Nani anamkumbuka Mzee Majambo?

Nani anamkumbuka Mzee Majambo?

Huyo mzee Majambo wako.........alikuwepo Tanzania nzima akiuza karanga.........?.........

Ha ha ha kweli bora umeuliza...wanavyosema ni as if alikuwa anapita Tanzania nzima kuuza karanga
 
Hahaha kwa wale waliyokulia magetini, obay, masaki, mikocheni hawajui khsu mzee hyu ila kwa sisi tuliyokulia uswazi kinondoni shamba tunampata vilivyopita hehehe

watoto wa mama kama Nyani Ngabu hawamjui huyu....
 
Last edited by a moderator:
Hahahaha..yule mzee hata kama ulikuwa kikojozi lazima uache,aisee alikuwa ananipa nightmares mbaya sana,sana sana alikuwa kinondoni ndio alikuwa anapita mara kwa mara......

Mkuu mm nmekulia kino shamba alikuwa anapita sana hadi mitaa kino mjini....ilikuwa shida kwa watoto vokojozi
 
Mkuu mm nmekulia kino shamba alikuwa anapita sana hadi mitaa kino mjini....ilikuwa shida kwa watoto vokojozi

Hayo maeneo ndio alikuwa anapita mara kwa mara,alikuwa tishio kwa watoto...
 
Preta hii sio yenu wa mikoani au wakuja.....hii yetu watoto wa dar tuliozaliwa uswazi! majambo noma,nilikuwa nikimsikia anakuja lazima nikajifiche uvungu wa kitanda!

Duh!!! poleni wa Dar...kwani na wewe ulikuwa kiko...zi???

Nauliza tu maana hapo juu imesemwa alikuwa kiboko yao watoto vikojozi...
 
kwa mtu aliyekaa dar miaka ya tisini lazima uwe unamjua mzee majambo..watu walikuwa wanasema ana nyumba kumi na pia ni usalama wa taifa. haka kawimbo tulitungiwa na mama zetu "mimi majambo nakula watuuu"
 
namkumbua alikuwa akipita chang'ombe wakati huo tulikuwa tukipenda kumtania akigeuka kila mtu anatafuta uelekeo wake
 
kama humjui wee pita tu......waliokulia dar miaka tisini kurudi nyuma acha wajikumbushe......!

Sema waliokulia mwananyamala na maeneo jirani ndo wanamfahamu,sisi tuliokulia kurasini mbona hatumjui. Watu wa mwananyamala ukiondoa bi nyau hakuna ninaemfahamu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom