geraldkowero1
JF-Expert Member
- Jul 5, 2014
- 1,838
- 647
Hizi propaganda za Johnson Mbwambo ni simulizi nyepesi zisizo na mashiko. Kwanza, kupitia kwa magazeti yake, Mbwambo ana maslahi na CCM hasa hiki kipindi cha kampeni hivyo haishangazi kuwa anapuliza zumari kulingana na matakwa ya mlipaji wake. Hilo liko wazi. Pili, kiuhalisia, Chadema/Ukawa hawajaachana na agenda ya ufisadi (soma Ilani yao!). Tatu, kinachomsumbua Mbwambo (na wenzake) ni hatari ya wazi ya CCM kung'oka katika uchaguzi huu kutokana na Chadema kuachana na siasa nyepesi za kiuanaharakati na kuendesha kampeni yenye dhamira ya kweli ya kuuondoa utawala wa wezi (KLEPTOCRATIC rule) wa CCM madarakani (ambao wananufaika nao). Walichokua daima wanataka ni kuiona Chadema, kama chama kikuu cha upinzani, kinaishia tu kuimba majukwaani: "Ufisadi! Ufisadi!" bila kuwa mkakati wa dhati wa kuing'oa CCM (ambayo ndio mhimili mkuu wa ufisadi) madarakani. Hakika sasa Chadema wameamua. Hawadanganyiki!!
Huyu Mbwambo kama wengi mlivyosoma uzi wake mrefu mtamwelewa ni wazi anakishabikia chama gani na ni kati ya wale wanaosemekana kulipwa kwa kueleweka udhaifu wao. Hawezi kudanganya popote kuwa mgombea wa chadema kwa maana ya ukawa hanadi sera za chama chake kila afanyapo mikutano ya kujinadi. Wote tunaona,kusikia na kusoma pia.Hivyo hivyo hawezi kusema chadema wameachana na kukemea ufisadi na wizi wa hela na rasmali za taifa na lipo pia katika ilani yao aisome na kuacha kuwaaminisha wananchi uongo. Hawezi pia kudai chadema inashabikia ukanda vinginevyo yeye ndie anaefanya hivyo kwani mgombea anaemshabikia wa chama chake wanatoka kanda moja pia. Hatuelezi ni kwa nini mgombea wake anakwepa kujinadi kwa jina la chama chake huku akijua yeye kama yeye hamiliki nchi na ametumwa na chama chenye usajili wa kudumu. Awaeleze watanzania mgombea wao atakavyotekeleza anayowaahidi watanzania ndani ya chama chake kwa mfumo walio nao ambao hana ubavu wa kubadilisha lolote na akabaki salama. Yote anayoeleza majukwaani yanaweza kutekelezwa na chama kilicho nje ya mfumo wao waite wapinzani au kama tungekuwa na mgombea binafsi na sio chama kinachoongoza nchi na serikali kwa sasa yaani ccm. Labda atuambie ccm yake kwa sasa imejiandaaje kulipa IPTL fedha zao kwani toka May mwaka huu wameshaleta barua ya kutaka kulipwa hela za tegeta escrow acc walizogawana eti sio za serikali. Tumeisoma wote humu humu Jf jukwaa hili hili. Naomba wananchi wenye uelewa na wanaotaka maendeleo ya nchi na mwananchi mmoja mmoja wampuuze huyu bwana na ushawishi wake usio na mwelekeo. MABADILIKO UKAWA UKAWA MABADILIKO.