Namtafakari Mh. Bernard Membe!

Namtafakari Mh. Bernard Membe!

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,535
Wakuu umofia kwenu...................!

Miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini wanaotajwa tajwa kwamba huenda wakajitokeza na pengine kupitishwa kugombe nafasi ya Urais wa nchi hii, ni pamoja na Waziri wa mambo ya nje Mh. Bernard Membe.Ijapokuwa mwenyewe hajatangaza nia, ila zipo dalili kwamba huenda akaishika njia hiyo!.

Binafsi si mfahamu sana Mh.Membe. Ninachojua tu ni kwamba ni waziri wa mambo ya nje wa Tanzania, wizara ambayo ameweza kuiendesha kwa umahiri na busara kweli kweli!.Ninachojua ni kwamba Mh.Membe ni mwanadiplomasia,tena mwanadiplomasia mahiri na hata tabia yake inamtambulisha hivyo.Ni mtu mtaratibu mwenye busara, busara ambayo ameidhihirisha wazi katika kushughulikia misuguano kadhaa kati ya Tanzania na nchi nyingine.Zaid ya hapo, binafsi simjui sana mwanasiasa huyu.

Ningependa kufahamu yafuatayo kutoka kwa wadau.

1. Je! Mh. Membe ana kashfa yeyote ya ufisadi?

2. je! ana kashfa yeyote katika suala la maadili ya uongozi?

3. Je! ana kashifa yoyote ya kijamii?

Kama hayo yote hana, ningependa kujua historia yake ya kiuongozi pamoja na elimu yake.

Ninachojaribu kuwaza ni kwamba, ikiwa CCM, Watampitisha mwanasiasa ambaye ni msafi na hana kashfa,mwanasiasa mwenye elimu nzuri, upeo mpana, na uzoefu wa uongozi, basi huenda uchaguzi wa 2015 ukapendeza sana sana! Mara huku kasimma Zitto, Mara kule kasima Membe au sijui nani......!.mara kule kasima yule! Basi tutarajie kuona mijadala mikali kwenye TV n.k, mijadala itakayojikita juu ya uchumi, masuala ya kijamii na masuala ya kimataifa ambayo itakuwa inatawaliwa na weledi mkubwa kulingana na upeo wa wahusika. Hii itakuwa ni bora kuliko kusikia siasa za mipasho mara fulani kahongwa na fulani, mara fulani kafanya vile, mara......!: siasa ambazo kwa sasa hazina tija tena.
 
Hana kashifa,anazo sifa toshelezi za kuiongoza tanzania ,ni mweledi wa siasa za uchumi na maendeleo kitaifa na kimataifa.
 
Hana kashifa,anazo sifa toshelezi za kuiongoza tanzania ,ni mweledi wa siasa za uchumi na maendeleo kitaifa na kimataifa.
Yeah! kwa sababu ndio natafakari kwamba kama ikitokea CCM, wakipitisha mtu kama huyu, hoja kama vile "Ufisadi" ambayo kuna watu wameishikilia hiyo peke yake hata kuiingiza pasipo husika hatimae haitofanya kazi kwa kuwa muhusika hoja itakuwa haimuhusu.Halafu kwa busara za muhusika, itakuwa ngumu kumtengenezea Zenge kama alilotengemezewa Zitto, hivyo ni lazima apate wapinzani wa level yake vile vile ili siasa inoge!.
 
endelea kumtafakari ukimaliza uanze kumtafakari na Lowassa.
2015 utashangaa anapita kwa kasi ya kimbunga zaidi ya Katrina
 
Wewe mtaje Bernard Membe na umahili sijui wa intelijensia na diplomasia, kwa taarifa yako kuna mtu atatokeza wala alikotoka hapatajulikana isipokuwa ni July mwakani 2015 ndiyo utamjua Membe kuwa anasdindikiza watu wengine
 
Haya maajabu eti Membe hana kashfa!!
Kuna mwanaCCM yoyote Nguli anayetaka urais asiye na kashfa?

Kwa mfano kuhusu Membe:
1/Mahakama yetu ya Kadhi kwetu sisi waislam imeishia wapi? Misikitini tulimwona sana Membe akija kujipendekeza alipowekwa chini na 'Wagalatia' kupitia maaskofu wao, tukaona amenywea!!

2/Zile pesa alizohongwa(Alipewa?!) na Gadafi zilikuwa za nini na amezipeleka wapi? Si alisema Gadafi ni rafiki yake wa karibu na angemtumia kuwasadia wananchi wa Kusini, vipi zile Pesa?

3/Pesa za chenji ya Rada ziko wapi? Si alisema atakufa nazo, vipi mbona Kimya? Katulizwa? Hiyo Akaunti ya hizo pesa iko wapi? Mbona vitabu havipo mashuleni? Au Oxford wamegoma kuvichapisha?

4/Siasa za Misikitini na Fitna zake huku Lindi ameshaziacha, yeye kazi yake ni kununua mashekh ili wampigie makofi na kumsema vizuri huku Kusini ili iweje?

5/Membe ameshaacha Siasa za 'kichawi'(Fitna za CCM) tena kwa wanaCCM wenzake? Kwani alishamwomba msamaha Mudhihir, Hawa Ghasia nk? Mbunge wa jimbo la Mtama lakini kutwa anakesha kufitini wananchi wa jimbo la Nchinga, Lindi mjini nk.

6/Zile Pesa za mradi wa viwanda vya Saruji kule Kusini ziko wapi? Si alisema ni yeye mwenyewe pekee mwenye uwezo wa kuvijenga? Kwani amebadili mawazo au umezirudisha kwa wahisani au amezitoa sadaka kama anavyofanya Fisadi Lowassa makanisani na Misikitini kwa jina za marafiki zake?

7/Siasa za kutumia madhabahu za makanisa ameiga kutika Monduli au ni Original version yake? Akiwa rais ataacha au ataendeleza ili 'wagalatia' waendelee kuzugwa?

8/Ilikuwaje akabadili msimamo wa Gesi ya Mtwara na kuwasaliti wananchi wa kusini.
Mwanzoni walikuamini uliposema Gesi itabaki Mtwara lakini Mwishoni ukawageuka na kusema Gesi lazima iende Dar na Msoga ifike, ukawaacha wananchi wa Mtwara wakipata kichapo cha JWTZ, ulikaa kimya kama maji mtungi, vipi ni woga tu au ni zile Pesa kutoka China kwenye ile akaunti yetu kulee......

*Ni UCHAFU mtupu kwa mwanaCCM mwenye akili timamu kumshabikia Lowassa, Membe au Sitta ili awe mgombea urais wa CCM 2015.
 
Mleta mada bwana umekuja kijanja kupiga debe mwanzo unajua kua ni mwanadiplomasia mzur,mahiri mwisho unataka kujua elimu yake debe ili
 
Wewe mtaje Bernard Membe na umahili sijui wa intelijensia na diplomasia, kwa taarifa yako kuna mtu atatokeza wala alikotoka hapatajulikana isipokuwa ni July mwakani 2015 ndiyo utamjua Membe kuwa anasdindikiza watu wengine

CCM kwa kuli-cycle ........ wewe unatuambia kuna mtu atatoka wapi?? Thubutu!! Ni hawa, hawa unaowajua. Unamkumbuka yule mama Maghembe wa UN aliyetaka kugombea 1995 ......... Nyerere akamtoa machozi alimtoa machozi mbele ya watu!! Kwa CCM, Rais hawezi kupatikana kama alivyopatikana Prof. Muhongo ............. Hizo sahau. CCM ina wenyewe bwana...!!
 
Kwa hiyo sasa hivi kutokuwa na kashfa ni sifa ya kuwa rais TZ? Only in TZ.
 

...., basi huenda uchaguzi wa 2015 ukapendeza sana sana! Mara huku kasimma Zitto, Mara kule kasima Membe au sijui nani......!..

betlehem

Kwa katiba ipi ndugu yangu? Maana hata kwa Rasimu hii hawezi kugombea hata Ubunge maana kashamaliza miaka 15 na pia hajafika miaka 40.

Au unazungumzia Udowani na Uenyekiti wa mtaa? kama ni uenyekiti wa Mtaa mbona unafanyika 2014 na sio 2015 ?
 
Last edited by a moderator:
Fuatilia mwenyewe jimboni kwake tangu alipoanza jugombea Ubunge mwaka 2000 ndo utajua kama anahonga wapiga kura na kuwnunua wapinzani wake au anapita bure. Kwa kifupi hakuna mgombea waCCM anayeshinda bila rushwa.
 
CCM kwa kuli-cycle ........ wewe unatuambia kuna mtu atatoka wapi?? Thubutu!! Ni hawa, hawa unaowajua. Unamkumbuka yule mama Maghembe wa UN aliyetaka kugombea 1995 ......... Nyerere akamtoa machozi alimtoa machozi mbele ya watu!! Kwa CCM, Rais hawezi kupatikana kama alivyopatikana Prof. Muhongo ............. Hizo sahau. CCM ina wenyewe bwana...!!
CCM ina wenyewe lakini nachokuambia take my words Membe,Sitta,Mwekyembe,Magufuli,Nchimbi hawawezi kuwa marais wa Tanzania,kama huniamini subiri utaona.Ni kweli watatoka CCM lakini hao niliowataja hawamo kwenye list.Tena wewe unaonekana unamuandermine sana Lowasa lakini nachokuambia Lowasa ana nafasi kubwa kuliko hao niliokutajia
 
Ni mpole mno...atakuwa kama anayeondoka; kifupi ni DHAIFU
 
Ingelikuwa ni mimi hawa wanaotoana jasho wote ningewasahau kabisa.Wakati ule wa wa kujenga ukomunist USSR, Lenin aliacha sokomoko la Stalin na Trosky bila kulitatua kabla ya kufa. Kilichotokea ni kwamba Stalin grabbed power by force and exiled Trosky. Stalin was the man of steel...he made USSR a super power by unimaginable cost of human life!
 
so whaaaaaaaaaaaaaaaaaat!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom