Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,702
Imekua ni kawaida wanaume na wanawake kulaumiana kuhusu nani hasa ambae sio mwaminifu katika ndoa,lakini hebu tujiulize uaminifu tunaouzungumzia ni upi ni ule wa kushiriki tendo la ndoa na mtu ambae sio mwanandoa au kushiriki tendo ndoa kinyume na asie kuwa umefunga nae ndoa?Kwa mujibu wa Abrahamic religion kushiriki tendo la ndo kabla ya kufunga ndoa ni kuzini au kwa lugha nyingine kutokuwa mwaminifu kwa mwanandoa wako mtarajiwa,au pia kushiriki tendo hilo na mtu ambae sio mwanandoa wako ikiwa umeshafunga ndoa,ieleweke kwamba tendo la ndoa ni maalumu nani haki ya mwanandoa wako tu,iwe unae au unatarajia kuwa nae,nikama zawadi umeinunua ukiwa safarini kwa ajili ya mama yako huwezi kumpa mtu njiani kwani sio yake,kwa mtazamo huo kama sio wote basi ni 98%sisi sio waaminifu kwani walio wanandoa wetu leo sio wale tulio lianzisha nao!Nimezungumzia Abrahamic religion coz naamini wengi wa wa member wa JF ni waumini wa dini hizo,na dini hizo ni Ukristo madhehebu yote,Uislam na Rastafarian!