tofauti, pia simu za Alluminium hazishiki vizuri Network kutokana na material yake compare na za plastic, hivyo kama eneo lako lina shida ya network pendelea zaidi simu za plastic au kama zinakuwa na alluminium iwe ni frame tu na sio full body.

kuhusu ku overheart almost simu yoyote yenye perfomance kubwa itapata moto, unachotakiwa ni kufunga apps usipotumia au kuweka battery server ili kudownclock processor simu isipate moto.

kama hizo simu hapo juu huna tena unaweza subiri miezi kadhaa ikitoka s8 basi s7 zitashuka sana bei, samsung kuacha utengenezaji wa note 7 kumefanya thamani ya s7 isishuke hivyo itakuwa ngumu kuipata budget hio (japo inawezekana kuipata), sababu umeshatumia s6 sioni simu nyengine ya kukushauri zaidi ya s7 na flagship za mwaka 2016. sema kutokana na warranty za samsung Tanzania sioni maana ya kununua kampuni za brand nyengine ambazo hata service centre hawana, labda Huawei kidogo na simu kama Honor 8 kama wataileta itamake sense budget hio.
Mkuu Chief-mkwawa jipange kutupa somo juu ya quantum computer!
 
Chief-Mkwawa Naomba msaada SIMU BORA

Naomba unichagulie simu bora ya kununua bajeti yangu Tsh 0.8mln up to 1.2mln napendelea sana double line kwajili ya kupunguza uzito mfukoni.

History yangu na simu, niliwahi kutumia simu zifuatazo:

1. Samsung Grand Duos miaka 3 – Internet slow sn

2. Samsung S6 miezi 8 - Ttzo kuchemka saana wakati inatumika

3. Samsung A8 miezi ninayo – Tatizo KUPOTEZA network inabidi washa zima mara kwa mara

Naomba kwa uwelewa wako nichagulie simu nzuri ilioko sokoni ninunue

Napengelea sana ku surf mtandaoni sana, Whattsapp, email , JF, Ila sina tabia ya kutunza music au movie hapana labda pics na movies za whatsapp tu
sorry kwa kuingilia uzi wa watu, najaribu kucreate thread ila inakataa, shida yangu ni:
je tecno y3+ ina uwezo wa kusapoti laini ya 4g?
 
mkuu siku nyengine usiandike jina langu kwenye kichwa cha habari kama ni message yangu tu tafadhali nitumie kama private msg sababu unazuia watu wengine kuchangia uzi huu.

kati ya hizo simu kuna hata moja unayo? haswa haswa hio galaxy s6 na A8 maana kwa muono wangu simu nyingi za around budget hio zinafanana na hizo, badala ya kukimbilia kununua simu mpya tunaweza tukazirekebisha hizo hizo. na zilipopata matatizo ulizipeleka samsung shop?

pia kuna jambo jengine muhimu unatakiwa ulijue, simu za maduka yetu kibongo bongo asilimia 90 sio mpya ni refurbished wanazitoa masoko ya korea, china na marekani kuja kuzitupa huku hivyo unaponunua simu Tanzania double check ni version ya Kimataifa ambayo huuzwa kwetu na pia utume imei yake kwenda namba ya samsung ili kuhakiki zaidi. mfano unakut.....kama wataileta itamake sense budget hio.
duka la samsung official liko wapi kwa daresalaam?
 
mkuu siku nyengine usiandike jina langu kwenye kichwa cha habari kama ni message yangu tu tafadhali nitumie kama private msg sababu unazuia watu wengine kuchangia uzi huu.

kati ya hizo simu kuna hata moja unayo? haswa haswa hio galaxy s6 na A8 maana kwa muono wangu simu nyingi za around budget hio zinafanana na hizo, badala ya kukimbilia kununua simu mpya tunaweza tukazirekebisha hizo hizo. na zilipopata matatizo ulizipeleka samsung shop?

pia kuna jambo jengine muhimu unatakiwa ulijue, simu za maduka yetu kibongo bongo asilimia 90 sio mpya ni refurbished wanazitoa masoko ya korea, china na marekani kuja kuzitupa huku hivyo unaponunua simu Tanzania double check ni version ya Kimataifa ambayo huuzwa kwetu na pia utume imei yake kwenda namba ya samsung ili kuhakiki zaidi. mfano unakuta simu kainunua mzungu marekani huko ina tatizo kairudisha kwenye kampuni then inaenda kurekebishwa na kuja kuuzwa kwa bei nafuu, wafanya biashara wa bongo huzinunua zile simu nafuu na kuja kuziuza huku, kama unataka kuspend hela nyingi kama hivyo hakikisha ni version ya kimataifa, kuwa safe zaidi kanunue duka la samsung official.

kuhusu network, ikiwa ni simu ya nje ambayo wameunlock na sio iliotengenezwa kwa ajili ya Tanzania unaweza kupata Tatizo la network sababu modem yake ni Tofauti, pia simu za Alluminium hazishiki vizuri Network kutokana na material yake compare na za plastic, hivyo kama eneo lako lina shida ya network pendelea zaidi simu za plastic au kama zinakuwa na alluminium iwe ni frame tu na sio full body.

kuhusu ku overheart almost simu yoyote yenye perfomance kubwa itapata moto, unachotakiwa ni kufunga apps usipotumia au kuweka battery server ili kudownclock processor simu isipate moto.

kama hizo simu hapo juu huna tena unaweza subiri miezi kadhaa ikitoka s8 basi s7 zitashuka sana bei, samsung kuacha utengenezaji wa note 7 kumefanya thamani ya s7 isishuke hivyo itakuwa ngumu kuipata budget hio (japo inawezekana kuipata), sababu umeshatumia s6 sioni simu nyengine ya kukushauri zaidi ya s7 na flagship za mwaka 2016. sema kutokana na warranty za samsung Tanzania sioni maana ya kununua kampuni za brand nyengine ambazo hata service centre hawana, labda Huawei kidogo na simu kama Honor 8 kama wataileta itamake sense budget hio.
Pls mkuu na mm cm yngu ni huawei ascending 630 inasumbua SNA upande wa network cjui ni kwnn hta nkitumia line ya Halotel wkt cm nyngne ni za kaida SNA wakitumia Halotel zinakamata hadi H plus ila kwngu ni tofaut.msada wako chief-mkwawa
 
Sim za sasa hivi watu wengi wanalia network. Simu unanunua vizuri iko safi lakini baada ya miezi kadhaa utakuta unashindwa kuingia internet hata km uko karibu na mnara
 
Simu ambazo ni nzuri na zenye ubora kuanzia, network, internet, camera, n.k

1. Nexus 6p
2. Samsung galaxy s7
3. Black berry priv
4. HTC 10
5. LG G5
6. Huawei mate 8
7. Huawei p9
8. Honor 8
9. Sony xperia Z5
10. Apple iPhone s7

Hizi ndio simu zenye ubora wake na ni new brands ( 2016 ).

Gharama zake zipo juu kiasi kwa toleo jipya za hizi simu mpya.

Kidokezo:
Kampuni ya simu aina ya samsung Mara Nyingi inakuwa ngumu sana zinakuwa na utofauti sana,
Kuna samsung ambayo brand yake ni kutoka china, na nyingine kutoka Korea,
Kwa kupata simu orijino ni vizuri ukaoda samsung galaxy kutoka Korea,
Hizi total huwa ni orijino,

Then kwa kauli uliyotumia kusema kuwa unapendelea simu yenye laini 2,
Na kuoredhesha matatizo yake.
Simu nzuri ni laini moja,
Na hakikisha una oda kutoka nchi husika, usiogope gharama kwa sababu kitu bora na kizuri lazima iwe na gharama kubwa.
 
Back
Top Bottom