Naomba msaada, dawa za mseto zinanisababishia tumbo kuumwa

bigmind

JF-Expert Member
Oct 28, 2015
12,457
12,668
Jamani hapa, ninajisikia kama kufa kabisa, ijumaa nilienda kuweka kambi kwenye pori moja kwa muda wa siku 2, kulikuwepo na mbu sijapata ona, niling'atwa si kawaida kusema kweli haraka nilijitabiria malaria ile jumapili narudi home nikawa hoi tayari malaria. Sasa nikachukua mseto, hizi dawa za wizara ya Afya.

Shida yangu ni kuwa dawa inanikwatuza tumbo sijapata ona, tumbo linanyonga mpaka nalia...!

Nilianza dozi jumapili usiku saa nne, bado vidonge nane tuu ambavyo vinapaswa kuisha kesho, ila hapa tayari nimeghairi sitavimalizia, je hili tatizo ni kwangu au kila mtu anasumbuliwa na mseto. Msaada jamani nafwaa...
 
Jamani hapa, ninajisikia kama kufa kabisa, ijumaa nilienda kuweka kambi kwenye pori moja kwa muda wa siku 2, kulikuwepo na mbu sijapata ona, niling'atwa si kawaida kusema kweli haraka nilijitabiria malaria ile jumapili narudi home nikawa hoi tayari malaria. Sasa nikachukua mseto, hizi dawa za wizara ya Afya.

SHIDA YANGU NI KUWA DAWA INANIKWATUZA TUMBO SIJAPATA ONA, TUMBO LINANYONGA MPAKA NALIA...!

Nilianza dozi jumapili usiku saa nne, bado vidonge nane tuu ambavyo vinapaswa kuisha kesho, ila hapa tayari nimeghairi sitavimalizia, je hili tatizo ni kwangu au kila mtu anasumbuliwa na mseto. Msaada jamani nafwaa...
Nenda hospitali hapa sanasana utaambiwa uache dozi na ukanywe bia
 
Mababu na mabibi zetu vizazi vinne ,vitano kuendelea kabla ya kuja wageni toka Asia na Ulaya walikuwa wanatumia miti hii kwa tiba za magonjwa yoyote yale na wanapona kabisa.
Sasa ndugu tafuta majani au mzizi wa muarobaini chemsha kunywa , ni tiba ya matatizo mengi ya kiafya.
 
Je, wajua asili ya jina la malaria ? Jina la malaria ni muungano wa maneno mawili ya ki Latin ambayo ni mal - yaani mbaya na aire ( air ) yaani hewa.Ukiunganisha haya maneno mawili unapata " mala aire maanake hewa mbaya.Zamani kabla ya ugunduzi wa darubini Wagiriki walipokuwa wanasafiri maeneo ya mbali kutafuta biashara waliweza kuumwa na mbu na mara tu baada ya kurudi walijisikia homa kali na kutetemeka.Kwa sababu ya kutokuwa na vyombo kama darubini ya kubaini chanzo cha homa hiyo walizoea kurahisisha tu kuwa wameugua kwa sababu ya " hewa mbaya " ( mal aire ) .Baada ya sayansi kuja na kubaini kuwa homa hiyo imetokana na kuumwa na mbu.Lakini jina lilibaki vivo hivyo la hewa mbaya. Kwa hiyo malaria maana yake kiasili ni hewa mbaya.
Hata wewe kule ulikoenda na baada ya kurudi ukaanza kujisikia vibaya ni kwa sababu ya " hewa mbaya " ya huko ( uliumwa na mbu na kupata malaria ).
 
Mababu na mabibi zetu vizazi vinne ,vitano kuendelea kabla ya kuja wageni toka Asia na Ulaya walikuwa wanatumia miti hii kwa tiba za magonjwa yoyote yale na wanapona kabisa.
Sasa ndugu tafuta majani au mzizi wa muarobaini chemsha kunywa , ni tiba ya matatizo mengi ya kiafya.
Mmmhh! Muarobain tena..!
 
Je, wajua asili ya jina la malaria ? Jina la malaria ni muungano wa maneno mawili ya ki Latin ambayo ni mal - yaani mbaya na aire ( air ) yaani hewa.Ukiunganisha haya maneno mawili unapata " mala aire maanake hewa mbaya.Zamani kabla ya ugunduzi wa darubini Wagiriki walipokuwa wanasafiri maeneo ya mbali kutafuta biashara waliweza kuumwa na mbu na mara tu baada ya kurudi walijisikia homa kali na kutetemeka.Kwa sababu ya kutokuwa na vyombo kama darubini ya kubaini chanzo cha homa hiyo walizoea kurahisisha tu kuwa wameugua kwa sababu ya " hewa mbaya " ( mal aire ) .Baada ya sayansi kuja na kubaini kuwa homa hiyo imetokana na kuumwa na mbu.Lakini jina lilibaki vivo hivyo la hewa mbaya. Kwa hiyo malaria maana yake kiasili ni hewa mbaya.
Hata wewe kule ulikoenda na baada ya kurudi ukaanza kujisikia vibaya ni kwa sababu ya " hewa mbaya " ya huko ( uliumwa na mbu na kupata malaria ).
Jamani..! Acha tu ndugu, ata sijaendelea na dozi..!
 
Nimetumia dawa mseto kutibu malaria, sawa ile ya 3000. Leo ni siku ya tatu uwezo wa Kunusa umepotea sisikii hata harufu ya perfume
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom