Nani aliyemuumba Mungu?

Thibitisha Mungu yupo kwanza.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Nimekuuliza swali kwani hayupo? Sasa ukiniambia nithibitishe kwanza nashindwa kuelewa ni vp nahitajika kuthibitisha kwanza badala ya kujibiwa nilichouliza!
 
Nimekuuliza swali kwani hayupo? Sasa ukiniambia nithibitishe kwanza nashindwa kuelewa ni vp nahitajika kuthibitisha kwanza badala ya kujibiwa nilichouliza!
Utajuaje yupo au hayupo kabla ya kuthibitisha?

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Wewe unadhani kila anayehoji kuhusu Mungu ni "Edward" Hawkins??? 🤣(Stephen Hawkins).
Naanzia hapa, sio "Edward" ni "Richard Hawkins". Hakuna mtu mwenye akili salama anae weza kuhoji au kuuliza ya kuwa "Mola ameumbwa na nani",nasema hivi sababu kila kiumbe kimeumbwa kumjua Mola muumbwa hii inaitwa "Fitrah(Innate Disposition) ".

Mambo ya Stephen Hawkins hayo yako na yeye, sisi tunamjua "Stephen Hawking".
Na ukome kuleta post bila kwanza kuzisoma kwa kina.
Nakuja na hii, post ipo wazi sana, ndio maana mpama muda huu umeshindwa kukosoa nilichokiandika zaidi ya kulalamika na hili huliwezi mpaka unakufa.
Ndiyo maana nasema wewe uli copy- paste BLINDLY post usiyoijua vizuri ndiyo maana huwezi kuitetea hapa, mlete Muhusika wa hiyo post hapa wewe huwezi kuijibu kwakuwa siyo post yako.
Hitimisho lako imeonyesha wazi ya kuwa nilichokiandika nakijua ndio maana ukaamua kuandika ya kuwa sio kila mtu ni "Edward" (Japo umekosea kuandika jina la mkusudiwa).

Pili, hapa ubaonyesha ya kuwa ulivamia mada bila kuielewa ila sasa umeielewa, ndio maana huwezi kukosoa nilichokiandika kabla na baada.
Najua kutoa tarjama (tafsiri) kwako itakuwa ngumu, basi nakusamehe, wewe sasa jibu hayo maswali matatu tu.
Mpaka najiuliza, kwanini hujibu maswali yangu, naishia kucheka sana.

Ajabu wewe unaejua unashindwa kuelezea, na mimi naweza kukukosoa, sababu maana uliyoitoa inakuumbua wewe na inaonyesha ya kuwa "Sophist" ni mtu wa ghishi na mpindishaji maana ndio maana mfano ulioweka pale katika maana uliyo itoa ni kumuhusu "Mwanasiasa".

Maswali yako matatu nimeshayajibu huko nyuma zaidi ya mara moja,ni wewe tu utulize akili usome uelewe.
Kijana mpaka unakufa maana nilizo zitoa na hii uliyoiweka wewe hivi punde kabla ile ya kwanza ambayo hukuweka marejeo hazina tofauti na huwezi kutoa utofauti wa maana hizo.

Sasa unaposemamimi nimechagua maana nyingine, nikikuuliza kwanini wewe hujachukua maana nilizo zitoa mimi ukachukua maana hiyo nyingine ? Japo hazina tofauti katika msingi wa maana ya maneno hayo. Sasa usiwe mjinga mpaka unakuwa kipofu wa moyo na akili, hufikirii.

Ahsante.
 
Nimekuuliza swali kwani hayupo? Sasa ukiniambia nithibitishe kwanza nashindwa kuelewa ni vp nahitajika kuthibitisha kwanza badala ya kujibiwa nilichouliza!
Hana uwezo wa kujibu swali hilo, na hawa huwa wanakimbia wajibi wa kututhibitishia ya kuwa wamejuaje Mola hayupo, zaidi ya wao wanatuachia sisi tunao amini uwepo wa Mola ndio tuthibitishie ila wao wao wanaona hawana wajibu wa kuthibitisha kutokuwepo kwake, huu ni uoga na kukimbia vivuli vyao na kuonyesha kwa namna gani walivyo wajinga.
 


Shida uliyonayo wewe ni kutokukubali kwamba ume copy-paste upuuzi bila kujua, sasa unashikilia na kuutetea huo upuuzi wa Mtu mwingine (eti Mwalimu wako), umekosa mwalimu hadi umnukuu huyo ???.

Eti, Mtu YEYOTE anayehoji kuumbwa kwa Mungu ni Muongo, tapeli nk???-- elimu gani hiyo??-- inapatikana kwenye kitabu gani cha kiislamu??.

Wewe leo unawakilisha jamii kubwa ya Waislamu wenye midomo mikali kama midomo ya Cobra, midomo yenye Sumu ya kujeruhi watu kwa matusi makali.

Sasa angalia hii screen shot uone maana ya asili ya Sophist sio hiyo maana yako ya "kuokoteza" (loose meaning).

 
Kuna ambao wanasema hakuna uthibitisho wa kuweza kujua kuwa Mungu yupo au hayupo ila hawa atheists wanadai hakuna Mungu na hupinga madai ya uwepo wake kwa sababu wao wanajua kuwa hayupo.

Kwahiyo hawa hupinga kwa sababu wanajua hayupo hivyo ni wazi wana uthibitisho wa wanachokijua.
 
Thibitisha Mungu yupo kwanza.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Kwanini unaniambie nithibitishe KWANZA? Kipi nilichosema humu hadi nihitajike kuthibitisha? Mie nimeanza kwa kukuuliza swali wewe kwamba kwani Mungu hayupo?
 
Kwanini unaniambie nithibitishe KWANZA? Kipi nilichosema humu hadi nihitajike kuthibitisha? Mie nimeanza kwa kukuuliza swali wewe kwamba kwani Mungu hayupo?
Sitaki kujadili kwa undani sana vitu ambavyo havina uthibitisho.

Thibitisha Mungu yupo kwanza ili tujadili kwa kina.

Kama huwezi kuthibitisha Mungu yupo, sitaki kujadili hadithi za kufikirika.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Tatizo huvunji hoja,una ruka. Kwahiyo ile maana yako nayo umeokoteza ? Maana inaenda kinyume na hiki ulichokiweka hapa.

Almuhimu ni kuwa bado nasubiri hoja zako.
 
Watuwekee hapa ushahidi wa kutokuwepo Mola muumba.
 
Amina mtumishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…