Naomba majibu kutoka kwa wanasheria

Rweye

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
16,958
7,512
Leo mimeona niweke haya mambo kwenu ili nipate kuelewa vyema, wanasheria naomba mnisaidie

1. Ni kwanini mtu anapelekwa mahakamani kabla ushaidi haujakamilika?. Tumeona kesi nyingi sana zikizungushwa kwa mda mrefu sana eti kisa ushaidi haujakamilika, kama ushaidi haujakamilika ni kwanini ashitakiwe na kuanza kuzungushwa mahakamani wakati bado mnaomushtaki hamna ushaidi wa kutosha?

2. Naangalia kesi ya Kenyatta na Ruto kule ICC, mbona hawa walikuwa wakihudhuria kesi kutokea makwao kisha wanarudi walikotoka. Kwanini huu utaratibu usitumike hadi pale huyo mtu atakapobainika kuwa na hatia ndo ahamishiwe sero?

3. Ninaangalia kesi za akina EPA, IPTL na ESCROW. Mara nyingi wananchi tumehoji ni kwanini wahusika hawapelekwi mahakamani na kila wakati yamekuwepo majibu yasiyo ridhisha kabisa. Mara nyingi TAKUKURU wamekuwa wakisema hawawezi kuwapeleka mahakamani hadi pale ushaidi na upelelezi utakapokamilika. Swali, kama hivyo ndivyo ni kwanini mfano leo tunaona akina Seth na Ruge wamepelekwa mahakamani na kila siku wanapigwa tarehe tukiambiwa bado upelelezi haujakamilika. Iweje hawa wamepelekwa japo upelelezi haujakamilika na watuhumiwa wengine wameachwa mtaani kwa kisingizio kile kile? Ni nini sasa maana ya upelelezi kukamilika ili mtu apelekwe mahakamani na upelelezi kutokukamilika mtu anaendelea kusoteshwa rumande?

4. Mtu anayepelekwa sero wakati kesi ikiendelea na baadae ikaonekana hakuwa na hatia na akaachiwa huru huku ameishi sero mda mwingi tu, huyu mtu huwa anastahili kulipwa na huwa analipwaje na sana sana pale anapokuwa alishtakiwa na serikali?

Kwa leo nakomea hapa kwanza ....
 
Maelezo yanawwza kuwa mengi mkuu, download sheria hizi upitie mkuu
 

Attachments

  • jinai.pdf
    688.5 KB · Views: 186
  • jinai.pdf
    688.5 KB · Views: 127
  • CIVIL PROCEDURE CODE.pdf
    665.4 KB · Views: 1,319
  • PENAL CODE OF TZ English version.pdf
    419.8 KB · Views: 108
Hapa niudikiteta tu.

Unawezaje kumshika mtu kwa hoja zakipuuzipuuzi tena watu wenye dhama kubwa kwenye taasisi mbalimbali kubwa na zaheshima

Madudu haya hupangwa kudhalilisha watu na heshima zao kwa visingizio vya hovyo namwisho huoneka hakuna hoja ila vioja.
 
Hapa niudikiteta tu.

Unawezaje kumshika mtu kwa hoja zakipuuzipuuzi tena watu wenye dhama kubwa kwenye taasisi mbalimbali kubwa na zaheshima
Unaweza kuwa sahihi Mkuu make ifs ni nyingi kuliko fact zenyewe

Madudu haya hupangwa kudhalilisha watu na heshima zao kwa visingizio vya hovyo namwisho huoneka hakuna hoja ila vioja.
 
Hapa niudikiteta tu.

Unawezaje kumshika mtu kwa hoja zakipuuzipuuzi tena watu wenye dhama kubwa kwenye taasisi mbalimbali kubwa na zaheshima
Unaweza kuwa sahihi Mkuu make ifs ni nyingi kuliko fact zenyewe

Madudu haya hupangwa kudhalilisha watu na heshima zao kwa visingizio vya hovyo namwisho huoneka hakuna hoja ila vioja.
 
Nadhani kunakuwa na ushahidi wa mwanzo kwanza ili mtu awe implicated, ila ushahidi usio na shaka wa kumtia mtu hatiani ndio mahakamani sasa.....au?
 
Maelezo yanawwza kuwa mengi mkuu, download sheria hizi upitie mkuu
Usituletee vifungu mkuu, tupe maelezo ya ujumla ni kwanini kuna matumizi ya hivyo vifungu na vya namna hiyo ambavyo kwanza haviko universal na pili vinaonekana kutokujali haki za mtuhumiwa. Kumbuka mtuhumiwa si criminal ila kisa katuhumiwa basi anakuwa treated kana kwamba tayari ni kweli ana hatia kumbe hata ushaidi bado haupo

Why such laws?
 
Nadhani kunakuwa na ushahidi wa mwanzo kwanza ili mtu awe implicated, ila ushahidi usio na shaka wa kumtia mtu hatiani ndio mahakamani sasa.....au?
Maswali yako 4 mama, sasa wewe unajibu lipi? Lakini pia, ni nini maana ya kuwabakisha hawa mtaani kwamba ushaidi bado na kuwapeleka wengine kwa maelezo kwamba ushaidi wa kuwafungulia mashtaka tayari na baadae mnaanza tena kuhairisha kesi kwamba eti ushaidi haujakamilika?
 
Ni nini maana ya kuwabakisha hawa mtaani kwamba ushaidi bado na kuwapeleka wengine kwa maelezo kwamba ushaidi wa kuwafungulia mashtaka tayari na baadae mnaanza tena kuhairisha kesi kwamba eti ushaidi haujakamilika?
Naona huo ushahidi unakuwa challenged na mawakili wa utetezi, wakileta mwingine wa wenye nguvu zaidi basi mshatkiwa anahukumiwa
 
Usituletee vifungu mkuu, tupe maelezo ya ujumla ni kwanini kuna matumizi ya hivyo vifungu na vya namna hiyo ambavyo kwanza haviko universal na pili vinaonekana kutokujali haki za mtuhumiwa. Kumbuka mtuhumiwa si criminal ila kisa katuhumiwa basi anakuwa treated kana kwamba tayari ni kweli ana hatia kumbe hata ushaidi bado haupo

Why such laws?
Wakuu mbalimbali, kwanza inategemea ni kesi ya jinai au ya madai. Polisi hushughulikia kesi za jinai tu (criminal cases), kesi za madai zote (civil) huanzia mahakamani moja kwa moja. Watu wengi kimsingi wamekua wakinyimwa haki zao kwa kutokujua sheria. Dhamana na haki ya kuwasiliana na ndg na matibabu nk nihaki ya mtuhumiwa. Unless kuna mazingira ya kunyimwa dhamana kwa mtuhumiwa kulingana na kutokwenda kuhribu ushahidi ama rekod yake ya nyuma, ama polisi au hakimu atavoona inakua ngumu kwa mazingira fulani, ndipo dhamana huweza kukataliwa. Dhamana ni haki y mtuhumiwa. Nimetoa hizo PDFs hapo ili angalau mzipitie mshibe kuliko haya maelezo nusunusu. Nawasilisha
 
Wakuu mbalimbali, kwanza inategemea ni kesi ya jinai au ya madai. Polisi hushughulikia kesi za jinai tu (criminal cases), kesi za madai zote (civil) huanzia mahakamani moja kwa moja. Watu wengi kimsingi wamekua wakinyimwa haki zao kwa kutokujua sheria. Dhamana na haki ya kuwasiliana na ndg na matibabu nk nihaki ya mtuhumiwa. Unless kuna mazingira ya kunyimwa dhamana kwa mtuhumiwa kulingana na kutokwenda kuhribu ushahidi ama rekod yake ya nyuma, ama polisi au hakimu atavoona inakua ngumu kwa mazingira fulani, ndipo dhamana huweza kukataliwa. Dhamana ni haki y mtuhumiwa. Nimetoa hizo PDFs hapo ili angalau mzipitie mshibe kuliko haya maelezo nusunusu. Nawasilisha
Shukurani mkuu kwa utangulizi ..sasa tusaidie katika swali la 2,3 na nne kwa kina
 
Naona huo ushahidi unakuwa challenged na mawakili wa utetezi, wakileta mwingine wa wenye nguvu zaidi basi mshatkiwa anahukumiwa
Asante ijapo kuna maswali hapa pia lakini nafuu. Tusaidie swali la mwisho
 
Asante ijapo kuna maswali hapa pia lakini nafuu. Tusaidie swali la mwisho
hahaa, mimi sio mwanasheria mkuu, najibu kutokana na ninavyoona, wanasheria wakija nadhani watajibu ufasaha zaidi

Ila kwenye hilo swali la nne najaribu kukujibu hivi, kama hakuna mizengwe (mahakama kuingiliwa na serikali au watu wengine wenye nguvu) mtu ni ngumu kuwekwa sero , kuna dhamana na dhamana inaendana na makosa husika, kama ni kosa la kawaida basi dhamana yake inakuwa ni rahisi tu mtu kumudu,ila kama ni makosa ni makubwa sana basi dhamana nayo inakuwa serious, sema watu wanakosa dhamana kwa makosa ya kawaida kutokana na kutojipanga kwao

Japo kuna makosa ambayo hayana dhamana mfano kesi ya mauaji ila nadhani mtu kushatkiwa kwa kesi ya mauji hadi na hadi akose dhamana basi kutakuwa na ushahidi mkubwa tu wa awali
Ila makosa mengine huwa sielewikwa nini hayana dhamana mfano kosa la utakatishaji fedha labda wakili Petro E. Mselewa aje atuambie
 
Wakuu, kesi ni ushahidi, (wa mazingira, vielelezo nk). Na kesi yyte ile ni wakili mzuri ndo atakunasua. Kesi ulizotaja hapo juu unaongelea watu wanaojua sheria na uwezo mkubwa wa kifedha, serikali haiwez kuingia kichwa kichwa ukizingatia ni nadra sana kushinda kesi kortini. Wamejitafakari wakaona hawawez kuivheza iyo ngoma. Mwenendo wa kesi ikishatoka ruling, mahakama inaweza kuamua serikali iwalipe hao watu gharama za uendeshaji na wanaweza kulipwa fidia ya pesa mzuri kwwli kweli.

Kuhusu swali la mwisho, kama nilivosema hapo juu, baada ya verdict, mtuhumiwa anayo haki kufungua shauri mahakmani dhidi ya polisi,au mlalamikji ama mtu yyte ambae ana malalamiko nae ya msingi kuhusiana na mwwnendo mzima wa shauri na mahakama ikijiridhisha juu ya madai hayo itaona namna inayofaa mlalamikaji kulipwa
 
Wakuu, kesi ni ushahidi, (wa mazingira, vielelezo nk). Na kesi yyte ile ni wakili mzuri ndo atakunasua. Kesi ulizotaja hapo juu unaongelea watu wanaojua sheria na uwezo mkubwa wa kifedha, serikali haiwez kuingia kichwa kichwa ukizingatia ni nadra sana kushinda kesi kortini. Wamejitafakari wakaona hawawez kuivheza iyo ngoma. Mwenendo wa kesi ikishatoka ruling, mahakama inaweza kuamua serikali iwalipe hao watu gharama za uendeshaji na wanaweza kulipwa fidia ya pesa mzuri kwwli kweli.

Kuhusu swali la mwisho, kama nilivosema hapo juu, baada ya verdict, mtuhumiwa anayo haki kufungua shauri mahakmani dhidi ya polisi,au mlalamikji ama mtu yyte ambae ana malalamiko nae ya msingi kuhusiana na mwwnendo mzima wa shauri na mahakama ikijiridhisha juu ya madai hayo itaona namna inayofaa mlalamikaji kulipwa
Mkuu nimepata la kuchukua hapa, asante. Sasa tusaidie tena, ni kweli walio mtaani ushaidi unakuwa bado?
Na je ni kweli wanaosemwa ushaidi umekamilika wakienda mahakamani ushaidi huwa bado ama nini huwa kinasemwa bado upelelezi unaendelea?

Na ni kweli kinachotekea mahakamani ni pesa zaidi ya kuliko haki? Make hata wewe naona unakazia sana maamuzi ya mahakama kudhoofishwa kati ya wenye nazo dhidi ya waso nazo, unamaanisha hukumu nyingi ni matokeo ya pesa na si matakwa ya kisheria ilivyo?

Na swali la mwisho kwa leo

5. Naelewa kuna kesi zinatakiwa kuanzia mahakama za wilaya n.k lakini pia kuna kesi zinapelekwa mfano kisutu wakati hii mahakama haina nguvu ya kusikiliza na kutoa hukumu juu ya baadhi ya kesi. Ni kwanini hizo kesi huwa hazipelekwi moja kwa moja kwenye mahakama stahiki badala ya kuanza kuzungushana kuanzia kwingine alafu ndo baadae muhamishiwe kwingine?

Nishukuru na niishie hapa ila nitarudi siku nyingine kwa ajiri ya kutafuta uelewa zaidi kutoka kwenu wanasheria.
 
Back
Top Bottom