Habari ya Sunday wana GT!
Nimetafakari sana kuhusu Ongozi (sio sanifu) zetu za kiafrika za kutumia nguvu nyingi kupitiliza kwa kukandamiza uhuru wa Raia na mali zao. Hii imekuwa ni kawaida kwa viongozi wetu wa kiafrika na wale wanaotoka Dunia ya tatu na ya kwanza nje ya Afrika wenye viashiria vya Ujamaa kama Cuba, Russia, Iran, China, Puerto Rico, Venezuela (past), Colombia, North Korea n.k.
Viongozi wamekuwa wababe kupitiliza kitu ambacho kinapelekea kuchukiwa na Raia.
Leo PLOII nitoe Somo kidogo kwa hawa wababe kwa Raia wao Trump akitia Mguu ubabe na ulinzi wao unayeyuka kama Barafu ya Congo Basin.
1. Viongozi wetu Usalama wa kwanza ni kuishi na Raia wako vizuri. Adui akiona unapendwa wanaweza kusogeza siku za kukumaliza au hata kushindwa kabisa mfano Hugo Chavez huu mtihani alishinda lakini Maduro kwa kiburi kapita angle mbovu sasa yupo kwenye ukuta mzito hana tofauti na Mende aliyeingia ndani ya Box.
2. Viongozi ni lazima tutengeneze mifumo ya kiutawala kila mtu awajibike sio kuwa na watu walio juu ya katiba wanafanya wanachotaka, ukweli ni kuwa bila National Cohesion, Solidarity & Integrity no security anymore.
NB: Viongozi wetu Russia hawezi kukupa hakikisho la kudumu la Ulinzi kwa sababu hata Putin anaishi kama Joka la Mdimu ni kiongozi ambaye amechokwa na watu wake na Fisadi Mfano mzuri, Wegner Group ni kikundi bora sana cha kupigana Putin aliamini ndicho kikundi sahihi cha kumsaidia lakini hakukuwa na Mwisho mzuri na 2023 Yevgeny Victorovich Prigozhin akapotezwa. Kiongozi kama Putin hana tofauti na Ayatollah Ali Khamenei au Maduro au Xi wanaishi kwa kubana watu na kuua wakosoaji wao. Unapotengeneza Adui ndani ya Taifa haupo Salama mfano mzuri Iran Top existing & Ex leaders became informers to CIA & MOSSAD Na hao ndio wametoa mchongo alipo Khamenei Mossad wakatupa Kiazi Mbatata.
Hii ni kusema Russia na China sio washirika sahihi linapokuja suala la Ulinzi na Usalama kwa Mshirika wao bado na wao wanajitafuta.
Tukubali kuwa Trump akiamua kumnyakua yeyote anaweza tofauti kuna sehem atafanya Operation ya siku 1 na nyingine 5.
Mwisho:
Viongozi wa Kiafrika Jifunzeni kuna yule Mzee M7, Kiir wamechoka lakini kuchinja watu sio shida kwao mnaacha Legacy mbaya, it is a stern to state their Equivocal Leadership.
Tusidanganywe kuwa Russia ni mbabe wa Vita. Russia alishindwa kutoa full control kule Afghanistan 1979, Russia Mshirika wake Colonel Muammar alishindwa kumlinda 2010-2011, Russia kashindwa kuwalinda Houths, Likud, Russia kashindwa kumlinda Bashar Assad kule Syria, Russia kashindwa kumlinda Nicolaus Maduro, Russia kashindwa kulinda usalama wa Mwamba sana A Supreme Leader ever on Earth Ayatollah Ali Khamenei.
Russia alipigwa na Japan Feb 1904 -Sep 1905 "Russo- Japanese War" chini ya Tsar Nicolas II against Emperor Meiji.
Russia alipigana Vita kubwa ni ile ya kumwondoa Kiongozi wa Kinazi na Fascist leader from Italy Adolf na Benito, naweza kusema kwa sababu ya kutengeneza internal insecurity ilikuwa rahisi Germany and Italy to be Languished miserably. Mbali na hivyo Russia kashinda Vita gani na hii ya Adolf Aloyce Hitler ni kwa sababu ya Triple Entente na USA akiwemo kama Weapons Supplier.
China ndio takataka kabisa kwenye Medali ya kivita hana uzoefu wowote ni sawa na India. Kihistoria Japan kamchapa sana kipindi cha Hirohito so Viongozi wetu pendeni watu wenu ili mpate hakikisho la Usalama. USA daily yupo Mzigoni mwamba ana uzoefu na washirika watiifu Je sisi wengine?