naomba msaada katika hili

ajmallah

Member
Jul 29, 2012
14
4
naomba mtu wa kunisaidia kulipa ada ya chuo kwasababu ya mama angu kushindwa kunilipia,nina mzazi mmoja tu ambae ni mama angu istoshe nina wadogo zangu ambao wanasoma sekondari katika shule ambazo si za serikali nao wanahitaji ada na sote tunamtegemea mama, na chuo ninacho soma nadaiwa ada ya mwaka wa pili wamasomo. Tafadhali kwa yeyote anaeweza kunisaidia mchango wowote ule hata wa mawazo nifenye nini kusuruhisha hili tatizo au niende wapi ambapo ntapata msaada.namaanisha kuwa nataka maada jamani
 
Funguka basi, chuo gani, kozi gani na kiasi gani unadaiwa. Je, hu-qualify kwa hiyo mikopo ??
Na likizo iliyopita, au sasa ulifanya juhudi zozote kuingiza ngawira au ?
 
nasoma chuo kikuu dodoma[udom] mwaka a pili, nasoma kozi ya Public Administration nadaiwa laki nne ndo ambazo hazijalipwa mpaka sasa,endapo chuo kikifunguliwa mwez wa kumi mwaka huu naingia mwaka wa tatu.Nimejitahid kutafuta japo ajira za muda mfupi ila sijapata,nimeomba maombi ya sensa baati ilkuwa si yangu,sijapata.Basi ndugu zangu hata sielewi na kama mavyojua ajira za siku hizi kujuana,na ketu mimi ndo mtu ambae nineza sema kuwa ndo nilobahatika kufika chuo.
 
nashidwa hata pa kuanzia ila pole sana.ila haujafunga ipasavyo kama mdau alivyosema hapo juu kama mtu akitaka kukusaidia atumie njia zipi?unapatikani wapi na nk.
 
mi naishi tegeta na familia yangu yani mama na wadogo zangu. kwa mawasiliano kwa lolote ushauri,nini nifanye ili ntatue tatizo langu unaweza ukantafuta kwa namba yangu ya simu 0717393652.
 
mi naish tegeta pamoja na familia yangu yaan mama na wadogo zangu,kwa mawasiliano kwa ajili ya mchango wowote ule ushauri juu ya tatizo langu,unataka kunisaidia pesa ili nilipe iyo ada namba zangu za simu ni 0714940663 au 0765818882.Pia nipo tayari kama mtu atataka tuandikishiane ili zile pesa alizoniazima nije kumrudishia baaada ya kumaliza masomo yangu yaan nikiwa nimepata ajira tayyari naahid ntakuwa muaminifu katika hili na atakuja kupajua kwetu na atamuona mama ili asidhan namdanganya au nataka kumdhurumu hapana,ni kweli ninashida na nataka kusaidiwa.
 
Naomba ufafanuzi kidogo. Je hiyo laki 4 ni sehemu ambayo bodi ya mikopo hailipi? (Nachukulia kuwa sehemu ya ada imelipwa na bodi). Kwenye hela ya chakula (laki 2 kwa mwezi nadhani kwa sasa) ulifanya saving yoyote kwa ajili ya ada?Nadhani ukijibana unaweza kusave hata laki 3 kwa ajili ya ada. Na hili ni muhimu sana kwa tunaotoka familia zenye uwezo mdogo kifedha. Tatizo wengi wakipata boom wanajirusha na kula maisha sana bila kufikiria mambo ya ada.
Kama ulijitahidi kufanya savings na ukalipa sehemu ya ada then unaweza pata msaada kidogo kama hadi hiyo October utakuwa hujapata kashughuli kakufanya ila nitahitaji details za kutosha kufanya due diligence usije ingiza watu mjini.
 
jamani mimi binafsi na mimi ni mhitimu wa chuo ambae bado sijapata kazi so nashindwa cha kukusaidia,ila nawaomba wenye uwezo msaidieni jamani kwa sababu hapa jf we are brothers and sisters na nina amini kuna watu wenye moyo wa kutoa watamsaidia.Ila na wewe mleta thread ukisaidiwa urudi hapa jf utujuze na kushukuru ili kutambua mchango wa wana jf.pole sana kila la kheri.
 
najitahidi sana kujibana huwezi amin ndugu yangu,Kozi ninayosoma ada yake ni laki 8 na bodi wananilipia laki 2 tu kwa hiyo laki 6 nalipa mwenyewe tangu mwaka wa kwanza najilipia mwenyewe ada kwa kubana pesa zangu za matumizi, nimeshindwa safari hii kwasababu ya kumlipia mdogo wangu ada kwa pesa zangu nizipatazo bodi ya mikopo ameanza form one private school,ndo mana nimejikuta nina deni la laki nne na chuo kikifunguliwa nahitajika kulipa ada japo nusu na pesa ya mahali pa kulala[hosteli] hapo ndo nachanganyikiwa nina deni halafu nahitaika kulipa pesa kabla sijaisajiliwa.
SIWEZI KUWAINGIZA WATU MJINI NINASHIDA NNAHITJI MSAADA NIMALIZIE MWAKA WANGU WA MWISHO WA MASOMO ALIETAYARI NIKOLADHI AJE MPAKA NYUMBANI NAISHI NA MAMA ANGU PAMOJA NA WADOGO ZANGU NMPATIE TAARIFA ZANGU ZOTE ANAZOZITAKA,MIMI SI TAPELI JAMAN NAMAANISHA NINALOLISEMA.
 
kwahiyo unahitaji hela kwa ajili ya kulipa ada na sio vinginevyo kwahiyo unataka hela cash au mtu akuingize kwenye account ya benki ya chuo na akuletee risiti ya benki yenye kiasi cha hela ambazo unataka kulipiwa na mimi naona hii ni njia rahisi na salama kama kweli shida yako ni ada ili watu waondokane na huu wizi wa mtaani wezi wengi na wote wanalia hivyohivyo na wako full documented May be au ni lazima chuo uende na hela Cash
 
chuoni wao wanahitji tu risiti zinazoonesha umelipa ada na wala si pesa cash,mtu anaweza akanilipia benk kwenye akaunt ya chuo ya tution fee na kunikabidhi risiti ambazo ndo muhimu siku ntakayo clear madeni yangu ya chuo.Hata mimi ntapenda mtu anipe risiti na si pesa cash.
 
Back
Top Bottom