Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 21,239
- 36,274
Habari zenu,
Yaani.leo jumatatu, kwa yaliyonikuta hata napata nguvu na utashi wa kuandika hapa..... acha namshukuru Mungu.... acha niimbe siku nzima leo. Ushuhuda baadae.
Ni kwa Neema tuu na Rehema.
Update:
Habari za muda wa ndugu, poleni kwa kuwaweka hewani. Ilinibidi kuweka uzi asubuhi kwa namna ile sababu sikuwa na muda.
Kasie amekuwa mtu wa matukio sana, na mengi yapo huyaleta humu.
Kilichotokea leo asubuhi ni kuwa, huku kazini kulikuwa na fukuto la mabosi kuondoshwa kazini, sasa ikatokea fitina. Msione hivi mjue hata wazungu nao wanafanyiana fitina na mizengwe, immediate supervisor wangu na bosi walikuwa kwenye hali hata ya kutimuliwa kwenye kampuni sababu ya fitina tuu wala hakuna kosa la kiutendaji.
Kwanza kitengo chetu ndo huwa kinachangia faida kubwa kwenye kampuni. Sina. Leo tumekuwa surprised kitengo chetu tumepewa barua za nyongeza ya mshahara, posho ya makazi usafiri na mawasiliano. Wale waliokuwa wanaleta fitina wamepewa barua za warning kwa utendaji mbovu. Si kuwa nafurahia wao kuonywa bali sikutegemea jamani looh, nnavopenda kusafiri na kula bata walaah ntakuwa kifutu kwa furaha.
Jambo moja likanijia, mie ni mkristo, huku SA nasali kanisa la walokole napenda sana kuimba na kuabudu na huku ibada yao asilimia 70 ni kuimba na kuabudu. Nikipata off nikija bongo ntaenda kufufua kadi yangu ya sadaka kanisani niwe naweka zaka na fungu la kumi kuanzia sasa. Maana kama Mungu amenitendea haya bure wacha sasa nami nirudishe shukrani walau kwa kadri alivyonibariki.
Pia ntaongeza kiasi cha akiba nnayotenga kwa ajili ya kujiandaa kustaafu. Zinazobaki ni kutumbua tuu.
Kutoka moyoni namshukuru Mungu.
Nna furaha sanaa.
Kasie Cough Kasiba.
Yaani.leo jumatatu, kwa yaliyonikuta hata napata nguvu na utashi wa kuandika hapa..... acha namshukuru Mungu.... acha niimbe siku nzima leo. Ushuhuda baadae.
Ni kwa Neema tuu na Rehema.
Update:
Habari za muda wa ndugu, poleni kwa kuwaweka hewani. Ilinibidi kuweka uzi asubuhi kwa namna ile sababu sikuwa na muda.
Kasie amekuwa mtu wa matukio sana, na mengi yapo huyaleta humu.
Kilichotokea leo asubuhi ni kuwa, huku kazini kulikuwa na fukuto la mabosi kuondoshwa kazini, sasa ikatokea fitina. Msione hivi mjue hata wazungu nao wanafanyiana fitina na mizengwe, immediate supervisor wangu na bosi walikuwa kwenye hali hata ya kutimuliwa kwenye kampuni sababu ya fitina tuu wala hakuna kosa la kiutendaji.
Kwanza kitengo chetu ndo huwa kinachangia faida kubwa kwenye kampuni. Sina. Leo tumekuwa surprised kitengo chetu tumepewa barua za nyongeza ya mshahara, posho ya makazi usafiri na mawasiliano. Wale waliokuwa wanaleta fitina wamepewa barua za warning kwa utendaji mbovu. Si kuwa nafurahia wao kuonywa bali sikutegemea jamani looh, nnavopenda kusafiri na kula bata walaah ntakuwa kifutu kwa furaha.
Jambo moja likanijia, mie ni mkristo, huku SA nasali kanisa la walokole napenda sana kuimba na kuabudu na huku ibada yao asilimia 70 ni kuimba na kuabudu. Nikipata off nikija bongo ntaenda kufufua kadi yangu ya sadaka kanisani niwe naweka zaka na fungu la kumi kuanzia sasa. Maana kama Mungu amenitendea haya bure wacha sasa nami nirudishe shukrani walau kwa kadri alivyonibariki.
Pia ntaongeza kiasi cha akiba nnayotenga kwa ajili ya kujiandaa kustaafu. Zinazobaki ni kutumbua tuu.
Kutoka moyoni namshukuru Mungu.
Nna furaha sanaa.
Kasie Cough Kasiba.