Namuonea huruma huyu binti

Nikisema bado umefungwa na vyeti nitaomba tu unisamehe,
Bro maisha hayana kusubili ajora rasmi inawezekana ukawa unapoteza muda kutafuta kazi
Kaa tafakari tafuta ajira mbadala vyeti weka pembeni kwanza utakuja kunishukuru baadae
Usiogope maisha , chukua chombo weka ndani, Kama kakuvumilia kwa wakati huu hata mkiwa pamoja atakuvumilia tu
Usiogope maisha. Cha msingi tafuta ajira mbadala I mean jiajiri.
Afu nikwambie kitu ukioa Kuna matumizi mengi yanapungua
Mfano ilikuwa mwende guest tsh 15k na kuendelea zaidi ya Mara 3 na kuendelea kwa mwezi lakini sasa show zote mjengoni , hiyo hela unafanyia matumizi mengine
 
Njoo veta pata ujuzi uupendao anzia hapo then fungua enterprise,Anza hata na ufundi bomba,then jitolee pale Dawasco from their ukiwa unafanya na Kazi zako binfsi,miradi ya maji itakuchukua,, commit yourself to God and everything will be like a b,c ....
 
Nimejaribu kujiajiri mara kadhaa lakini niliishia kufeli changamoto kubwa za kujiajiri zinazonikwamisha ni mtaji, kukosa uzoefu/ujuzi wa biashara, utunzaji wa hela na tatizo la kiafya(nina shida kidogo ya kusikia vizuri ni ngumu kuwa sharp kwenye biashara mfano kuwasiliana na watu kwa haraka, kutumia simu kwa mawasiliano n.k)
 
Usiusemee moyo wake, usikute umewekeza akili kwenye comment za kina dada wa Jamii forum zile za "tafuta hela" humu wengi wameolewa na kina "SELE" wako wanajitafuta mdogo mdogo mwaka wa kumi wa ndoa ila wanalisongesha mmoja mmoja tu ndo wameangukia dodo na wako busy na miradi huko humu wanakuja kusoma soma weekend tu kwa hiyo ukijishtukia unampa shida na aliyekuamini akakupenda.

Wewe mueleze hali yako ilivyo ataelewa au anaelewa tayari akitaka kitu kama huna mwambie ukweli ! Pia muwe mnazungumzia hali zenu za uchumi sio kuchakatana na kusengenya wengine !

Najua kinachokupa tabu anakuuliza unamuoa lini ? 😂 Na hilo swali likiingia kichwani wewe picha unayopiga ni mahari na harusi gharama zake huku ukicheki muhuni huenda hata jana hujala mjibu hilo swali kulingana na hali yako na umweleze mipango yako kufikia hilo lengo kwa hiyo hata kama utakua unakwama anakua anaelewa kila kitu! Hivyo hivyo huwa wananuna ukijibu mambo bado ila kichwani huwa wanaelewa kabisa hali halisi na demu kama anakuelewa mradi vitu vidogo vidogo muhuni unasolve atasubiri tu !!

Usimkimbie mweleze na umuoneshe ukweli wa maisha yako yalivyo na una mikakati gani hapo mbeleni !
Yakimshinda ataondoka mwenyewe ila usiusemee moyo wake "eti uchumi sijui umekuchumu" mpaka unaanza kujishtukia yeye anajua na anaelewa.
 
Ada ya kulipa nafikiri itakua changamoto na nafasi za kujitolea sasa hivi imekua kama kuomba kazi ya kuajiriwa yaani nazo zimekua na competition kubwa ila nitajaribu kufanyia kazi ushauri wako.
 
-Kwanini uliingia kwenye mahusiano ilihali unajua vyema kuwa hauna kipato cha kuwa na mwanamke kwa muda mrefu.

-Ungeliweka tokea mwanzo kuwa hauhitaji mahisiano ya muda mrefu. Wewe ni chapa ilale mbele.

- Muda mwingine tunajitafutia mikosi laana kurogwa bure.
 
Nimekuelewa mkuu, ingawa sometimes nikimfikiria naumia sana why ameangukia kwangu. I feel like i don't deserve her. Ni juzi tu katoka kaniomba nimuongezee nauli aende kwao karatu kumuona mama ake anaumwa nimemwambia sina hela nikajaribu kuweka mkeka jana nipate hela ya kumpa nauli kuna timu ya bulgaria inaitwa Ludogorets ilichonifanyia nikaingia kulala na maumivu makubwa sana
 
Pamoja na hayo uliyoeleza usikubali kuishi kinyonge wala usiruhusu hofu ya kuachwa ikuandame. Bado una nafasi ya kuanza tena kwa upya na kuangalia wapi ulifeli ili usirudie tena makosa yale yale. Pia mshukuru Mungu kwa kukuletea mtu anayekupenda na kukujali bila kuangalia mapungufu uliyonayo.
 
Mahusiano ya kimapenzi ni hitaji la asili mkuu haichagui masikini wala tajiri
 
Mahusiano ya kimapenzi ni hitaji la asili mkuu haichagui masikini wala tajiri

-Kweli ni hitaji lakini kukidhi kiu ya hitaji lako halikuhitaji kuzunguka na kuumiza mtu moyo. Kuna uwezo wa kumwambia pia kuwa nataka kutuliza haja zangu na kutembea mbele.

- Hivyo ndivyo wanaume marijali wanafanya. Unaweka wazi mipango yako.
 
Msaidie kile unachoweza , hata kama hakitimii anataka 50k wewe mpatie ile unayoweza kuipata hata kama elfu tano na umwambie ukweli ! Kwamba huna hiyo 50k ila nimeweza kupata hii hapa kiasi kidogo kinaweza kukusaidia anaweza kununa au kujisikia vibaya ila ataelewa !!Na siku umepata kikubwa basi mpe kweli. Mahusiano ndo yanavyokwenda haya formula na njia haijanyooka .
 
Usiogope Maisha, yawezekana Milango ya Baraka haifunguki sababu ya kuchelewa Kuoa. Wewe Muoe huyo Binti.

Mwanaume usililie, wewe pambana usichangue kazi. Kijana unakuwa lenge lenge hivo broo.

Kuna dogo la mwaka 1999 lina mtoto mkubwa na halina Ajira (standard 7) lina Maisha na lina Familia.

Miaka 6 iliyopita ume graduate bado unalalamika Mkuu ??

 
Oaneni. Uasherati na uzinzi ni uchafu.
 
Mkuu sijamaanisha kwamba sijishughulishi na chochote. Sio kila mpambanaji anatoboa. Baada ya dhiki ni faraja lakini kuna wengine huwa hawaipati iyo faraja mpaka wanakufa na dhiki zao.
 
Kwani yeye kakuambia kwamba unampotezea muda? Au umeamua tu kumsemea? Au umemchoka?

Kuwa makini,usijedhani kwamba unampotezea muda kumbe wewe ndie wapotezewa muda.

Sent from my M2006C3MG using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…