Nani Ashinde, nani ataamua mshindi?

mumeshawahi kuona movie inaitwa THE INTERPRETER?

ni movie nzuri ambayo inaelezea jinsi viongozi wanapokua njee ya madaraka na kukusanya watu na kusema anapigania haki na maslahi ya watu! na then akipata madaraka na yeye anakuwa worst of worsts!... watu wengi wanaogopa changes!

most of them people wanaogopa changes in regimes kwasababu inaambatana na visasi!.... usiongelee kuhusu mapinduzi lazima uelewe damu za ndugu zetu wa visiwani waliopotea wakati wa mapinduzi na baada ya mapinduzi!!...
 
mumeshawahi kuona movie inaitwa THE INTERPRETER?

ni movie nzuri ambayo inaelezea jinsi viongozi wanapokua njee ya madaraka na kukusanya watu na kusema anapigania haki na maslahi ya watu! na then akipata madaraka na yeye anakuwa worst of worsts!... watu wengi wanaogopa changes!

most of them people wanaogopa changes in regimes kwasababu inaambatana na visasi!.... usiongelee kuhusu mapinduzi lazima uelewe damu za ndugu zetu wa visiwani waliopotea wakati wa mapinduzi na baada ya mapinduzi!!...

ni wazi kuwa neno "mapinduzi" limekupiga chenga..
 
mumeshawahi kuona movie inaitwa THE INTERPRETER?

ni movie nzuri ambayo inaelezea jinsi viongozi wanapokua njee ya madaraka na kukusanya watu na kusema anapigania haki na maslahi ya watu! na then akipata madaraka na yeye anakuwa worst of worsts!... watu wengi wanaogopa changes!

most of them people wanaogopa changes in regimes kwasababu inaambatana na visasi!.... usiongelee kuhusu mapinduzi lazima uelewe damu za ndugu zetu wa visiwani waliopotea wakati wa mapinduzi na baada ya mapinduzi!!...

So what's ur point, we let u guys eat your loot in peace or what? forget it, as simple as that!! the wave of change is slowly rising!!
 
Nakubali kwamba njia ni mapambano lakini si ni lazima mapambano yenyewe yaongozwe na itikadi ambayo iko wazi na inayoeleweka kwa wale walio mstari wa mbele na wale wanaohamasishwa kujiunga na mapambano yenyewe?

Pengine moja ya sababu kubwa zinazotufanya baadhi yetu kushindwa kushiriki kikamilifu katika mapambano ni kukosekana kwa itikadi ya mantiki ya mapambano yenyewe. Si kila anayeshiriki katika kuifia dini anakuwa anayo itikadi inayomsukuma kufanya hivyo?
 
Nakubali kwamba njia ni mapambano lakini si ni lazima mapambano yenyewe yaongozwe na itikadi ambayo iko wazi na inayoeleweka kwa wale walio mstari wa mbele na wale wanaohamasishwa kujiunga na mapambano yenyewe?

Pengine moja ya sababu kubwa zinazotufanya baadhi yetu kushindwa kushiriki kikamilifu katika mapambano ni kukosekana kwa itikadi ya mantiki ya mapambano yenyewe. Si kila anayeshiriki katika kuifia dini anakuwa anayo itikadi inayomsukuma kufanya hivyo?

Inkosikazi... hili lisikupe shaka.. very soon itikadi ya wazi itajulikana na itakuwa ni kigezo kikubwa cha uchaguzi wa 2010..
 
Mzee Mwanakijiji hili linanipa shaka kwa sababu kwangu mimi muda uliobakia hadi kufikia masanduku ya kura ya mwaka 2010 ni mfupi mno. Itikadi inahitaji kuainishwa mapema na wale wanaokubaliana nayo wajitokeze na kujipembua kwa uelewa wao wa itikadi yenyewe ili waweze kushiriki katika mapmabnao na kuchukua nafasi zao stahili.

Napata taabu kuamini kwamba inawezekana itikadi hiyo ikaibuliwa sasa hivi na kuwekwa bayana na kupatikana muda na nyenzo za kutosha kuuhamasisha umma kuona maana, umuhimu na mantiki ya kushiriki katika mapambano na kuleta mapinduzi stahili hata kama mapinduzi yenyewe ni kupitia katika sanduku la kura.

Ni kwa nini basi itikadi hiyo isiwekwe wazi sasa hivi ili iwe ni moja ya silaha muhimu katika mapambano yenyewe?

Mimi naamini kwamba bila ya kuwa na itikadi ya wazi itakuwa ni vigumu sana kuendesha mapambano kwa sababu wapiganaji wanahitaji kujua falsafa gani inayowaongoza katika mapambano yenyewe na ni nini hatima ya kile wanachokipigania.
 
Inkosikazi.. katika vita ambapo adui amekuzidi kwa idadi, ubora wa silaha na zana za kivita mikononi mwako una vitu vichache sana vya kukusaidia.. the most important one is timing.. so.. timing here is everything..
 
Sawa nakubali kwamba timing ni muhimu sana lakini unafanya mapinduzi ili upate nini? Nina maana lazima kuwepo na malengo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Tuseme tumefanikiwa kukiondoa chama tawala kutoka katika madaraka, jambo ambalo litawezekana kama kweli kuna dhamira ya kweli miongoni mwa wanaoshiriki mapambano, baada ya hapo nini kinafuata?

Nini kitafuata ushindi utakaopatikana katika sanduku la kura? nani tunayemtaka ashinde na kwa sababu gani? Kuna mkataba gani kati ya kundi jipya la watawala watakaokuja kutokana na jitihada zetu za kuwasukuma na kuwashawishi wapiga kura kuleta mapinduzi na umma?

Umma utajihakikishia vipi kwamba kundi jipya (kwa sababu wote hatuwezi kuwa watawala) liwe la viongozi au watawala wataleta mabadiliko ya kweli kama hakuna itikadi ambayo itatumika kama dira ya pamoja ya kutanabahi kama tuliyokubaliana ndiyo yanayotekelezwa? Hapo ndipo panaponipa shida na wala si uwezekano wa ushindi.

Napenda badio kusaidiwa kwani kuna kitu kinanitatiza hapa. Kumbuka kwamba mapinduzi uliyoyaongelea kwa ujumla katika dibaji ya mjadala huu takriban yote yalisaidiwa na ukweli kwamba yalikuwa yameendeshwa katika msingi wa itikadi zilizokuwa wazi kabisa. hata ufashisti ulikuwa na itikadi yake pamoja na kwamba ulishindwa hatimaye lakini uliitikisa dunia kutokana na ukweli huo. Naomba tusaidiane katika hili ndugu yangu.
 
Inko.. that is why I'm saying.. don't worry.. kuna vitu ambavyo inabidi tuchukue wenyewe mikononi.. what is in the workings is something never attempted in Tanzania before.. believe me.. will send shockwaves even to the most persistent critics..
 
Siri kubwa ya wananchi kushinda ni kuelimika.

Vyombo mbalimbali vya habari kama REDIO, TVS, MAGAZETI NA mitandao ya

internet, kama JF, ni silaha kubwa sana kwa watanzania...Kwa mfano halisi,

mimi binafsi nimepata mtazamo-hasi baada ya kukutana na website hii!!!!

Imenibadilisha, NIMEKUWA MPIGANIA HAKI NA USAWA...

Je kule kwenu GUNGULUGWA wana silaha kama hizi?

Shime sote, na kila mtu kwa nafasi aliyo nayo, aanzishe mapinduzi ya

UKOMBOZI WA AKILI.

Naam, umenena.
umefika wakati wa kutoka kwenye internet, Magazeti, TV, Radio, n.k. na kuunda kikosi cha 'ukombozi' cha kwenda vijijini kuelimisha na kuhamasisha wananchi! Wapigania Uhuru wa nchi yetu walikuwa si wasomi kama walivyo wengi humu lakini waliweza kwenda vijijini kuwahamasisha wananchi na kuikomboa nchi kutoka kwa Wakoloni Wazungu wenye elimu na mabavu. Iweje wasomi wa zama hizi washindwe?
Tutoke kwenye internet!
 
Inkosikazi.. katika vita ambapo adui amekuzidi kwa idadi, ubora wa silaha na zana za kivita mikononi mwako una vitu vichache sana vya kukusaidia.. the most important one is timing.. so.. timing here is everything..

Finally!

More importantly finding a thread which connects different angles! The fire will burn!
 
Naam, umenena.
umefika wakati wa kutoka kwenye internet, Magazeti, TV, Radio, n.k. na kuunda kikosi cha 'ukombozi' cha kwenda vijijini kuelimisha na kuhamasisha wananchi! Wapigania Uhuru wa nchi yetu walikuwa si wasomi kama walivyo wengi humu lakini waliweza kwenda vijijini kuwahamasisha wananchi na kuikomboa nchi kutoka kwa Wakoloni Wazungu wenye elimu na mabavu. Iweje wasomi wa zama hizi washindwe?
Tutoke kwenye internet!

Uchaguzi uliopita nilizunguka vijiji zaidi ya 100 katika mikoa mitatu kwa muda wa miezi saba, nikiongelea, kusimamia, na kufudisha elimu ya uraia! Tulifanya kazi na mashirika ya kiserikali, vikundi vya vijana na kimama, shule za sekondari na vyuo. Nilihakikisha mashirika yaliyopewa pesa za ufundishaji yanafanya kazi ipasavyo, na walifanya kazi na wananchi kama mikataba ilivyoainisha!

Lakini macho machache sana yalimetameta kwa hamu na uchu wa mabadiliko kwa maana wafundishaji walikuwa wanatoa elimu ya jumla ya upigaji kura na uraia kwa mifano iliyokuwa haijabeba uhalisi wa mazingira yale.

Kinachohitajika ni zaidi ya neutrality in knowledge sharing, it is about taking position and defining the right direction.
 
Mimi naamini kwamba bila ya kuwa na itikadi ya wazi itakuwa ni vigumu sana kuendesha mapambano kwa sababu wapiganaji wanahitaji kujua falsafa gani inayowaongoza katika mapambano yenyewe na ni nini hatima ya kile wanachokipigania.

Itikadi ni kitu kinachokuwa na hali halisi ya mazingira! Kwa mwaka wa uchaguzi ujao hatuhitaji itikadi - tunatakiwa kutafuta connection of peoples frustrations - you gat make them see the time of change is now, and they have all the power in their votes! Make them believe in the future!

Kitu ambacho kinatakiwa kwa sasa kwa upande wa tanzania ni wagombea kuwa na agenda katika uchaguzi - sio barabara! Sio maji! it is about vision - make people believe in something! change and themselves! Pili, wagombea kupresent facts katika majukwaa - state of development ya jimbo, na mchango halisi wa wangopea waliopita! Tatu kuwa na jeshi - capacity of defining and mobilize new kadas and vote's - hasa, those who have never voted before - and yet get the women in.
 
Petu hapa.. ni lazima watu wapewe kitu wanachotamania, kitu hicho has to be as clear as a crystal; Kitu hicho ni lazima kiteke fikra zao na hamu zao... kiwe defined and articulated kiasi kwamba mkulima wa Bujosa na mlima mpunga wa Kyela na wale wavuao samaka kule Mbamba Bay wanakielewa vizuri kabisa.

Obama alikuja na kitu kinachoitwa "change" aliidefine hiyo change very clearly na kuwa it was more than changine the person at the white house but the change of the very way the american system works. Ilikuwa ni tofauti kama ya mchana na usiku; watu walimuelewa.

So, I believe kama tutangeneza ideology haiwezi kuwa ideology without specificities.. it is has to be an ideology that is sensible, reasonable and more than that it has to be an ideology that is believable and leads to clear achievements. Haiwezi kuwa itikadi ya vitabuni.
 
So, I believe kama tutangeneza ideology haiwezi kuwa ideology without specificities.. it is has to be an ideology that is sensible, reasonable and more than that it has to be an ideology that is believable and leads to clear achievements. Haiwezi kuwa itikadi ya vitabuni.

Tunarudi kwenye wakulima na wafanyakazi - Wakulima na wafanyakazi - Hawa wanapaswa kukumbushwa kwamba nguvu kazi yao inaweza kuwakomboa katika maisha duni. Pia wanapaswa kukumbuka ni muunganiko wa wakulima na wafanyakazi ndio uliowezesha kuutoa utawala wa kikoloni!
Nivyema kuwakumbusha nia ya Uhuru, maadai ya uhuru na kwanini hayajatimia mpaka sasa, lakini dawa ya umasikini ipo jikoni iwapo wakulima na wafanyakazi watasema "sasa imetosha".

Kuwapata wakulima na wafanyakazi, uchambuzi wa kina juu ya masoko ya wakulima ya ndani na nje lazima ufanyike na maswala ya ruzuku yaangaliwe. Kwa wafanyakazi ni bayana kuangalia maswala ya mishahara - si kwa kusema nyongeza itakuwa shilingi ngapi, ila kuangalia mgawanyo na matumizi ya pesa za serikali, na kukosoa sehemu ambazo matumizi hayako sahihi, na hizo pesa zikitumiwa sahihi basi ni lazima mishahara itaongezeka. Mfumo wa huduma za jamii - hasa afya ni tatizo kubwa sana kwa wakulima na wafanyakazi wa chini! kuwa na mpango wa kutatua tatizo hilo wananchi wanaweza kukusikiliza kwa kina.

Pili kunaswala zima la wapiga kura wapya, hawa ndio watakaoleta mabadiliko katika uchaguzi ujao. Hili kundi linahitaji sababu ya kupiga kura. Sijui idadi yao ni wangapi, lakini naamini ni wengi sana - mimi nawaita watu wa kati. Nitabaka lililokanganyika kabisa - kiuchumi, kisiasa, kiitikadi, kimaadili na mapokeo, lakini linashabihiana katika swala moja tu kuchoshwa na uongozi na jinsi inavyoendeshwa. Kama sio wamechoshwa na uongozi, basi wanachukia foleni za barabarani, ame jinsi internet hazifanyi kazi, uduni wa huduma mbalimbali, kutokupandishwa vyeo, wengi wanawivu wa maendeleo - yawe yale ya taifa au ya ubinafsi. Vichwani mwao wanapicha fulani ya tanzania, yawezekana ni ya ndoto, ama ni ya matamania.

Watu hawa wanaona serikali inaendeshwa kihunihuni, haithamini wala kujali uwezo wa taaluma mbalimbali - agenda yeyote ya kuendesha nchi hii kwa ethics na taaluma ni jambo la msingi sana kwao. Iwapo wataonyeshwa uongozi wetu umeshidwa kutoa muongozo wa maendeleo, na ukatoa mfumo mpya utakaojali ufanisi, mahusiano juu ya elimu na mafanikio, basi ujue utapata wapigaji kura wengi.

Hapa kuna makundi mawili ya wapiga kura, kunawale wanaotaka kujua watafanyiwa nini, na wale wanaotamani kuona nchi hii inaweza kubadilika.
 
460>_1805073.jpg


Ni mgongano wa kihistoria ambao ulipaswa kutokea. Ni mgongano ambao hutokea mahali popote panapokuwa na tofauti kubwa kati ya watawala na watawaliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwenye Mapinduzi ya Ufaransa, Mapinduzi ya Marekani na Mapinduzi ya Bolshevik (Urusi).

Ni yale yale yaliyotokea na kusababisha mapinduzi ya Cuba yaliyomuingiza Castro madarakani. Ndiyo! Ni yale yale yaliyotokea pia kwenye mapinduzi ya Zanzibar!

Migongano ya namna hiyo asili yake mara zote ni pale wananchi wanapotambua kuwa hawana usawa na watawala wao na ya kuwa tofauti ya maisha yao na yale ya watawala ni kubwa mno na ya kwamba mwananchi wa kawaida anajikuta hana nafasi yoyote aidha ya kufanikiwa au ya kuweza kuishi maisha yenye utu, usawa, haki na heshima.

Nchi chache zimeweza kupitia mgongano huo kwa njia ya nguvu (kama mifano niliyotoa) au kama ilivyotokea huko Ukraine na Georgia miaka ya karibuni kwa njia ya nguvu ya umma.

Tanzania yetu inapitia mgongano huo katika hatua zake za awali. Silaha ambayo wananchi wanatumia leo hii ni nguvu yao ya hoja na wanatarajiwa kubadilisha serikali yao kwa nguvu ya kura.

Hata hivyo hilo halitakuwa rahisi kwani dalili yote inaonesha kuwa watawala hawako laini kuruhusu mabadiliko makubwa ya kiutawala yenye kupendelea wananchi wa kawaida. Hivyo, mgongano unaendelea. Swali ni nani ashinde? Na ni nani ataamua mshindi!?

Nisikilize:

[mp3]http://mwanakijiji.podomatic.com/enclosure/2009-04-29T23_41_36-07_00.mp3[/mp3]
Tofauti ya maisha kati ya watawala na watawaliwa imeongezeka zadi.tatizo ni kwamba kuna ile mentality ya kwamba thats the way it should be.Nadhani wapiga kura wengi ni wakulima na wanavijiji ambao hawaelewi?Nataka sana kujua demographic ya wapiga kura wa Tanzania.Ningependa sana kujua ni kina nani hao wanaotuchagulia viongozi kwa wingi wao.Hivi ni kweli hao wananchi wana furaha kiasi cha kuirudisha ccm madarakani all the time kwa ushindi wa kishindo?Kwanini tunaona umma unajitokeza kwenye mikutano na maandamano,je umma huo hujitokeza kwenye kupiga kura?
 
Back
Top Bottom