Naomba kueleweshwa Albadiri na Itikafu

Naomba kueleweshwa Albadiri na Itikafu

Wilson Leguna

Senior Member
Joined
Feb 22, 2017
Posts
104
Reaction score
92
Naomba kueleweshwa kuhusu kisomochenye nguvu zaidi, miaka ya tisini mwanzoni kulikua na mtafaruku wa kidini, na kiongozi mmoja wa serikali akaombewa Itikafu, sio Albadiri, sinus Kama ilimpata
 
Nina maana sijui kama kisomo hicho kilimdhuru...Naomba kuwasilisha...
 
Jirani yetu aliishi na mtoto wa dada yake, dada yake alikuwa na mtoto huyo mmoja tu. Sekondary alikwenda kukaa kwa mama yake mdogo aliiba mkufu wa dhahabu.

Mama mdogo aliuliza nani aliyeiba, kila mtu kimya, aliitwa sheikh baadavya kusoma albadir mtoto alianza kuvimba tumbo mpaka mauti yanamfika
 
Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya kutaka kujikaribisha kwa Mola wake. Itikafu si jambo maalumu lililovumbuliwa na Uislamu, na wala si jambo ambalo lipo kwenye dini ya Kiislam tu, bali jambo hili pia lilikuwepo katika dini mbali mbali zilizopita, kisha ulipokuja Uislamu ukaliendeleza na kulipa nguvu, pia yawezekana kuwa baadhi ya sheria zake zimebadilishwa na dini hii ya Kiislam. Itikafu huwa haina muda maalumu, lakini lililo muhimu na la lazima katika itikafu ni kufunga saumu, kwa hiyo ni lazima mtu anapotaka kukaa itikafu, achaguwe zile siku ambazo zinaruhusiwa kufunga saumu ndani yake. Hivyo basi zama zozote zile ambazo saumu huwa inajuzu ndani yake, itikafu pia itakuwa ni yenye kujuzu katika siku hizo, lakini nyakati bora zaidi kwa ajili ya itikafu, ni zile siku za ndani ya kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani, au ndani ya masiku meupe ya mwezi wa Rajabu. Na kuna sehemu maalum ambazo zinaruhusiwa kufanya ibada hii ya itakafu. Kauli maaru kuhusiana na mahala pa kufanyia itikafu ni kwamba: ibada hii inatakiwa kufanywa ndani ya mmoja kati ya misikiti minne, nayo ni: msikiti wa Makka, msikiti wa Madina, Masjid Kufa na Masjid Basra. Lakini kuna wanazuoni wengine wambao wamesema kuwa: inafaa pia kufanya itikafu katika kila msikiti mkuu wa mji au mahala fulani.
 
Jirani yetu aliishi na mtoto wa dada yake, dada yake alikuwa na mtoto huyo mmoja tu. Sekondary alikwenda kukaa kwa mama yake mdogo aliiba mkufu wa dhahabu.

Mama mdogo aliuliza nani aliyeiba, kila mtu kimya, aliitwa sheikh baadavya kusoma albadir mtoto alianza kuvimba tumbo mpaka mauti yanamfika
Ndo maana hasa ya alal badiri...waliomba alieiba adhurike bila wao kujua nani kaiba...
 
Alal badiri ni kisomo cha kumlilia Mungu atoe hukumu pale unapoona wewe kama wewe umeshindwa.....lakini Mungu atatoa hukumu only kama wewe uko msafi Na uko upande Wa haki...
 
Naomba kueleweshwa kuhusu kisomochenye nguvu zaidi, miaka ya tisini mwanzoni kulikua na mtafaruku wa kidini, na kiongozi mmoja wa serikali akaombewa Itikafu, sio Albadiri, sinus Kama ilimpata
Huyu uliyemtaja ni yule yule wa kabla ya itikaf na baada ya itikaf? Kusoma hujui hata macho huna mkuu?
 
Back
Top Bottom