iron finger
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 358
- 221
John Legend ni gwiji wa mziki toka USA ambaye ni mtunzi na mwimbaji mahiri wa nyimbo za blues.Ni moja kati ya wanamuziki wanaoweza kukufanya utabasamu kwa tungo zake mwanana zenye ujumbe na kubembeleza pia hasa pale unapokuwa na simanzi moyoni iwe ni ya mapenzi au maisha.
Kwa sasa anaweza kuwa ndiye mtunzi anaeongoza kwa mashairi ya nyimbo tamu mpaka kufikia hatua ya rais wa Marekani Obama kujitangaza hadharani kuwa ni shabiki mkubwa wa John.
Mnamo mwaka 2007 alialikwa kutumbuiza katika sherehe za ufunguzi wa mkutano wa chama cha Democratic na kuwakonga Maseneta na Magavana kwa kibao kikali cha "if you're out there".
Sio katika nchi ya Marekani tu bali hata mabara ya EUROPE,ASIA na AFRICA John Legand ana mashabiki kibao wa nyimbo zake nikiwemo mimi.
Baadhi ya nyimbo za legend ninazopenda ni TONIGHT,ALL OF YOU,ORDINARY PEOPLE na SAVE ROOM.
Nani anampenda Legend?
Karibuni
Last edited by a moderator: