Wanagawana pale Lumumba ofisi ndogo tu. Hizo sio za kupeleka ofisi kuu. Hakuna shaka yeyote Maccm wamegawana viwanja vya kupuria ngano. Kuna wenye masilaha mazito mzito wao wakaingia kuvuna faru na tembo, mkuu wa kaya kasema anawafahamu kwa majina na anwani zao hivyo wasithubutu kupiga panga mrejesho wao.
Kuna waliowekwa pale hazina, sasa kampeleka Mwingulu kusimamia zoezi kikamilifu, akisaidiwa na yule Bwana wa Madolas na mabunduki na mabastola aliyeibiwa na kimwana kaka Malima. Hao kazi yao ni moja tu, kulinda mrejesho huo wa hazina.
Yote tisa kumi bado, Umeme umepandishwa, Maswi anachekacheka pale bandarini, kuonesha mashine mpya kumbe zimepakwa rangi. Ongezeko lote la umeme ni kuhakikisha njuluku zinaokotwa kila kona. Wanajua 2015 ni ngumu kwa ccm kurudi lakini kama wataweza kugawa njuluku za kutosha kila mgombea akawa na kifuko chake chenye minoti, kwani hapo hakuna Taa kuu kuu wala Tisi, kwani hao kila mmoja atakuwa likizo. Ukichanganya tena na mkuu wa kaya katoa ruksa kuwatenda upendavyo wapinzani. 2015 Rais wa ccm, atapitishwa kwa kura laki moja tu. Nisameheni haya ni mawazo potofu tu. Sidhani kuna mtu mwenye moyo wa kuiba fedha nyingi hivyo. Utto arudie mahesabu