Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Watanzania wengi tuna tabia ya kumpaka mafuta mtu kwa mgongo wa chupa, tunatabia ya kumwonea mtawala na tajiri huruma pale anapokuwa ananyanyasika au ameyumba kidogo lakini hatuna tabia za kulia na watu wazalendo wala wasiokuwa na kitu.
Mzee Membe amekuwa kwenye utawala na amekula mema ya nchi kwa miaka mingi na kipindi chote hicho hakuwa kujishusha na kuwa muungwana wa kuwasaidia maskini na wasiojiweza, hakuwahi kulia na waliolizwa na tawala alizokuwa anazitumikia bali miaka hiyo yote alikuwa upande wa ukandamizaji wa serikali dhidi ya wanannchi.
Leo amekaa pembeni tumeanza kumpa sifa zisizofaa, kumwita membe jasusi nguli bila kutueleza faida za ujasusi wake kwa Taifa ni kudhiaki majasusi Duniani. Kumwita Membe mwanadiplomasia nguli bila kutueleza ubobezi wake kwenye diplomasia ni kuwatukana wanadiplomasia Duniani.
Hakuna Mambo yakimaendeleo kwa nchi yaliyoletwa na mzee huyu ambayo tunayaona na ambayo yanatushawishi kuona kwamba anapaswa kuungwa mkono, huyu amejituliza na kujiunga kundi la wanyonge kwa sababu tu anataka wanyonge wamwinue arudi kileleni lakini akifika kileleni hawezi kuwakumbuka waliomnyanyua.
Angalia jimboni kwake amefanya nini hadi tuseme anafaha kutuongoza kama Taifa.
Hakuna mwanachama aliyelelewa na kukulia kwenye siasa za chama tawala anaweza kulia na wanaolia bali anao uwezo wakupaka mate machoni tukajua analia kumbe anatusindikiza kulia.
Let us be serious na tutoe sifa kwa watetezi wa Taifa letu waliokubali kuteswa kwa ajili yetu na bado wanapigania kutukomboa.
Mwisho, sikubaliani kabisa na kauli ya Jasusi nguli wala mwanadiplomasia nguli ...sifa hizi wapewe waliotenda Mambo ya kulikomboa Taifa siyo kutukandamiza.
Mzee Membe amekuwa kwenye utawala na amekula mema ya nchi kwa miaka mingi na kipindi chote hicho hakuwa kujishusha na kuwa muungwana wa kuwasaidia maskini na wasiojiweza, hakuwahi kulia na waliolizwa na tawala alizokuwa anazitumikia bali miaka hiyo yote alikuwa upande wa ukandamizaji wa serikali dhidi ya wanannchi.
Leo amekaa pembeni tumeanza kumpa sifa zisizofaa, kumwita membe jasusi nguli bila kutueleza faida za ujasusi wake kwa Taifa ni kudhiaki majasusi Duniani. Kumwita Membe mwanadiplomasia nguli bila kutueleza ubobezi wake kwenye diplomasia ni kuwatukana wanadiplomasia Duniani.
Hakuna Mambo yakimaendeleo kwa nchi yaliyoletwa na mzee huyu ambayo tunayaona na ambayo yanatushawishi kuona kwamba anapaswa kuungwa mkono, huyu amejituliza na kujiunga kundi la wanyonge kwa sababu tu anataka wanyonge wamwinue arudi kileleni lakini akifika kileleni hawezi kuwakumbuka waliomnyanyua.
Angalia jimboni kwake amefanya nini hadi tuseme anafaha kutuongoza kama Taifa.
Hakuna mwanachama aliyelelewa na kukulia kwenye siasa za chama tawala anaweza kulia na wanaolia bali anao uwezo wakupaka mate machoni tukajua analia kumbe anatusindikiza kulia.
Let us be serious na tutoe sifa kwa watetezi wa Taifa letu waliokubali kuteswa kwa ajili yetu na bado wanapigania kutukomboa.
Mwisho, sikubaliani kabisa na kauli ya Jasusi nguli wala mwanadiplomasia nguli ...sifa hizi wapewe waliotenda Mambo ya kulikomboa Taifa siyo kutukandamiza.