Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
Job Ndugai ni mwanachuo mwenzangu pale UD miaka hiyo.
Mengi yasiyopendeza yamesemwa dhidi yake kwa nafasi aliyo nayo, hasa kwa namna alivyolifuta Bunge na kulifanya kuwa idara ya SerikaliRais kipindi cha uongozi wa Marehemu.
Kipindi cha uongozi wa marehemu, Bunge lilibakia jina tu, lakini halikuweza kufanya kazi yoyote ya kibunge zaidi ya kubakia kuwa kaidara ka Serikali.
Lakini Ndugai huyu hakuwa hivyo mwanzo, na anataka kutokuwa hivyo kwa sasa. Tujiulize, nini kilimtokea hata akawa vile?
Tusisahau kuwa ambaye alitenda kinyume cha utu, imani, na msimamo wake wakati wa utawala wa marehemu, hakuwa pekee yake, walitofautiana tu kwa viwango.
Rais wetu Samia anayesisitiza haki, demokrasia, kodi zisizo za uonevu, hakuweza kutamka hivyo akiwa chini ya marehemu.
Mwigulu ambaye sasa anasema TRA wasiwabambikie kodi wafanyabiashara, hakuweza kunena hivyo enzi za marehemu, tena alimsifia marehemu kama vile ni mtakatifu aliyeshushwa toka mbinguni.
Musukuma anayesema sasa kuwa walionyang'anywa viwanda na utawala wa marehemu walionewa, hakuthubutu hata kuota kama angeweza kutamka jambo hilo. Kila siku bungeni alibaki kuimba mapambio ya kumsifu marehemu.
Kimei anayesema walioonewa na kubambikiwa kodi, Serikali iwarejeshee, akiwa mkurigenzi wa CRDB aliwahi kuidhinishwa kujengwa jengo la ghorofa kijijini Chato wakati hakuna wateja.
Kabudi aliwahi kumwita Magufuli Mungu. Mwanrwi aliwahi kunena kuwa Mungu anatakiwa amshukuru Rais Magufuli. Kangi Lugola alisema Rais Magufuli ni Yesu. Hawa wote, kama kweli wanamwabudu Mungu wa kweli, wanatakiwa wafanye toba ya pekee kwa kukufuru.
Lakini kwa nini hawa wote watende na kunena ya ajabu kiasi hicho? Sisi wengine hatujui, lakini wao waliokuwa karibu na marehemu wanajua kwa undani ilikuwa hatari kiasi gani kutokubaliana na aliyokuwa anayataka.
Kutokana na Ndugai anayoyanena sasa mara kadhaa Bungeni, unapata ujumbe wa aina 3:
1) Anajutia kwa kuunga mkono udhalimu
2) Anataka kuwaomba msamaha Watanzania lakini anakosa ujasiri
3) Anataka ayahitimishe maisha yake katika nafasi aliyo nayo kwa heshima, lakini anajua kuwa aliyoyatenda yamemwondolea heshima na kumfanya aonekane mtu asiye na msimamo, mnafiki, kigeugeu na asiyeaminika.
Kwa kuwa huyu collegemate inamwia vigumu kusema anaomba msamaha kwa kauli ya moja kwa moja, naomba tumsamehe na tumwombe aungane na Mama Samia katika kuhakikisha Taifa linapata katiba iliyo bora. Katiba ambayo vizazi vijavyo vitatenda kazi kwa mujibu wa sheria na katiba bila ya hofu yoyote toka kwa yeyote.
Najua Ndugai amewakera wengi, lakini kwa yale mazuri machache aliyoyatenda, yatoshe kupata msamaha wa mabaya aliyoyatenda. Kumbukeni hapo mwanzo, hata wapinzani walimpenda Ndugai, na siyo Tulia. Alivyorudi toka kwenye tiba, wabunge wengi walifurahia. Hapa kati, aliingiwa na nguvu ya shetani iliyozidi uwezo wa kuihimili.
Namwombea msamaha.
Mengi yasiyopendeza yamesemwa dhidi yake kwa nafasi aliyo nayo, hasa kwa namna alivyolifuta Bunge na kulifanya kuwa idara ya SerikaliRais kipindi cha uongozi wa Marehemu.
Kipindi cha uongozi wa marehemu, Bunge lilibakia jina tu, lakini halikuweza kufanya kazi yoyote ya kibunge zaidi ya kubakia kuwa kaidara ka Serikali.
Lakini Ndugai huyu hakuwa hivyo mwanzo, na anataka kutokuwa hivyo kwa sasa. Tujiulize, nini kilimtokea hata akawa vile?
Tusisahau kuwa ambaye alitenda kinyume cha utu, imani, na msimamo wake wakati wa utawala wa marehemu, hakuwa pekee yake, walitofautiana tu kwa viwango.
Rais wetu Samia anayesisitiza haki, demokrasia, kodi zisizo za uonevu, hakuweza kutamka hivyo akiwa chini ya marehemu.
Mwigulu ambaye sasa anasema TRA wasiwabambikie kodi wafanyabiashara, hakuweza kunena hivyo enzi za marehemu, tena alimsifia marehemu kama vile ni mtakatifu aliyeshushwa toka mbinguni.
Musukuma anayesema sasa kuwa walionyang'anywa viwanda na utawala wa marehemu walionewa, hakuthubutu hata kuota kama angeweza kutamka jambo hilo. Kila siku bungeni alibaki kuimba mapambio ya kumsifu marehemu.
Kimei anayesema walioonewa na kubambikiwa kodi, Serikali iwarejeshee, akiwa mkurigenzi wa CRDB aliwahi kuidhinishwa kujengwa jengo la ghorofa kijijini Chato wakati hakuna wateja.
Kabudi aliwahi kumwita Magufuli Mungu. Mwanrwi aliwahi kunena kuwa Mungu anatakiwa amshukuru Rais Magufuli. Kangi Lugola alisema Rais Magufuli ni Yesu. Hawa wote, kama kweli wanamwabudu Mungu wa kweli, wanatakiwa wafanye toba ya pekee kwa kukufuru.
Lakini kwa nini hawa wote watende na kunena ya ajabu kiasi hicho? Sisi wengine hatujui, lakini wao waliokuwa karibu na marehemu wanajua kwa undani ilikuwa hatari kiasi gani kutokubaliana na aliyokuwa anayataka.
Kutokana na Ndugai anayoyanena sasa mara kadhaa Bungeni, unapata ujumbe wa aina 3:
1) Anajutia kwa kuunga mkono udhalimu
2) Anataka kuwaomba msamaha Watanzania lakini anakosa ujasiri
3) Anataka ayahitimishe maisha yake katika nafasi aliyo nayo kwa heshima, lakini anajua kuwa aliyoyatenda yamemwondolea heshima na kumfanya aonekane mtu asiye na msimamo, mnafiki, kigeugeu na asiyeaminika.
Kwa kuwa huyu collegemate inamwia vigumu kusema anaomba msamaha kwa kauli ya moja kwa moja, naomba tumsamehe na tumwombe aungane na Mama Samia katika kuhakikisha Taifa linapata katiba iliyo bora. Katiba ambayo vizazi vijavyo vitatenda kazi kwa mujibu wa sheria na katiba bila ya hofu yoyote toka kwa yeyote.
Najua Ndugai amewakera wengi, lakini kwa yale mazuri machache aliyoyatenda, yatoshe kupata msamaha wa mabaya aliyoyatenda. Kumbukeni hapo mwanzo, hata wapinzani walimpenda Ndugai, na siyo Tulia. Alivyorudi toka kwenye tiba, wabunge wengi walifurahia. Hapa kati, aliingiwa na nguvu ya shetani iliyozidi uwezo wa kuihimili.
Namwombea msamaha.