Nani Ashinde, nani ataamua mshindi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
460%3E_1805073.jpg


Ni mgongano wa kihistoria ambao ulipaswa kutokea. Ni mgongano ambao hutokea mahali popote panapokuwa na tofauti kubwa kati ya watawala na watawaliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwenye Mapinduzi ya Ufaransa, Mapinduzi ya Marekani na Mapinduzi ya Bolshevik (Urusi).

Ni yale yale yaliyotokea na kusababisha mapinduzi ya Cuba yaliyomuingiza Castro madarakani. Ndiyo! Ni yale yale yaliyotokea pia kwenye mapinduzi ya Zanzibar!

Migongano ya namna hiyo asili yake mara zote ni pale wananchi wanapotambua kuwa hawana usawa na watawala wao na ya kuwa tofauti ya maisha yao na yale ya watawala ni kubwa mno na ya kwamba mwananchi wa kawaida anajikuta hana nafasi yoyote aidha ya kufanikiwa au ya kuweza kuishi maisha yenye utu, usawa, haki na heshima.

Nchi chache zimeweza kupitia mgongano huo kwa njia ya nguvu (kama mifano niliyotoa) au kama ilivyotokea huko Ukraine na Georgia miaka ya karibuni kwa njia ya nguvu ya umma.

Tanzania yetu inapitia mgongano huo katika hatua zake za awali. Silaha ambayo wananchi wanatumia leo hii ni nguvu yao ya hoja na wanatarajiwa kubadilisha serikali yao kwa nguvu ya kura.

Hata hivyo hilo halitakuwa rahisi kwani dalili yote inaonesha kuwa watawala hawako laini kuruhusu mabadiliko makubwa ya kiutawala yenye kupendelea wananchi wa kawaida. Hivyo, mgongano unaendelea. Swali ni nani ashinde? Na ni nani ataamua mshindi!?

Nisikilize:

[mp3]http://mwanakijiji.podomatic.com/enclosure/2009-04-29T23_41_36-07_00.mp3[/mp3]

http://www.box.net/shared/nfq7nv9lit
 
Napster ni very smart sidhani kama unamtendea haki kucopy jina lake na kulitumia very low like this!

lengo as usual kubadili mada iliyopo... sijui huwa kuna matatizo gani.. tuna safari ndefu kweli.. 'if you don't have anything good to say, don't say anything'.. ndivyo ningemwambia..
 
lengo as usual kubadili mada iliyopo... sijui huwa kuna matatizo gani.. tuna safari ndefu kweli.. 'if you don't have anything good to say, don't say anything'.. ndivyo ningemwambia..

Tatizo bado tu wafungwa wa fikra na nidhamu za woga ndo hiki kinacho tugharimu watanzania siku zote safari bado ni ndefu sana.
 
Kwi kwi kwi kwi!!! kama haya ndio mapambano yaliyoleta mapinduzi Cuba basi kazi ipo.

Hao walalahoi wana uhusiano gani na watu kama JK, Mbowe, Mengi au Rostam? Kwa wao hao viongozi wote ni mafisadi tu ambao wametumia njia mbalimbali mbovu kufikia hapo walipo.

Where is our Castro?

Mapambano ya sasa ni ya makundi yanayopingana kulilia ulaji. Sioni mikakati yoyote ya maana kati ya haya makundi ya kumsaidia Mtanzania wa kawaida.

Wote wanamtumia mlalahoi kama baiskeli tu ya kuwafikisha kule kunakotafunwa resources za taifa letu.

Na sisi wengine tumebaki wapiga makofi kwa kuafuata rangi, ukabila, kufaidika, kuwa karibu na wahusika na hata kutumwa.

Pamoja na kuheshimu gazeti kama thisday lakini sitegemei na sijawahi ona hata siku moja waandike jambo lolote baya kuhusu Mengi, why? Hivyo hivyo magazeti kama Mtanzania au RAI, pamoja na mashambulizi yote dhidi ya RA wao wanaimba nyimbo tu za kumsifia. Kweli utasema waandishi kama hawa ni huru na wapo pale kutetea maslahi ya taifa? Kwa mazingira niliyoyaona hapa siamini.

Huwezi hata siku moja kupata mabadiliko ya kweli kwenye mazingira na watu kama hawa. Tumefunikwa na ushabiki wa kisiasa na watu na jina la mlalahoi tunalitumia kama chambo tu ili tuvue nyangumi au papa.

Kweli mapambano kama haya ndiyo yalileta mapinduzi Cuba? Labda kama tunaota ndoto.
 
lengo as usual kubadili mada iliyopo... sijui huwa kuna matatizo gani.. tuna safari ndefu kweli.. 'if you don't have anything good to say, don't say anything'.. ndivyo ningemwambia..
Hilo tumeshaligundua mkuu, wewe kaza mwendo safari ni ndefu na ngumu.
Dhambi kubwa hapa ni kukata tamaa.
 
Wote wanamtumia mlalahoi kama baiskeli tu ya kuwafikisha kule kunakotafunwa resources za taifa letu.

Na sisi wengine tumebaki wapiga makofi kwa kuafuata rangi, ukabila, kufaidika, kuwa karibu na wahusika na hata kutumwa.
Labda sasa ndio wakati wa kujiyoa huko na kuingia kwenye mapambano, ili tusiendelee kuwa wapiga makofi milele
 
Mwanakijiji, huo mzogo unaokokotwa hapo kwenye picha ni bomu la mbagala au ni gas cylinder?
 
Mimi nina amini kwamba kila mmoja kwa nafasi yake akitaka anaweza kuanza/kufanya mabadiliko. Waliojaliwa uwezo wa kuthubutu kesema na wafanye hivyo; wa kutumia kalamu wafanye hivyo; wa kwenye majukwaa na wafanye hivyo; na kwa ujumla wetu sote tukutane kwenye sanduku la kura ili tufanye hivyo. Kama itakuwa hivyo pamoja na ukweli kwamba hatutaweza kuwa hivyo wote, WATAWALA watatawaliwa na WATAWALIWA!
 
Siri kubwa ya wananchi kushinda ni kuelimika.

Vyombo mbalimbali vya habari kama REDIO, TVS, MAGAZETI NA mitandao ya

internet, kama JF, ni silaha kubwa sana kwa watanzania...Kwa mfano halisi,

mimi binafsi nimepata mtazamo-hasi baada ya kukutana na website hii!!!!

Imenibadilisha, NIMEKUWA MPIGANIA HAKI NA USAWA...

Je kule kwenu GUNGULUGWA wana silaha kama hizi?

Shime sote, na kila mtu kwa nafasi aliyo nayo, aanzishe mapinduzi ya

UKOMBOZI WA AKILI.
 
So long as the ballot box ndiyo njia of choice ya kupata/kubadilishana uongozi, political landscape iliyopo na uwanja wa kuchezea usiosawasawa sioni tukibadilika ki vile.Ushindi utakuwa kwa walewale "tuliowazoea" - wenye nacho kuendelea kupata zaidi na wasio nacho kupoteza hata kile kidogo walicho nacho - ( wenye fedha kuwadanganya walalahoi kwa kuwahonga kanga, kofia, pilau, nguo za ndani n.k)
 
So long as the ballot box ndiyo njia of choice ya kupata/kubadilishana uongozi, political landscape iliyopo na uwanja wa kuchezea usiosawasawa sioni tukibadilika ki vile.Ushindi utakuwa kwa walewale "tuliowazoea" - wenye nacho kuendelea kupata zaidi na wasio nacho kupoteza hata kile kidogo walicho nacho - ( wenye fedha kuwadanganya walalahoi kwa kuwahonga kanga, kofia, pilau, nguo za ndani n.k)

Usikate tamaa!!!! Hakuna dhambi iliyo kubwa zaidi ya kukata tamaa.
 
Kwi kwi kwi kwi!!! kama haya ndio mapambano yaliyoleta mapinduzi Cuba basi kazi ipo.

Hao walalahoi wana uhusiano gani na watu kama JK, Mbowe, Mengi au Rostam? Kwa wao hao viongozi wote ni mafisadi tu ambao wametumia njia mbalimbali mbovu kufikia hapo walipo.

Where is our Castro?

Mapambano ya sasa ni ya makundi yanayopingana kulilia ulaji. Sioni mikakati yoyote ya maana kati ya haya makundi ya kumsaidia Mtanzania wa kawaida.

Wote wanamtumia mlalahoi kama baiskeli tu ya kuwafikisha kule kunakotafunwa resources za taifa letu.

Na sisi wengine tumebaki wapiga makofi kwa kuafuata rangi, ukabila, kufaidika, kuwa karibu na wahusika na hata kutumwa.

Pamoja na kuheshimu gazeti kama thisday lakini sitegemei na sijawahi ona hata siku moja waandike jambo lolote baya kuhusu Mengi, why? Hivyo hivyo magazeti kama Mtanzania au RAI, pamoja na mashambulizi yote dhidi ya RA wao wanaimba nyimbo tu za kumsifia. Kweli utasema waandishi kama hawa ni huru na wapo pale kutetea maslahi ya taifa? Kwa mazingira niliyoyaona hapa siamini.

Huwezi hata siku moja kupata mabadiliko ya kweli kwenye mazingira na watu kama hawa. Tumefunikwa na ushabiki wa kisiasa na watu na jina la mlalahoi tunalitumia kama chambo tu ili tuvue nyangumi au papa.

Kweli mapambano kama haya ndiyo yalileta mapinduzi Cuba? Labda kama tunaota ndoto.

Mapambano si lazima yafanane na yale yaliyotajwa kwani ni tofauti na huu ni muda mwingine. Nafikiri point hapa ni kuwa kuna mapambano ambayo inabidi yaendelee bila kuridi nyuma.

Hao watu uliowataja sitawarudia kwani nimechoka kuwasoma/ kuwasikia kila sehemu wao ni asilimia ndogo sana ukiweka plua wafanyakazi wao na familia zao. Hivyo kutoa mifano ya hao sidhani kama ni sawa. Kile ni chombo binafsi hivyo africa tulivyo kunakuwa na kuingiliwa kwani hata hao waajiliwa wanakuwa hawana msimamo imara kukataa.

SASA HIVI WATU WANA MATATIZO MENGI HIVYO MTU YEYOTE MWENYE UTAJIRI KWAO NI FISADI. KWANI HATA VIJANA SASA WANAONA UKIPOKEA RUSHWA AU KUFANYA DEAL UNAFANIKIW MAPEMA. Lakini ukweli unabaki palepale kuwa kuna mapambano yanaendelea na yataendelea whether you like it or not.
 
Kwi kwi kwi kwi!!! kama haya ndio mapambano yaliyoleta mapinduzi Cuba basi kazi ipo.

Hao walalahoi wana uhusiano gani na watu kama JK, Mbowe, Mengi au Rostam? Kwa wao hao viongozi wote ni mafisadi tu ambao wametumia njia mbalimbali mbovu kufikia hapo walipo.

Where is our Castro?

Mapambano ya sasa ni ya makundi yanayopingana kulilia ulaji. Sioni mikakati yoyote ya maana kati ya haya makundi ya kumsaidia Mtanzania wa kawaida.

Wote wanamtumia mlalahoi kama baiskeli tu ya kuwafikisha kule kunakotafunwa resources za taifa letu.

Na sisi wengine tumebaki wapiga makofi kwa kuafuata rangi, ukabila, kufaidika, kuwa karibu na wahusika na hata kutumwa.

Pamoja na kuheshimu gazeti kama thisday lakini sitegemei na sijawahi ona hata siku moja waandike jambo lolote baya kuhusu Mengi, why? Hivyo hivyo magazeti kama Mtanzania au RAI, pamoja na mashambulizi yote dhidi ya RA wao wanaimba nyimbo tu za kumsifia. Kweli utasema waandishi kama hawa ni huru na wapo pale kutetea maslahi ya taifa? Kwa mazingira niliyoyaona hapa siamini.

Huwezi hata siku moja kupata mabadiliko ya kweli kwenye mazingira na watu kama hawa. Tumefunikwa na ushabiki wa kisiasa na watu na jina la mlalahoi tunalitumia kama chambo tu ili tuvue nyangumi au papa.

Kweli mapambano kama haya ndiyo yalileta mapinduzi Cuba? Labda kama tunaota ndoto.


Inategemea na uelewa wako wa mapambano haya; ni kweli hata hivyo kuwa kwa kiasi fulani (labda kikubwa) vyombo vya habari vina maslahi lakini hili si geni. Huwezi kuhukumu vyombo vya habari kwa kile ambacho hayaandiki as long as kuna vyombo vingine vya habari vinavyoandika. Wingi wa vyombo vya habari unatusaidia kuwa na mawazo tofauti tofauti. Kama hadi This Day waandike habari mbaya za Mengi ndio ujue wako independent au RAI za Rostam basi unajiandaa kwa kuwa disappointed. Mara ya mwisho uliona lini CNN wameandika habari mbaya kuhusu Ted Turner au Fox za Mardox?

Vyombo vya habari duniani pote leo hii vinawakilisha maslahi mbalimbali; maslahi yanayotegemea umiliki wake.

Lakini zaidi mapambano hayaongozwi na vyombo vya habari yanaongozwa na watu walio huru wenye mawazo huru na walio tayari kuchagua upande bila hofu ya kuonekana wanaupendelea upande huo.

Mapambano yetu si lazima yafanane na mapambano mengine; yaliyotokea Afrika Kusini si sawa na yaliyotokea Angola na si sawa na yaliyotokea Msumbiji. Hata hivyo the essence of the struggle is and has always been idential; the inequality between the rulers and ruled; the oppression of the weak and the indeference of the powerful and fueled by the apathy of many.

Kama mtu anaona mapambano haya hayawezekani, siyo au ni ya njozi hana sababu ya kushiriki kwa sababu ni kama watu wa Biblia waliotumwa na Musa kwenda kuichunguza nchi ya ahadi. Wengi waliporudi walileta taarifa mbaya ya kutowezekana kwani mijitu ya huko Kanaani ilikuwa mikubwa, ina nguvu n.k Isipokuwa watu wawili tu, Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni ambao waliangalia changamoto iliyopo mbele yao na kusema it is beatable!

I'll be counted with those two.. and probably a few more people will as well. The majority will ridicule the efforts and will the carry the bad news of "haiwezekani".
 
Back
Top Bottom