Ligogoma
JF-Expert Member
- Aug 27, 2010
- 3,503
- 6,374
Habari wan JF!!!
Hapa ofisini tuna jamaa (mwanaume) kaajiriwa takribani mwaka sasa umeisha, wakati anahama kutoka alikokuwa (Singida) alikuja na mpenzi wake!
Mpenzi wake huyu jamaa alikuwa anakuja kwa ofisi kumfuata mshikaji wake yaani full malovee! Ila cha ajabu baada ya kama miezi minne hapa wakagombana kabisa na jamaa likamtimua nyumbani yule binti ila akapata hifadhi kwa rafiki yake ambaye ni staff mwenzetu na alimfahamu huyu rafikiye kupitia mpenziwe wakati akija hapa kazini!
Kiutani utani jamaa siku hiyo akaropoka `nimempiga chini yule demu.....` bosi wetu akamuuliza, upo serious umemuacha mtoto mzuri na mvumilivu vile? Kumbuka ulivyosota wakati unakuja hapa lakini kakuvumilia leo umeseto unamtosa? Jamaa halikujali likajibu tu ahaa atajua mwenyewe bana!!! Bosi wetu akaongea kiutani kuwa asijekulaumu!!
Baada ya siku kadhaa yule binti kaibukia kwa bosi wetu, anamfuata kazini kama kawa tena bila woga na ninaposimulia hapa wamefunga ndoa mwezi mmoja sasa.
Jamaa yetu anatamani kuacha hata kazi.....kachanganyikiwa yaani hatuelewi tumsaidieje wivu si wivu sijui alikuwa bado na mapenzi nae au inamuuma demu kuolewa hapa hapa tena na bosi wake...hatujui!!
Kuna wanaolaumu demu kuolewa na mtu mwingine hapa hapa kazini kwa mpenzi wake wa zamani na kuna wanaomlaumu bosi wetu kuoa mpenzi wa zamani wa mfanyakazi wake na pia kuna wanaomlaumu staff mwenzetu kumpa hifadhi huyu binti mpaka bosi wetu akapata nafasi ya kuonana nae...yaani hapa vurugu tupu!!!
Sasa wewe mwana JF kwa mtazamo wako, lawama zako zinakwenda wapi? na kwa nini?!!!
Je! Huyu jamaa yetu aliyemtoa mpenzi wake hukooo mikoani na kuja nae hapa na baadae kuachana nae but binti kaolewa na bosi wake halafu binti ndo ana shine ile mbaya sasa hivi......Unamshaurije!!!????
Hapa ofisini tuna jamaa (mwanaume) kaajiriwa takribani mwaka sasa umeisha, wakati anahama kutoka alikokuwa (Singida) alikuja na mpenzi wake!
Mpenzi wake huyu jamaa alikuwa anakuja kwa ofisi kumfuata mshikaji wake yaani full malovee! Ila cha ajabu baada ya kama miezi minne hapa wakagombana kabisa na jamaa likamtimua nyumbani yule binti ila akapata hifadhi kwa rafiki yake ambaye ni staff mwenzetu na alimfahamu huyu rafikiye kupitia mpenziwe wakati akija hapa kazini!
Kiutani utani jamaa siku hiyo akaropoka `nimempiga chini yule demu.....` bosi wetu akamuuliza, upo serious umemuacha mtoto mzuri na mvumilivu vile? Kumbuka ulivyosota wakati unakuja hapa lakini kakuvumilia leo umeseto unamtosa? Jamaa halikujali likajibu tu ahaa atajua mwenyewe bana!!! Bosi wetu akaongea kiutani kuwa asijekulaumu!!
Baada ya siku kadhaa yule binti kaibukia kwa bosi wetu, anamfuata kazini kama kawa tena bila woga na ninaposimulia hapa wamefunga ndoa mwezi mmoja sasa.
Jamaa yetu anatamani kuacha hata kazi.....kachanganyikiwa yaani hatuelewi tumsaidieje wivu si wivu sijui alikuwa bado na mapenzi nae au inamuuma demu kuolewa hapa hapa tena na bosi wake...hatujui!!
Kuna wanaolaumu demu kuolewa na mtu mwingine hapa hapa kazini kwa mpenzi wake wa zamani na kuna wanaomlaumu bosi wetu kuoa mpenzi wa zamani wa mfanyakazi wake na pia kuna wanaomlaumu staff mwenzetu kumpa hifadhi huyu binti mpaka bosi wetu akapata nafasi ya kuonana nae...yaani hapa vurugu tupu!!!
Sasa wewe mwana JF kwa mtazamo wako, lawama zako zinakwenda wapi? na kwa nini?!!!
Je! Huyu jamaa yetu aliyemtoa mpenzi wake hukooo mikoani na kuja nae hapa na baadae kuachana nae but binti kaolewa na bosi wake halafu binti ndo ana shine ile mbaya sasa hivi......Unamshaurije!!!????