Umenikumbusha mbali sana.
Nilipokuwa Moro wakati fulani (nilikuwa katoto) nilitumwa hao nguruka.
Kwa uroho wangu wa samaki na kwa sifa nilizozisikia kuhusu utamu wa nguruka nikaona isiwe case...ngoja nidokoe kabla sijawafikisha home.
Ladha niliyokutana nayo hadi leo nikiwaona najisikia vibaya.
Ilikuwa kama magadi hiviiiiii...
Kufika home nikamueleza mamdogo ukweli kuwa hawa samaki mbona sio watamu kama mnavyowasifu?
Alicheka sana...akaniambia sikupaswa kuwala kabla hawajachomwa.
Daaaah hata alipowachoma na kunipa nilikataa kabisa.