Simba haipendi kujifunza mpaka inakuwa imechelewa. Ni bora captain asiwe beki maana inakuwa vigumu kumzonga refa wakati mpira unaendelea pale anapotoa maamuzi yasiyoridhisha.
Pia ni bora tuige wenzetu, captain awe ni mchezaji bora au mwenye thamani zaidi kwenye timu. Yaani anatakiwa awe ni ile robo ya timu uwanjani.
Pia ni vizuri captain awe ana uwezo wa kuzungumza lugha mojawapo ya kimataifa kwa ufasaha ili awe msaada mkubwa katika mashindano ya kimataifa ambayo ndiyo yana changamoto sana za kimaamuzi.
Kwa sasa kuna changamoto ya kiuongozi kwa wachezaji baada ya kuondoka kwa pamoja waliokuwa wanapokezana majukumu ya ucaptain Zimbwe, Malone, Ngoma na Manula.
Dalili zote zinaonyesha atapewa Kapombe maana ndiye senior player aliyebaki na captain msaidizi anaweza kuwa Mpanzu. Wanaweza pia kumpa Kibu kama msaidizi kwa sababu ya uwezo wa kuzungumza lugha mbalimbali ingawa naona hastahili. Upambanaji wake umepungua sana na sidhani kama moyo wake upo sana pale Simba kwa sasa.