Dah! Siasa zikitumika katika uendeshaji wa kesi kama hizi, kamwe hatutapata jibu kamili kuhusu nani alihusika kufanya nini katika sakata hili ambalo linaonekana litawasomba wengi. Kikubwa ni kwamba kama viongozi wetu wanayo nia ya dhabiti ya kuyamaliza mambo haya, basi waziache vyombo husika vifanye kazi za kitaalam na wahusika wote wawepo kujibu walivyohusika. Endapo mmoja kati ya wahusika wakuu atapotea au atakuwa dhoofu kabla ya kusema mchezo mzima ulikuwaje, basi mbwembwe hizi zote za kuwafikisha mahakamani vigogo hawa, itakuwa ni kiini macho tu.