Naogopa kumwumiza ushauri please

Naogopa kumwumiza ushauri please

Mapenzi hayana umri....changamkia fursa twenzetu....watu wanazisaka hizo lol
 
Ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni

Ila najiuliza tu hivi hayo ya umri na shule nk si ndio vitu vya kujua kwa mwenzi kabla ya kuwa wapenzi!!!
 
mkuu Lizzy umesomeka vyema, na nyongeza ndogo hapo juu ingekuwa vyema kama ungetafutwa utaratibu wa huyu mdogo wetu wa miaka 18 akaenda kusoma mbali kidogo na mji anaoishi sasa, lengo ikiwa ni kupunguza mawasiliano na hatimaye kufa kabisa (fimbo ya mbali haiui nyoka), lakini pamoja na hili msisitizo wa kusoma uwe juu zaidi manake ukimkwepa haraka sana anaweza poteza dira afu akanaswa na wale wasio waungwana..
jamani mi naomba jina la super market pamoja na number zake ili wakati huu wa matokeo niendelee kumpa tuition na somo husika ni Biology na ninaahidi kumfundisha vizuri sana na hamtajutia uamuzi wenu!

my take, mara mia umle wewe(Mlanje) mstaarabu than akutane na bad guyz wasio na huruma hata chembe maana hata shule anaweza acha kabisa! au hata kama hutamla kuwa karibu naye ila priority iwe kwenye kumsisitiza asome, kuwa naye utakua umemlinda dhidi ya wenye kiu kama sisi na mabazaziteam!
CC;Lizzy angelita Munkari miss chagga Mlanje
 
Mpunguzie mawasiliano kidogo kidogo na ongeza muda wa nyie kuonana kama ilikuwa kila baada ya siku 2 mnaonana nw fanyeni muwe mnaonana kila baada ya siku 4 then mnazid kupanda mpk siku 6 akiona mawasiliano yanapungua itamfanya na yy achoke vituko vyako kidogo kidogo atapunguza mapenzi na ww maana mapenzi yanajengwa na ukaribu uliopo then baada ya kama wiki tatu hivi unaweza ukamchan live.
 
Wanaume wengi si waungwana kama wewe, la huwa hawajui malengo ya mahusiano ni nini...

Kwa kifupi kabisa ongea naye kwa namna hii hii uliyotueleza hapa jamvini, mwambie malengo yako na challenges uzionazo ambazo kwa hakika zinamuweka nje ya picha...

Najua atapata tabu kukielewa kwa kuwa ni mdogo lakini ukweli huweka watu huru.
 
Hongera baba na Mungu akupatie mke mwema wa kufanana na ww,km wadau walivyosema mwambie ukweli tu huku ukijitoa tararibu.
 
Helo ndugu zangu wanajamii, najua tunaendelea na maisha vizuri.

Mimi ni mwanaume wa miaka 29 niliachana na mpenzi wangu mwaka jana so baada ya muda mrefu kuwa mpweke nilianzisha urafiki na dada mmoja aliyeniambia anafanya kazi kwenye supermarket moja hapa mjini. Baadae nilimtongoza na akakubaliana nami so nikaona vyema na pia yeye anadai hajawahi kulala na mwanaume.

Wiki iliyopita nimegundua kuwa amemaliza form four mwaka jana na ana miaka 18 vitu ambavyo sikujua hapo awali,kiukweli naona nimemzidi sana umri(miaka 11) na pia sihitaji kusubiria amalize mambo yake ya shule maana nafikiria kuoa mapema. Yeye anadai ananipenda sana yaani usiku akipiga simu akakuta inatumika basi analia sana na pia sitaki kumtoa hiyo bikira yake maana najiona sisitahili hiyo heshima bali mtu mwenye mapenzi ya dhati kwake.

Naombeni ushauri wenu jinsi ya kumwambia kwani sifikirii kuwa nae kwanza ni mdogo sana kiumri na pia siwezi kumsubiri amalize shule

Samahani kwa uandishi usio mzuri.
Mwambie mama yake; kwa uungwana wako panda hata ndege kamweleze kama yuko mbali.
 
Jaman wamebak wachache sana km wewe ubarikiwe mpk ushangae juct mwambie ukwel mapema ili ajipange mana ukisubir yatakua mengne bt be wise wen u talk 2 her!
 
Huyo ndio mbomba mtoto bado bado mbichii,unataka kuoa ambao washajichokea!!!!!mchunguze kama ni kweli ana bikra mkague isije kua bikra ya mdomoni,kama unampenda huwezi muacha kisa visababu vyako hivyo
 
muite siku moja.. kaa nae karibu.. andaa mahali ambako mtakuwa wawili peke yenu.. mueleze kwa kinagaubaga nini hasa

unawaza juu ya mustakabali wake wa ki-mahusiano. nadhani utakuwa umechangia kupunguza uvunjifu wa bikra usiokuwa na maana...

hilo tunda ni halali ya atakaemuoa..
 
Dah,
Hii habari yako mkuu imeni-touch balaa sababu umesimulia situation niliyo kumbana nayo.

In short ni wiki 2 sasa toka nimkatie mawasiliano huyu binti simply kwa kuwa sioni future nae kabisa ktk maisha na nimemsihi hiyo bikra yake amtunzie mumewe I don't deserve it at all Yuko Chuo
 
unamfahamu reginald mengi? yule manager wa IPP na mwenye vyeo vingine vinginevyo?

mke wake jackline ntuyabaliwe unamfahamu? yule mwanamziki anaeitwa k lyn?

hivi ushawahi kujiuliza wameachana miaka mingapi? mbona wameoana na watoto wamezaa vizuri tu?

see them..
attachment.php
 
Helo ndugu zangu wanajamii,
najua tunaendelea na maisha vizuri.

Mimi ni mwanaume wa miaka 29 niliachana na mpenzi wangu mwaka jana so
baada ya muda mrefu kuwa mpweke nilianzisha urafiki na dada mmoja
aliyeniambia anafanya kazi kwenye supermarket moja hapa mjini. Baadae
nilimtongoza na akakubaliana nami so nikaona vyema na pia yeye anadai
hajawahi kulala na mwanaume.

Wiki iliyopita nimegundua kuwa amemaliza form four mwaka jana na ana
miaka 18 vitu ambavyo sikujua hapo awali,kiukweli naona nimemzidi sana
umri(miaka 11) na pia sihitaji kusubiria amalize mambo yake ya shule
maana nafikiria kuoa mapema. Yeye anadai ananipenda sana yaani usiku
akipiga simu akakuta inatumika basi analia sana na pia sitaki kumtoa
hiyo bikira yake maana najiona sisitahili hiyo heshima bali mtu mwenye
mapenzi ya dhati kwake.

Naombeni ushauri wenu jinsi ya kumwambia kwani sifikirii kuwa nae kwanza
ni mdogo sana kiumri na pia siwezi kumsubiri amalize shule

Samahani kwa uandishi usio mzuri.

the best thing to do is to tell her the truth, nothng but the truth.. n that will set u free.
 
Kakangu Mungu aendelee kukupa imani hyo mwambie tuh kwamba akazanie masomo na kazi kwanza ili awe na maisha mazuri baadae huku ukiendelea kukaa nae mbali kijanja na kujifanya uko busy coz ukiongeza ukaribu nae itakua ngumu sana kumuacha.. Mungu na akupe mke mwenza coz u deserve kua na mke mwema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom