Kimsingi Lowasa hafai kuwa Rais wa tz, na hili watu wanatakiwa kutambua kwamba watz ili tuweze kupata zile ndoto za wengi, ni jitihada za kupata wabunge wa kutosha kwa upande wa upinzani, huo ndo ukombozi wetu, viongozi wa UKAWA akiwemo Mbatia, yani inasikitisha sana, wao wanakomaa na Lowasa ambaye kimsingi si msafi sana, wanazembea kuweka nguvu kwenye udiwani na ubunge, wanatambua na kulalamika kila siku kwamba tume haitendi haki, wakati wanataka Urais,
Wamesahau kwamba bunge ndo sehemu pekee ya kutengeneza sheria nzuri ambazo zitafanya tupate hiyo tume huru ya uchaguzi, wanatambua kwamba Urais auhojiwi mahakamani lakini ubunge una hojiwa mahakani, hawa viongozi wetu wa upinzani wengi ni mizigo kweli kweli, Lowasa wakati akiwa ccm tena nafasi kubwa sana serikalini anataka kujidahi kwamba alikuwa hajui kuwa tume si huru? Na kimsingi Lowasa anaipenda tume iliyopo kwa maana moja kubwa, kwamba kama akibahatisha kuingia Ikulu basi na yy ataitumia kwa faida yake na washirika wake, hasingekuwa anaipende asingethubutu kugombea nafasi hiyo.
Ni bora tungebakia na UKAWA original kwa maana kwamba tungepata faida nyingine ya kuongeza wabunge wengi sana, lakini Lowasa kachanganya vichwa vya akina Mbatia na Mbowe, kwa hali hiyo hawana muda na mambo ya ubunge na ukizingatia wabunge wengi watakuwa ni wapya ukilinginisha na hawa wa ccm ni wazoefu na uchumi wao ni mzuri kwa maana ya kupiga kampeni jimbo zima, ss wenzetu upande wa UKAWA itafikia mahala wagombea ubunge watakosa hata pesa ya kufanya kampeni majimboni kwao.
Sasa faida ni ipi, tuongeze wabunge au tuchague Lowasa ambaye atakuwa na wabunge 50 au 60, na je hayo mabadiliko yatakuja vipi? ni aibu kubwa sana sana, ila naamini na hata mm sintopiga kura kwa Lowasa, ntakachofanya ni Makufuri na mbuge wa UKAWA.