Domo Kaya
JF-Expert Member
- May 29, 2007
- 531
- 59
Ndugu yangu kama umeamua kuoa wala usisikirize watu watu wanasemaje, au ndoa nyingine zina matatizo gani, sio kila tatizo linalotokea kwenye ndoa za watu na wewe zikutokee, mie nipo kwenye ndoa mwaka wa nne sasa na sijakutana na tatizo lolote ambalo kabla sijaingia kwenye ndoa watu walikuwa wanahadidhia. Muamini mwandani wako na yeye ajiamini, jiamini mwenyewe na yeye akuamini, mpende, muheshimu... na usiache kumuomba m/mungu, kwani mke bora kutoka kwa mwenyezimungu. Na hakuna kitu kitamu duniani kama ndoa yenye upendo, amani na uvumilivu.