The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 11,100
- 13,698
Japo tunawaona kama watu wawili tofauti, wanasiasa na viongozi wa dini ni kitu kimoja au niseme mapacha walioungana kiunoni. Ukitaka kuliona na kulijua hili angalia yafuatayo:
Wote, huvuna wasipopanda na kupanda wasipovuna. Mfano, wote wanatumia maneno hasa ahadi hewa na za uongo kuwaibia na kuwatuliza wafuasi wao na wahanga kwa ujumla. Wote hutoa ahadi zisizotekelezeka wala kuingia akilini. Wanasiasa uahidi vinono duniani wakati viongozi wa dini uahidi hivyo hivyo peponi. Wote si wana demokrasia. Wanahubiri maji na kunywa mvinyo, unafiki na uongo.
Wote wanawatoza watu fedha na kuzitumia bila kutoa kutaka wala kuwa tayari kutoa maelezo ya zinavyotumika. Wote wanapenda ujiko hata wasipostahili. Pia, chanzo cha dini na siasa ni kimoja, yaani vimeletwa toka ughaibuni kututawala na kutunyonya.
Viongozi wa dini wakisifia watawala, hii siyo kuchanganya dini na siasa bali uzalendo. Wakiwaapisha na kuwabariki, wanafanya vyema. Ila wanapoonya, wanachanganya dini na siasa. Wanasiasa wakichangia shughuli za dini, wanatimiza wajibu wao. Viongozi wa dini wakiwa machawa, ni sawa. Wakikengeuka na kuunga mkono wapinzani, wanachanganya dini na siasa. Kimsingi, dini na siasa vyote ni mifumo ya kikoloni ya kumtawala na kumpumbaza mwanadamu ili kumuibia na kumdhibiti.
Viongozi wakiwapumbaza waumini na kuwasihi waiunge mkono serikali mbovu siyo kuchanganya dini. Wakiwaaminisha wahanga wa jinai hizi kuwa umaskini wao ni wa kuumbwa, wanatenda vyema. Ila wakiwastua wadai haki, wanachanganya dini na siasa.
Wote hujifanya wajuaji hata kwa yale wasiyojua. Na katika hili, hawapendi wala kukubali kupingwa wala kukosolewa. Tuna mashehe waliojigeuza machawa na maaskofu waliokataa uchawa. Wote wanafanya siasa japo wana milengo na makundi tofauti. Kimsingi, dini na siasa vinalala kitanda kimoja na kufanya jambo moja. Hata ukiangalia ukoloni barani Afrika, bila dini, huenda usingefanikiwa haraka na kwa kasi kama iivyotoke
Kiukweli, hakuna kitu kinaitwa kuchanganya dini na siasa bali usanii na gea ya kuwachanganya wahanga wa jinai hizi za kujitakia tulizoletewa na wakoloni.
Wote, huvuna wasipopanda na kupanda wasipovuna. Mfano, wote wanatumia maneno hasa ahadi hewa na za uongo kuwaibia na kuwatuliza wafuasi wao na wahanga kwa ujumla. Wote hutoa ahadi zisizotekelezeka wala kuingia akilini. Wanasiasa uahidi vinono duniani wakati viongozi wa dini uahidi hivyo hivyo peponi. Wote si wana demokrasia. Wanahubiri maji na kunywa mvinyo, unafiki na uongo.
Wote wanawatoza watu fedha na kuzitumia bila kutoa kutaka wala kuwa tayari kutoa maelezo ya zinavyotumika. Wote wanapenda ujiko hata wasipostahili. Pia, chanzo cha dini na siasa ni kimoja, yaani vimeletwa toka ughaibuni kututawala na kutunyonya.
Viongozi wa dini wakisifia watawala, hii siyo kuchanganya dini na siasa bali uzalendo. Wakiwaapisha na kuwabariki, wanafanya vyema. Ila wanapoonya, wanachanganya dini na siasa. Wanasiasa wakichangia shughuli za dini, wanatimiza wajibu wao. Viongozi wa dini wakiwa machawa, ni sawa. Wakikengeuka na kuunga mkono wapinzani, wanachanganya dini na siasa. Kimsingi, dini na siasa vyote ni mifumo ya kikoloni ya kumtawala na kumpumbaza mwanadamu ili kumuibia na kumdhibiti.
Viongozi wakiwapumbaza waumini na kuwasihi waiunge mkono serikali mbovu siyo kuchanganya dini. Wakiwaaminisha wahanga wa jinai hizi kuwa umaskini wao ni wa kuumbwa, wanatenda vyema. Ila wakiwastua wadai haki, wanachanganya dini na siasa.
Wote hujifanya wajuaji hata kwa yale wasiyojua. Na katika hili, hawapendi wala kukubali kupingwa wala kukosolewa. Tuna mashehe waliojigeuza machawa na maaskofu waliokataa uchawa. Wote wanafanya siasa japo wana milengo na makundi tofauti. Kimsingi, dini na siasa vinalala kitanda kimoja na kufanya jambo moja. Hata ukiangalia ukoloni barani Afrika, bila dini, huenda usingefanikiwa haraka na kwa kasi kama iivyotoke
Kiukweli, hakuna kitu kinaitwa kuchanganya dini na siasa bali usanii na gea ya kuwachanganya wahanga wa jinai hizi za kujitakia tulizoletewa na wakoloni.