Sijui niite huu ni ushauri au la..lakini ndio ukweli! Unapohisi kuwa umecheza rafu nyingi, na una hofu sana kupima VVU ujue afya yako...basi mtu wa hivyo ndio mlengwa mkubwa wa kampeni nyingi za kuhusu kujikinga na maambukizi. Huku kujali kote wadau wanakoonyesha, na mabilioni ya shilingi kutumika..ni hasa kwa ajili ya watu wa kundi hili linalojihisi liko kwenye hatari (risk) kubwa ya kupata maambukizi.
Si kila mwenye tabia hatarishi ameambukizwa (japo anajiweKa katika uwezekano mkubwa wa kuambukizwa)...na si kila aliyeambukizwa basi ni mcheza rafu..toa huo unyanyapaa kwanza, kisha ndio utaona kupima maambukizi ya VVU ni jambo la kawaida na lenye manufaa hasa kama kwako ambapo unalenga kubadili tabia na kutulia na kuanzisha familia.
Unapoogopa/unapogoma kupima VVU mapema, fahamu kuwa itakuja tu siku ambapo utalazimika kupima..na mara nyingi ni baada ya VVU kuanza kusumbua, na magonjwa nyemelezi (opportunistic infections mfano TB, Meningitis, Pneumonia etc) yashatia nanga, utalazimika kupima ili uweze pata matibabu stahiki..na katika hali kama hii survival inaweza kuwa 50/50, kwani tayari CD4 ziko chini sana kiasi cha kuanza kuugua magonjwa nyemelezi.
Ni busara kupima mapema kabla hujaanza kupata dalili..ili 'kama' umeambukizwa, basi uanze dawa mapema wakati CD4 cells hazijashuka chini ya kiwango na kabla ya kuchoka kutokana na magonjwa nyemelezi, mara nyingi hapa survival na quality of life is guaranteed.
NB: HAIKUSAIDII KUOGOPA KWENDA KUPIMA SABABU...WENGI WANAOOGOPA KWENDA KUPIMA HUASSUME WAMESHAATHIRKA NA HIVYO KUENDELEA NA TABIA ZAO HATARISHI, NA HIVYO KUAMBIKIZWA HATA KAMA WALIKUWA HAWAJAAMBUKIZWA MWANZO...WENGI WANAOOGOPA KWENDA KUPIMA HULAZIMIKA KUPIMA WAKATI WAMEANZA KUUGUA NA WANAWEZA POTEZA MAISHA KWA KUCHELEWA MATIBABU, WAKATI WENGI WALIOKUWA NA UJASIRI WA KUPIMA MAPEMA WAKIKUTWA NA MAAMBUKIZI HUANZA MATIBABU MAPEMA NA WANAISHI MAISHA MAZURI TU!