Naomba kujua ukweli kuhusu 'kiama'

Mr Antidote

JF-Expert Member
Jan 11, 2015
944
1,271
Habari zenu wana JF,

Kuna kitu nimekiwaza na kukitafakari kwa muda wa kama siku 3 hivi lakini bado sijapata majibu yake. Basi nipo hapa kuomba msaada wa kueleweshwa kiundani kwa watu wenye uelewa wa mambo ya kidini awe muislam, mkristo budhaa na hata asiye na dini.

Suala kubwa linalonitatiza ni kuhusu ukweli wa siku ya kiama, jehanamu na pepo. Je kweli hivi vitu vipo kweli? Nikiri wazi kabisa kwamba mimi ni mkristo mkatoliki na nimekua nikifundishwa haya kama sio kukaririshwa toka nikiwa mdogo katika mafundisho ya komunio ya kwanza na kipaimara kwamba kuna hivyo vitu 3 nilivyovitaja.

Yafuatayo ni maswali ambayo najiuliza na ningefurah kama nitapata majibu ya kina na kuridhisha.

1. Je ni kweli kuna siku ya kiama?

2. Na kama kweli ipo kwanini MUNGU aliwaadhibu na kuviangamiza baadhi ya vizazi kwa matendo yao machafu na kutosubiri siku ya kiama?

3. Je hawa walioadhibiwa na kuangamizwa siku za nyuma walikuwa waovu kuliko sisi wa zama hizi?

4. Je hao walioangamizwa wataletwa tena mbele ya hukumu? Na nini hatima yao na ilihali walishaadhibiwa kwa kuangamizwa?


Baada ya kupata ufafanuzi wa kutosha wa maswali hayo nadhani suala la pepo na jehanamu nitaweza kulielewa kwa urahisi.

Inawezekana kabisa kuwa kuna mada kama hii imeshawahi kujadiliwa kama hamtojali naomba kuwekewa link yake.

NB: Nimetumia zama za nabii Nuhu na gharika kuu kuuliza maswali hayo.


Shukrani.
 
Ukisha vika umri wa miaka 18 unakua na uwezo wa kujua jema na baya. Hakuna ajuae siri ya kiama umaut wako ndio kiama chako. Kama unavyojua kua mungu yupo ila hujawah kumwona. Hapa twende kwa hisia. Epuka kutenda mabaya yasiyompendeza mungu wako ili kiama yako usije ukawa kuni upumzike kwa amani
 
hukumu(kiama) ya mwanadamu inaanza mara tu baada ya mtu kufa. aliyetubu dhambi na kupatana na Mungu atapelekwa Mbinguni na asiyetubu ataenda motoni. wale wa zamani walioangamizwa sio kwamba ni waovu zaidi yetu bali ni matashi ya Mungu kuchagua njia ya kutunyoosha viumbe wake. ulichofundishwa ktk imani yako ni kweli kabisa, kishike. tenda mema acha mabaya. penda kutubu kila unapomkosea Mungu.
 
hukumu(kiama) ya mwanadamu inaanza mara tu baada ya mtu kufa. aliyetubu dhambi na kupatana na Mungu atapelekwa Mbinguni na asiyetubu ataenda motoni. wale wa zamani walioangamizwa sio kwamba ni waovu zaidi yetu bali ni matashi ya Mungu kuchagua njia ya kutunyoosha viumbe wake. ulichofundishwa ktk imani yako ni kweli kabisa, kishike. tenda mema acha mabaya. penda kutubu kila unapomkosea Mungu.
Haya mambo ya kiroho kwa kiasi kikubwa yana utata sana. Tunaambiwa mtu yaani nafsi anapatikana kutokana na muunganiko wa mwili na roho (pumzi ya uhai) na kwamba mtu huyo anapokufa mwili uoza lakini roho ubaki ikisubiri siku ya kiama. Sasa swali ni kwamba kama kiama kinaanza muda au siku ile mtu anapokufa iweje adhabu iwe ni kwa roho tu na siyo kwa mwili pia wakati kipindi cha kutenda dhambi vilikuwa pamoja?

Na kama mateso yanaanza mara moja baada ya mtu kufa basi ni dhahiri kwamba wale wenzetu waliofariki karne nyingi zilizopita hadi siku ya kiama itakapofika watakuwa wamepata mateso makubwa zaidi (ya muda mrefu) kuliko wale watakao wamekufa miaka michache (mfano mwaka mmoja, miwili kumi n.k.) kabla ya hiyo siku ya kiama. Na kama wakianza kutumikia adhabu zao baada ya kiama hao waliokufa na kupata mateso karne nyingi zilizopita kuliko wengine watapunguziwa adhabu au la?!

Kingine mtu anazaliwa na kudumu duniani kwa dakika, masaa, siku au miaka michache tu lakini siku ya kiama anakuja kutumikia adhabu jehanamu milele! Daah...mimi hata sielewi bana.
 
Kwakuwa umeuliza kwa imani zote nami nisemi kidogo. Katika uisilam kiama ni siku ngumu kuliko ugumu wowote ambao mwanadamu anaweza waza. Ni siku ya hukumu. Kabla ya kusimama kiama ni wazi kuwa viumbe wote watakafu(wakiwemo maaika wote mpaka mtoa roho-Izraeli).

Kisha watu watafufuliwa kutoka katika matumbo ya ardhi wakiwa katika hali tofauti tofauti.kulingana na matendo yao. Hata hivyo bado siku hiyo itakuwa ngumu sana isipokuwa tu kwa wale waliridhiwa na mola wao.

Hapo ndipo watu watahukumiwa kwa matendo yao. Kuna mchakato mrefu.sana siku hiyo. Hakuna kujuana hapo baba hatamjua mwana wala mwana hatamjua mama. Kila mtu nafsi yake itakuwa imeshughulishwa na mambo yake. Kisha watu watahukumiwa kwa kuulizwa juu ya.yale waloyatenda. Na pindi watakapo danganya,itafungwa midomo yao kisha kila kiungo kipekee kitatoa ushahidi wa kila ulichokifanya.

Kwa wale wanodhani ukifa ndio kiama chako,hakika hawapo sahihi hata.kidogo. Kufa ni katika kitendo cha kufika.mwisho.wa dumia.na mwanzo wa akhera. Kaburi watu watu wataanza kukutana na kheri zao ama shari zao kulingana na matendo yao. Hapo ni adhabu kwa makosa hadi itakapo fika kiama. Na adhanu hii haipunguzi.adhabu atakayoipata mwanadamu siku ya kiama baada ya kuhukumiwa.

Hakika kiama ni siku nzito na tunamuomba Molla wetu atufishe.ili hali yu radhi na sisi ili tuweze kuongoka adhabu zake. Amin.
 
kwa mjib wa biblia kunasiku ya mwisho ambapo yesu atakuja na kutakuwa na parapanda kuu, ambapo itawaamsha wafu na wale watakatifu watamlaki yesu Mawinguni,

waovu wataikimbilia milima, na mito ili wajistiri lakini mito na milima itawakimbia, kutakuwa na kitimtim balaa,

baada ya hapo waovu, watakufa na kusubri hukumu ya mwisho ya kuchomwa moto, kisha yetu atarejea na watakatifu mji wa yeruslem na ndipo waovu watafufuliwa na kuchomwa moto..

kumbuka moto umeandaliwa kwa ajiri ya shetani na malaika zake, wanadam ni kuni tu, kwa kukataa kutii sauti ya Mungu

kuwa sehem ya kumfuata kristo kama bwana na mwokozi wa maisha yako...
 
si
kwa mjib wa biblia kunasiku ya mwisho ambapo yesu atakuja na kutakuwa na parapanda kuu, ambapo itawaamsha wafu na wale watakatifu watamlaki yesu Mawinguni,

waovu wataikimbilia milima, na mito ili wajistiri lakini mito na milima itawakimbia, kutakuwa na kitimtim balaa,

baada ya hapo waovu, watakufa na kusubri hukumu ya mwisho ya kuchomwa moto, kisha yetu atarejea na watakatifu mji wa yeruslem na ndipo waovu watafufuliwa na kuchomwa moto..

kumbuka moto umeandaliwa kwa ajiri ya shetani na malaika zake, wanadam ni kuni tu, kwa kukataa kutii sauti ya Mungu

kuwa sehem ya kumfuata kristo kama bwana na mwokozi wa maisha yako...
mkuu leta vifungu angalau kuuthibitisha ukweli huu
 
Majibu ya maswali yako kwa upande wa ukirsto iko hivi;

Moja, ni kweli siku ya kiama ipo na kwenye biblia inafahamika kama siku ya hukumu. Soma biblia Mathayo 24:14 "Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja".

Pia siku hii kibiblia inafahamika kama har-magedon soma ufunuo 16:14-16.

Majibu ya swali la pili kuhusu kwanini Mungu aliwaangamiza wanadamu wa kipindi cha kwanza bila kusubiri siku ya kiama, ni kweli Mungu aliwangamiza wanadamu hawa bila kusubiri siku ya kiama ilikuwa ni kwa sababu Mungu alitoa agizo kwa wanadamu hawa juu ya nini wanapaswa kufanya na nini hawapaswi kufanya lakini wanadamu hawa walishindwa kutii agizo hili.

Soma Mwanzo 3:1-4
"Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, msile matunda yote ya miti ya bustani? mwanamke akamwambia nyoka matunda ya miti ya bustani twaweza kula lakini matunda ya mti wa katikati ya bustani Mungu amesema msiyale wala msiyaguse msije mkafa.."

Majibu ya swali la tatu, sikweli kwamba wanadamu wa Enzi hizo walikuwa na dhambi nyingi kuliko sisi bali wanadamu wa sasa na wakipindi hicho wanafanana kwa matendo na dhambi kinacho wasaidia wanadamu wa sasa ni ule upendo wa Mungu kuelekea ulimwengu huu kupitia damu ya mwanaye Yesu kristo ambapo Mungu aliupenda ulimwengu huu tena. Soma Yohana 3;16.

Majibu ya swali la nne kuhusu wanadamu wa Enzi hizo watafufuliwa ili kuhukumiwa ni kweli watafufuliwa tena na kuhukumiwa hukumu ya haki ukiacha ya kipindi kile ambayo iliwakumba hata ambao hawakuwa na makosa au dhambi. Soma 2Petro 4-9
 
hukumu(kiama) ya mwanadamu inaanza mara tu baada ya mtu kufa. aliyetubu dhambi na kupatana na Mungu atapelekwa Mbinguni na asiyetubu ataenda motoni. wale wa zamani walioangamizwa sio kwamba ni waovu zaidi yetu bali ni matashi ya Mungu kuchagua njia ya kutunyoosha viumbe wake. ulichofundishwa ktk imani yako ni kweli kabisa, kishike. tenda mema acha mabaya. penda kutubu kila unapomkosea Mungu.

Muwe mnaandka na maandiko bac co mnaropoka tu
 
kwa mjib wa biblia kunasiku ya mwisho ambapo yesu atakuja na kutakuwa na parapanda kuu, ambapo itawaamsha wafu na wale watakatifu watamlaki yesu Mawinguni,

waovu wataikimbilia milima, na mito ili wajistiri lakini mito na milima itawakimbia, kutakuwa na kitimtim balaa,

baada ya hapo waovu, watakufa na kusubri hukumu ya mwisho ya kuchomwa moto, kisha yetu atarejea na watakatifu mji wa yeruslem na ndipo waovu watafufuliwa na kuchomwa moto..

kumbuka moto umeandaliwa kwa ajiri ya shetani na malaika zake, wanadam ni kuni tu, kwa kukataa kutii sauti ya Mungu

kuwa sehem ya kumfuata kristo kama bwana na mwokozi wa maisha yako...
atarejea yerusalemu ipi?? hii hapa mashariki ya kati? Siamini kitu kama hicho. Mbona patakuwa padogo sana? hiyo "yerusalemu mpya" ni picha tu bwana ya dunia mpya yenye amani na furaha tele. Au kuna uthibitisho tofauti wa maandiko? halafu hiyo milima na mito watakayokimbilia "waovu" si milima na mito halisi bali njia wanazotumia watu kutafuta msaada wanapopigwa na ghadhabu/misukosuko. "Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso". Sasa hao "waovu" wakati wa mateso badala ya kukimbilia kwa Mungu wanakimbilia kwa vitu vingine. Ndo hivyo vimepewa jina la milima na mapango.
 
Kwakuwa umeuliza kwa imani zote nami nisemi kidogo. Katika uisilam kiama ni siku ngumu kuliko ugumu wowote ambao mwanadamu anaweza waza. Ni siku ya hukumu. Kabla ya kusimama kiama ni wazi kuwa viumbe wote watakafu(wakiwemo maaika wote mpaka mtoa roho-Izraeli).
Kisha watu watafufuliwa kutoka katika matumbo ya ardhi wakiwa katika hali tofauti tofauti.kulingana na matendo yao. Hata hivyo bado siku hiyo itakuwa ngumu sana isipokuwa tu kwa wale waliridhiwa na mola wao.
Hapo ndipo watu watahukumiwa kwa matendo yao. Kuna mchakato mrefu.sana siku hiyo. Hakuna kujuana hapo baba hatamjua mwana wala mwana hatamjua mama. Kila mtu nafsi yake itakuwa imeshughulishwa na mambo yake. Kisha watu watahukumiwa kwa kuulizwa juu ya.yale waloyatenda. Na pindi watakapo danganya,itafungwa midomo yao kisha kila kiungo kipekee kitatoa ushahidi wa kila ulichokifanya.
Kwa wale wanodhani ukifa ndio kiama chako,hakika hawapo sahihi hata.kidogo. Kufa ni katika kitendo cha kufika.mwisho.wa dumia.na mwanzo wa akhera. Kaburi watu watu wataanza kukutana na kheri zao ama shari zao kulingana na matendo yao. Hapo ni adhabu kwa makosa hadi itakapo fika kiama. Na adhanu hii haipunguzi.adhabu atakayoipata mwanadamu siku ya kiama baada ya kuhukumiwa.
Hakika kiama ni siku nzito na tunamuomba Molla wetu atufishe.ili hali yu radhi na sisi ili tuweze kuongoka adhabu zake. Amin.
Ungezungumzia pia yake mateso ya kaburi mkuu!
 
Habari zenu wana JF,

Kuna kitu nimekiwaza na kukitafakari kwa muda wa kama siku 3 hivi lakini bado sijapata majibu yake. Basi nipo hapa kuomba msaada wa kueleweshwa kiundani kwa watu wenye uelewa wa mambo ya kidini awe muislam, mkristo budhaa na hata asiye na dini.

Suala kubwa linalonitatiza ni kuhusu ukweli wa siku ya kiama, jehanamu na pepo. Je kweli hivi vitu vipo kweli? Nikiri wazi kabisa kwamba mimi ni mkristo mkatoliki na nimekua nikifundishwa haya kama sio kukaririshwa toka nikiwa mdogo katika mafundisho ya komunio ya kwanza na kipaimara kwamba kuna hivyo vitu 3 nilivyovitaja.

Yafuatayo ni maswali ambayo najiuliza na ningefurah kama nitapata majibu ya kina na kuridhisha.

1. Je ni kweli kuna siku ya kiama?

2. Na kama kweli ipo kwanini MUNGU aliwaadhibu na kuviangamiza baadhi ya vizazi kwa matendo yao machafu na kutosubiri siku ya kiama?

3. Je hawa walioadhibiwa na kuangamizwa siku za nyuma walikuwa waovu kuliko sisi wa zama hizi?

4. Je hao walioangamizwa wataletwa tena mbele ya hukumu? Na nini hatima yao na ilihali walishaadhibiwa kwa kuangamizwa?


Baada ya kupata ufafanuzi wa kutosha wa maswali hayo nadhani suala la pepo na jehanamu nitaweza kulielewa kwa urahisi.

Inawezekana kabisa kuwa kuna mada kama hii imeshawahi kujadiliwa kama hamtojali naomba kuwekewa link yake.

NB: Nimetumia zama za nabii Nuhu na gharika kuu kuuliza maswali hayo.


Shukrani.
Usipoteze muda na dini hizo si ukiristu wala uislamu wote useless tu
 
all livings things hapa dunian vimeshapitia kihama in a sense of exntiction the major one ilikua the permian exntiction ambayo ilitokea almost miaka milioni 250 iliyopita na almost 96% of species were wiped out.

Kihama cha all mankind katika karne yetu kinaweza kusababishwa na either kimondo chenye ukubwa kuipiga dunia, au vita ya nuclear katika ya nchi kubwa au ugonjwa wowote wa mlipuko unaosababishwa na super virus au bacteria.

Pia kuharibu ozone layer kutokana na uchafuzi wa mazingira kunaweza kuchangia kuleta kihama kwetu binadamu na all land animals. Bila ozone layer ambayo imechukua zaidi ya miaka milioni 120 kutengenezwa kutokana na oxygen ilikuwa inatoka baharini na kufanya chemical reaction na sunrays maisha ya viumbe hai ardhini yasingewezekana kwasababu ya dangerous radiation kutoka kwenye jua.

Lakini kiama cha dunia kama dunia ni almost miaka billion moja ijayo in which jua litakua limetumia hydrogen yake vya kutosha na likisha'exhaust elements zote kama fuel then litapanuka kwa ukubwa in which dunia inaweza kuwa swallowed na gravity ya jua.
 
hukumu(kiama) ya mwanadamu inaanza mara tu baada ya mtu kufa. aliyetubu dhambi na kupatana na Mungu atapelekwa Mbinguni na asiyetubu ataenda motoni. wale wa zamani walioangamizwa sio kwamba ni waovu zaidi yetu bali ni matashi ya Mungu kuchagua njia ya kutunyoosha viumbe wake. ulichofundishwa ktk imani yako ni kweli kabisa, kishike. tenda mema acha mabaya. penda kutubu kila unapomkosea Mungu.

kwa mjib wa biblia kunasiku ya mwisho ambapo yesu atakuja na kutakuwa na parapanda kuu, ambapo itawaamsha wafu na wale watakatifu watamlaki yesu Mawinguni,

waovu wataikimbilia milima, na mito ili wajistiri lakini mito na milima itawakimbia, kutakuwa na kitimtim balaa,

baada ya hapo waovu, watakufa na kusubri hukumu ya mwisho ya kuchomwa moto, kisha yetu atarejea na watakatifu mji wa yeruslem na ndipo waovu watafufuliwa na kuchomwa moto..

kumbuka moto umeandaliwa kwa ajiri ya shetani na malaika zake, wanadam ni kuni tu, kwa kukataa kutii sauti ya Mungu

kuwa sehem ya kumfuata kristo kama bwana na mwokozi wa maisha yako...

Hv nyie mnatumia biblia tofauti au?
 
Haya mambo ya kiroho kwa kiasi kikubwa yana utata sana. Tunaambiwa mtu yaani nafsi anapatikana kutokana na muunganiko wa mwili na roho (pumzi ya uhai) na kwamba mtu huyo anapokufa mwili uoza lakini roho ubaki ikisubiri siku ya kiama. Sasa swali ni kwamba kama kiama kinaanza muda au siku ile mtu anapokufa iweje adhabu iwe ni kwa roho tu na siyo kwa mwili pia wakati kipindi cha kutenda dhambi vilikuwa pamoja?

Na kama mateso yanaanza mara moja baada ya mtu kufa basi ni dhahiri kwamba wale wenzetu waliofariki karne nyingi zilizopita hadi siku ya kiama itakapofika watakuwa wamepata mateso makubwa zaidi (ya muda mrefu) kuliko wale watakao wamekufa miaka michache (mfano mwaka mmoja, miwili kumi n.k.) kabla ya hiyo siku ya kiama. Na kama wakianza kutumikia adhabu zao baada ya kiama hao waliokufa na kupata mateso karne nyingi zilizopita kuliko wengine watapunguziwa adhabu au la?!

Kingine mtu anazaliwa na kudumu duniani kwa dakika, masaa, siku au miaka michache tu lakini siku ya kiama anakuja kutumikia adhabu jehanamu milele! Daah...mimi hata sielewi bana.

majibu ya maswali yako kwa upande wa ukirsto iko hivi ,moja ni kweli siku ya kiama ipo na kwenye biblia inafahamika kama siku ya hukumu soma biblia matahyo 24:14 "tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja"pia siku hii kibiblia inafahamika kama har-magedon soma ufunuo 16:14-16.
majibu ya swali la pili kuhusu kwanini Mungu aliwaangamiza wanadamu wa kipindi cha kwanza bila kusubiri siku ya kiama , ni kweli Mungu aliwangamiza wanadamu hawa bila kusubiri siku ya kiama ilikuwa ni kwa sababu Mungu alitoa agizo kwa wanadamu hawa juu ya nini wanawapaswa kufanya na nini hawapaswi kufanya lakini wanadamu hawa walishindwa kutii agizo hili soma Mwanzo 3:1-4 basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, msile matunda yote ya miti ya bustani? mwanamke akamwambia nyoka matunda ya miti ya bustani twaweza kula lakini matunda ya mti wa katikati ya bustani Mungu amesema msiyale wala msiyaguse msije mkafa ......
majibu ya swali la tatu , sikweli kwamba wanadamu wa Enzi hizo walikuwa na dhambi nyingi kuliko sisi bali wanadamu wa sasa na wakipindi hicho wanafanana kwa matendo na dhambi kinacho wasaidia wanadamu wa sasa ni ule upendo wa Mungu kuelekea ulimwengu huu kupitia damu ya mwanaye Yesu kristo ambapo Mungu aliupenda ulimwengu huu tena soma yohana 3;16
Majibu ya swali la nne kuhusu wanadamu wa Enzi hizo watafufuliwa ili kuhukumiwa ni kweli watafufuliwa tena na kuhukumiwa hukumu ya haki ukiacha ya kipindi kile amabayo iliwakumba hata ambao hawakuwa na makosa au dhambi soma 2petro 4-9


Kabla mm cjakuuliza mjibu huyo hapo juu
 
Hakuna kujuana hapo baba hatamjua mwana wala mwana hatamjua mama. Kila mtu nafsi yake itakuwa imeshughulishwa na mambo yake. Kisha watu watahukumiwa kwa kuulizwa juu ya.yale waloyatenda.
Kwa wakristo kama kuna mwenzetu amefariki ni kawaida sana wakati wa ibada kusikia mchungaji au padri akisema "...ndugu zangu katika kristo mpendwa wetu ametangulia. Lakini tusilie na kuhuzunika sana. Kwa sababu kama mpendwa wetu aliyelala mauti alikuwa mtenda mema, na kama sisi tuliobaki hai tutatenda mema mbele za Mwenyezi Mungu, basi yesu atakaporudi tutakutana na mpendwa wetu mbinguni.....".

Sasa ukiangalia hapo inaonekana kuna kutambuana kipindi hicho. Na kama kuna uwezekano wa kutambuana, najiuliza hakuna uwezekano pia wa kuanza kuwa na vikundi vikundi vya watu waliokuwa wakifahamiana siku nyingi kabla ya siku ya kiama kama wanandugu, marafiki, majirani au staff mwenza na pengine huo ukaribu wa awali ukafikia kuleta upendeleo au ubaguzi fulani miongoni mwa hao wateule mfano hata kupenda kukaa na kuimba pamoja? Je hii hali au sababu nyingine yoyote haitatokea na kuvuruga mpango wa Mungu wa wateule kuishi raha mstarehe milele?

Nauliza hivyo nikijua kuwa kwenye biblia kuna sehemu imeandikwa kuwa mambo yote ya duniani kama wivu, magonjwa yatakuwa yamepita. Lakini ukiangalia historia ya mambo ya Mungu kuna mambo yamekuwa yakibadilika na kuwa kinyume na matarajio au mipango (?) ya Mungu aliyokuwa nayo kabla. Mfano Lucifer (shetani), Adamu na Hawa walitenda dhambi na kuvuruga mipango ya Mungu aliyokuwa nayo juu yao (?).

Anyway, najiuliza tu hayo maswali katika udhaifu wangu wa kibinadamu.
 
Ukisha vika umri wa miaka 18 unakua na uwezo wa kujua jema na baya. Hakuna ajuae siri ya kiama umaut wako ndio kiama chako. Kama unavyojua kua mungu yupo ila hujawah kumwona. Hapa twende kwa hisia. Epuka kutenda mabaya yasiyompendeza mungu wako ili kiama yako usije ukawa kuni upumzike kwa amani
Kwa mujibu wako kiama kipo na silaha ni matendo yako, ila bado hujakidhi majibu ya maswali yangu. Ila yote kwa yote asante kwa muda wako kwa kunidadavulia hayo machache
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom