Nani huwazalisha wanawake vichaa?

Nani huwazalisha wanawake vichaa?

Vituka

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2011
Posts
2,268
Reaction score
1,267
Habari wana MMU,

Nadhani mtakubaliana na mimi kwamba wanawake wasio na akili timamu wanaongoza katika suala zima la uzazi holela. Kuna wamama hapa mjini vichaa, yaani after 2 years ukimkuta hana kichanga basi ni bahati sana. Wengi wao wanazaa sana na nadhani sio kosa lao huenda wangekuwa na akili timamu wangeweza kujizuia.

Kinachonitatiza mimi, ivi nani huwapa ujauzito wanawake hawa? Ni vichaa wenzao wa jinsia ya kiume au ni wanaume wenye akili timamu? Kama ni vichaa wenzao wa kiume, kwa nini wakati mwingine unaweza kuta hapo mtaani hakuna chizi mwanaume lakini unamkuta chizi mwanamke ana mimba?? Hivi inawezekana kweli mwanaume mwenye akili timamu akafanya mapenzi na mwanamke kichaa?

Kuna siku tulijadili hili suala pamoja na wanaume watatu, mmoja akiwa mtu mzima na yule baba alidai kuwa eti kuna dakika fulani chache za uchizi kwa wanaume, na dakika hizo ndizo hupelekea kufikia hatua ya kufanya mapenzi na kichaa, je ni kweli? Alitoa mfano kwamba ukimuweka mwanaume mwenye akili timamu na mwanamke kichaa sehemu 1 kwa muda wa masaa 24, uku yule mwanamke chizi akifanya vitendo vyake vya uchizi mbele ya uyo mwanaume mwenye akili timamu kuwa uwezekano mkubwa sana wa ngono kufanyika. Anadai kwamba mfanya icho kitendo kwa dakika hizo chache huwa hajielewi na fahamu humjia pale anapomaliza kile kitendo, je ni kweli?
 
masharti ya mganga kama unataka kuwa tajiri lazima uzae na kichaa
 
ama kweli kila mwanamke ni mzuri mbele ya macho ya mwanaume.
 
wanaume wenye akili timamu kabisa ndo wanalala nao,tena wengine wana wake na watoto nyumbani,,,,,kuna baba mmoja namfahamu ana utajiri wa kishirikina na sharti lake ni kulala na wanawake vichaa.Mambo mengine ukiyafikiria akili ina stuck.
 
Mwanaume wa kawaida mwenye kudindisha na kutoa manii...

Ata mbwa dume nae anaweza! Vipi binaadam mwenye akili timamu kumuingilia kichaa tena bila kinga ili hali ukijua matokeo yake?
 
Ata mbwa dume nae anaweza! Vipi binaadam mwenye akili timamu kumuingilia kichaa tena bila kinga ili hali ukijua matokeo yake?

Labda tu nikuulize swali...Hivi unadhani ni kwa nini watu wanafanya mapenzi? Au ni nini nia ya kushiriki ngono?
 
Na wakisha zaa nao huwa wanarudi kuchukua watoto? Kweli inawezekana wanaume nao ni machizi, lol!!

sharti ni kuzaa nae tu yule mtoto anakuwa mtoto wa jini .....halafu unajua kumnyang'anya kichaa mtoto si kazi ndogo
 
Kama yule mama mwenye watoto wengi pale chini ya nje ya uzio wa viwanja wa Gymkanah. Huwa najiuliza mpaka leo hivi anazaa na nani vile vitoto vidogo vidogo vingi namna ile.

Yule sio kichaa completely, sometimes anakuwaga very smart kichwani!
 
Acha lugha ya udhalilishaji.Hawa si vichaa ila wana ulemavu wa akili.
Kama ambavyo huwezi kumwita mlemavu wa macho kipofu
Samahani platzoom kwa kuwadhalilisha, sikufahamu kuwa jina mbadala ni Ulemavu wa Akili (UA)
 
Nimesikia zamani alikuwa mwalimu, je ni kweli mkuu?

Nilishawahi kumsikia akihojiwa na ITV siku moja akasema alikuwa mwalimu ila I doubt kwani huwa hamalizii story ya maisha yake na kuishia kulia. Hapo ndio huwa nahakikisha kuwa ana ulemavu wa akili (UA)
 
Back
Top Bottom