Nani alikua mkali kati ya Zlatan Ibramovic and Edward Henrik Larsson?

bryan2

JF-Expert Member
Jun 8, 2016
3,323
4,667
1704830898257.png

Zlatan Ibramovic
1704830971379.png

Edward Henrik Larsson

Hawa wote ni miamba ya Soka toka nchini Sweden japo kwao Sweden kuna mdau mmoja wa Sweden aliniambia Wasweden wanampenda sana Zlatan Ibramovic sio ajabu kukutana na Mabango yake nchini Sweden kama yale ya 5g za Yanga dhidi ya Simba.

Ukiangalia takwimu zao hawa miamba kama zinafanana vile kidogo kwa timu walizochezea Larson kapita Celtic, Barcelona pia alikuja pale Man utd kula mafao yake pale Mtaalamu Zlatan naye kapita Barcelona pia alikuja kula mafao yake pale old Trafford.

Uzuri binafsi nimewaona wote wakicheza kwa nyakati zao, wote wameutendea mpira haki, wote wanakubalika sana tu pale Sweden ni kama mabalozi wa Soka kwa sweden.

Napata ugumu sana kutoa Marks zangu je wewe kama mdau wa mpira wa Soka nani alikua mkali zaidi kati ya miamba hiyo miwili.
 
Kuna msweden mwingine anaitwa Freddie Ljungberg,alikua bonge la winger,
Aliwahi kucheza kwenye team kama Arsenal,Westham,Celtic.

Zlatan na Larson naungana na mleta mada,nashindwa kuamua nani alikua bora zaidi ya mwingine.
 
Kwangu ni Ibra kadabra, huyo mtu ni wadunia nyingine linapokuja swala la ufungaji.
 
Back
Top Bottom