Naomba kujua maana ya neno Mungu

Naomba kujua maana ya neno Mungu

Kila mtu na kila dini ina maana yake..labda wewe unataka kujua according to who or what religion?
 
tanga2017 naomba kukuuliza maswali yafuatayo?
1. Una miaka mingapi?
2. Unaishi wapi?
3. Unajishughulisha na nini
4. Upo kwenye kundi lipi la kipato juu , chini au kati kati?
 
Nitakupa maana yangu niliyoibuni nilipokuwa mdogo chini ya miaka 10. Nilimuuliza Bibi yangu mzaa Baba: Sisi tumeumbwa na Mungu. Je, Mungu aliumbwa na nani? Mungu alitoka wapi? Na kama hakuna Mungu ndo maana hakuna kitu, kila kitu hakuna kabisa ni utupu (empty) nikaingia ndani nikazama peke yangu nakuambia nilikalibia kuchanganyikiwa. Ebu na wewe waza kama nilivyowaza hata sasa hivi kwamba kama hakuna asili ambayo hiyo asili ilipelekea wewe kuwako na fikilia kwa vile kila kitu kina mwanzo fikilia kuwa mwanzo haupo zama ndani baba/mama hawakuwahi kuwako na wewe automatically usingekuwepo nenda backwards ndani nakuambia utafikia kuchanganyikiwa. Sasa hiyo asili ambayo ukitaka kuiondoa unapelekea ubongo kuchanganyikiwa ndo Mungu. Mungu ndo asili ya kila kitu! Mungu alikuwepo! Ilikuwaje akawepo hakuna hajuaye na ukitaka kumuondoa na kuamini hayupo automatically utachanganyikiwa. Kitu cha kwanza kuumba ulikuwa muda. Muda uliumbwa kwasababu Mungu haishi kulingana na muda. Mungu uishi katika umilele. Kwahiyo uumbaji wote ulianza pale alipoumba muda. Huu muda tunaoujua kwa sekunde, dakika, saa, siku, wiki, mwezi, mwaka, majira, nyakati, n.k. viliumbwa. Fuatilia mwanasayansi anaitwe Stephen Hawking' Anakubali kuwa kitu cha kwanza kuumbwa ni Muda na kwamba Mungu hayupo kwasababu angekuwepo angetakiwa kuwa na muda (time) ya kuumba muda na kwamba muda ulijiumba automatically (big bang). Nahitimisha kwa kusema: Aliyeumba muda ndo Mungu kuanzia pale akaumba kila kitu tukiwemo wanadamu
 
Kulingana na Biblia na lugha ya Kiebrania:
Chochote kinachoabudiwa kinaweza kuitwa mungu,maadamu yule anayeabudu naona ni mungu na kuisifu. Mtu anaweza hata kuruhusu tumbo lake kuwa mungu. (Ro 16:18; Php 3:18, 19) Biblia inataja miungu mingi (Zab. 86: 8; 1Kor 8: 5, 6), lakini inaonyesha kuwa miungu ya mataifa ni miungu isiyo na maana.
 
Mungu ni kitu chochote ambacho mtu anaamua kukiabudu na kukiamini kuwa kitu hicho ama kiumbe hicho kuwa chenyewe ni sababu ya yeye kuwepo, namaanisha kilichomuumba na kilichoumba kila kitu. Sifa kubwa za Mungu ama Miungu ni kuwa huaminika kuwa na nguvu zisizo za kawaida.
 
Nitakupa maana yangu niliyoibuni nilipokuwa mdogo chini ya miaka 10. Nilimuuliza Bibi yangu mzaa Baba: Sisi tumeumbwa na Mungu. Je, Mungu aliumbwa na nani? Mungu alitoka wapi? Na kama hakuna Mungu ndo maana hakuna kitu, kila kitu hakuna kabisa ni utupu (empty) nikaingia ndani nikazama peke yangu nakuambia nilikalibia kuchanganyikiwa. Ebu na wewe waza kama nilivyowaza hata sasa hivi kwamba kama hakuna asili ambayo hiyo asili ilipelekea wewe kuwako na fikilia kwa vile kila kitu kina mwanzo fikilia kuwa mwanzo haupo zama ndani baba/mama hawakuwahi kuwako na wewe automatically usingekuwepo nenda backwards ndani nakuambia utafikia kuchanganyikiwa. Sasa hiyo asili ambayo ukitaka kuiondoa unapelekea ubongo kuchanganyikiwa ndo Mungu. Mungu ndo asili ya kila kitu! Mungu alikuwepo! Ilikuwaje akawepo hakuna hajuaye na ukitaka kumuondoa na kuamini hayupo automatically utachanganyikiwa. Kitu cha kwanza kuumba ulikuwa muda. Muda uliumbwa kwasababu Mungu haishi kulingana na muda. Mungu uishi katika umilele. Kwahiyo uumbaji wote ulianza pale alipoumba muda. Huu muda tunaoujua kwa sekunde, dakika, saa, siku, wiki, mwezi, mwaka, majira, nyakati, n.k. viliumbwa. Fuatilia mwanasayansi anaitwe Stephen Hawking' Anakubali kuwa kitu cha kwanza kuumbwa ni Muda na kwamba Mungu hayupo kwasababu angekuwepo angetakiwa kuwa na muda (time) ya kuumba muda na kwamba muda ulijiumba automatically (big bang). Nahitimisha kwa kusema: Aliyeumba muda ndo Mungu kuanzia pale akaumba kila kitu tukiwemo wanadamu
Hii ya kuwaza kurudi nyuma kwamba vipi wazazi wetu wasingekuwepo na vipi kusingekuwepo na chochote kile katika ulimwengu huu ( empty)....! Huwa na kwama kabisaa....!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaweza kutoa tafsiri juu ya Mungu au miungu inayoonekana. Mfano sanamu,ngo'mbe, viumbe hai wengine kama mizimu,mashetan n.k ambao kwa wanaowaamini wanaita Miungu.

Uhalisia? Mungu mwenyewe hana tafsiri ya kimaumbile,sababu ni uwepo/umbile lisilojulikana/onekana. Zaidi labda anaweza kutafsiri kwa sifa zake na uwezo wake.

Nitakupa tafsiri ya kidini.
Muumba wa mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake vyenye sifa ya uhai na visivyo na sifa na uhai.
 
Back
Top Bottom