Naomba kufahamishwa kampuni nzuri ya bima za Magari ambao siyo wasumbufu

ghona18

JF-Expert Member
Apr 5, 2013
573
327
Habari Za mchana Naomba kwa mwenye uelewa juu ya makampuni ya bima Za magari anifamishe. Nahitaji kampuni ambayo pindi upatapo tatizo siyo wasumbufu kukulipa. Naomba kiwasilisha
 
Habari Za mchana Naomba kwa mwenye uelewa juu ya makampuni ya bima Za magari anifamishe. Nahitaji kampuni ambayo pindi upatapo tatizo siyo wasumbufu kukulipa. Naomba kiwasilisha
Mkuu naomba nikushauri usikimbilie kwa kampuni ya bima(insurer) bali nenda kwa insurance broker mwenye hadhi na utakuwa salama zaidi.Sababu kuu ni hii, insurance companies zinapata ripoti za claims kila dakika.Unapokuwa umepitia moja kwa moja kwa kampuni ya bima disadvantage ni kwamba claim yako huwa haipati uzito unaotakiwa unless kuna ujanjaujanja unaufanya kwa kupata msaada wa mtu aliye ndani ya kampuni.Advantage ya kupitia kwa broker wa hadhi ya juu ina maana ile claim haiwi jukumu lako kuifuatilia bali ni ya broker.Broker huyu unakuta anamuingizia insurer huyu mwenye kutakiwa kushughulikia claim yako mathalani TZS bilioni 600 na $ 30m kwa mwaka.Huyu broker ni lulu kwa insurance company, insurance company haiwezi kutaka kumpoteza, so ukipitia kwake utambue claim yako itafuatiliwa na kama ukiwa unastahili kulipwa utalipwa pasipo usumbufu.Kama hauja elewa nipo tayari kwa maswali.
 
Mkuu naomba nikushauri usikimbilie kwa kampuni ya bima(insurer) bali nenda kwa insurance broker mwenye hadhi na utakuwa salama zaidi.Sababu kuu ni hii, insurance companies zinapata ripoti za claims kila dakika.Unapokuwa umepitia moja kwa moja kwa kampuni ya bima disadvantage ni kwamba claim yako huwa haipati uzito unaotakiwa unless kuna ujanjaujanja unaufanya kwa kupata msaada wa mtu aliye ndani ya kampuni.Advantage ya kupitia kwa broker wa hadhi ya juu ina maana ile claim haiwi jukumu lako kuifuatilia bali ni ya broker.Broker huyu unakuta anamuingizia insurer huyu mwenye kutakiwa kushughulikia claim yako mathalani TZS bilioni 600 na $ 30m kwa mwaka.Huyu broker ni lulu kwa insurance company, insurance company haiwezi kutaka kumpoteza, so ukipitia kwake utambue claim yako itafuatiliwa na kama ukiwa unastahili kulipwa utalipwa pasipo usumbufu.Kama hauja elewa nipo tayari kwa maswali.

Nashukuru sana kwa mchango wako mkuu Vipi uhakika wa pesa yangu ambapo broker atafilisika au kufa. Naomba kufahamu badhii ya hao broker
 
Insurance broker mzuri ni Ndege Insurance Company, kama ni insurance company basi NICO wapo vizuri
 
Nashukuru sana kwa mchango wako mkuu Vipi uhakika wa pesa yangu ambapo broker atafilisika au kufa. Naomba kufahamu badhii ya hao broker
Mkuu niliposema broker sikumaanisha mtu bali kampuni.Kwahiyo katika mazingira yoyote unapaswa kutambua kuwa wewe utakuwa salama.Hela yako haipo kwa broker mkuu, yeye anapata commission tu, hela ipo kwa anaebeba risk ambaye ni insurer.
 
Nashukuru sana kwa mchango wako mkuu Vipi uhakika wa pesa yangu ambapo broker atafilisika au kufa. Naomba kufahamu badhii ya hao broker
Kuhusu kuwafahamu ni jambo pana kidogo, kwani kampuni zilizosajiliwa kwa commissioner of insurance ni nyingi, ila ni chache ndio zenye uwezo ueledi,uaminifu na uwezo wa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili.Hapa nina maana ya kwamba, brokers wazuri sio tu wale wenye uwezo wa kifedha na biashara, bali pia uwezo wa kitaalamu na kuweza kumshauri mteja kulingana na aina ya bima anayohitaji wakushauri ni kampuni gani iliyo sahihi.Kwani kuna makampuni ya kikanjanja ambayo wao wanacho tazama ni commission kiasi gani wanayopata lwa insurer, hivyo wako radhi kukukatia bima ya kampuni ambayo wanatambua kuwa inasumbua kulipa ikitokea claim ila wao wanapewa commission kubwa katika mauzo hivyo ni faida zaidi kwao,bila kujali wewe kama mteja utakuwa katika usalama upi chini ya mikono ya hiyo kampuni.
 
Kuhusu kuwafahamu ni jambo pana kidogo, kwani kampuni zilizosajiliwa kwa commissioner of insurance ni nyingi, ila ni chache ndio zenye uwezo ueledi,uaminifu na uwezo wa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili.Hapa nina maana ya kwamba, brokers wazuri sio tu wale wenye uwezo wa kifedha na biashara, bali pia uwezo wa kitaalamu na kuweza kumshauri mteja kulingana na aina ya bima anayohitaji wakushauri ni kampuni gani iliyo sahihi.Kwani kuna makampuni ya kikanjanja ambayo wao wanacho tazama ni commission kiasi gani wanayopata lwa insurer, hivyo wako radhi kukukatia bima ya kampuni ambayo wanatambua kuwa inasumbua kulipa ikitokea claim ila wao wanapewa commission kubwa katika mauzo hivyo ni faida zaidi kwao,bila kujali wewe kama mteja utakuwa katika usalama upi chini ya mikono ya hiyo kampuni.

Nashukuru unanipa mwanga Ila ningepanda walau unitajie kampuni (broker) ili tuendele kupata uhakika kutoka kwa wajumbe wengine asante
 
Mkuu, kuna F&P INSURANCE BROKERS,ASTRA INSURANCE BROKERS,ARIS etc..Hata CRDB BANK pia wana kampuni ya insurance brokerage.List ni ndefu mkuu
 
Mkuu naomba nikushauri usikimbilie kwa kampuni ya bima(insurer) bali nenda kwa insurance broker mwenye hadhi na utakuwa salama zaidi.Sababu kuu ni hii, insurance companies zinapata ripoti za claims kila dakika.Unapokuwa umepitia moja kwa moja kwa kampuni ya bima disadvantage ni kwamba claim yako huwa haipati uzito unaotakiwa unless kuna ujanjaujanja unaufanya kwa kupata msaada wa mtu aliye ndani ya kampuni.Advantage ya kupitia kwa broker wa hadhi ya juu ina maana ile claim haiwi jukumu lako kuifuatilia bali ni ya broker.Broker huyu unakuta anamuingizia insurer huyu mwenye kutakiwa kushughulikia claim yako mathalani TZS bilioni 600 na $ 30m kwa mwaka.Huyu broker ni lulu kwa insurance company, insurance company haiwezi kutaka kumpoteza, so ukipitia kwake utambue claim yako itafuatiliwa na kama ukiwa unastahili kulipwa utalipwa pasipo usumbufu.Kama hauja elewa nipo tayari kwa maswali.
Insurance broker mmoja aliniambia hivi hivi sema shida ni kuwa wapo magumashi ambao sometimes hawafikishi hela!
 
Insurance broker mmoja aliniambia hivi hivi sema shida ni kuwa wapo magumashi ambao sometimes hawafikishi hela!
Upo sahihi kabisa mkuu, ndio maana mtu anapaswa kwenda sehemu sahihi.Wapo brokers ambao hata huo utaalamu hawana, ni ujanjaujanja tu.
 
Back
Top Bottom