Namshauri Nape aache visasi

Namshauri Nape aache visasi

Jamani hivi kweli mafisadi ni lowasa, chenge na rostam tuu??

Je mramba, wereme, zakia, mkapa, yona na rais mwenyewe jakaya.. Hawa wote ni mafisadi tu..

Nape nadhani ametolewa kafara na ccm ili aropoke tu na kudai wanajivua gamba... Ccm kujivua gamba ni ngumu sana kwani kimeshakufa siyo leo...

Na nape asipoangalia yatamkuta kama ya wenzie ambao wameropoka na ilipofika siku wakafa kabisa....
 
Hilo ni gamba jingine ambalo wanatakiwa kulivua pia. JK ndio namba moja kwa visasi sasa Nape unataka awe vipi?
 
Mkuu ni kweli NAPE anafanya kazi yake vizuri kwa kubwabwaja kila siku kwenye vyombo vya habari kuhusu hoja moja tu ya RACHEL,
LAKIni JE , katibu mwenezi (NAPE) anapojaribu kukisemea chama chake wakati akiwa na upungufu wa ushahidi wa hayo anayoyasema , au anacheza muziki wa Dr slaa , maana hakuna hata siku moja CCM waliyowahi kusema kwa nini wanawahita hao jamaa (RACHEL) magambo?
maana kila kukicha watu wanamshambulia Dr slaa, lakini kwa upande mwingine wanawachukulia hatua aliowatuhumu kwa ufisadi!!!!!
sasa ccm hao jamaa ni magamba kwa mpango upi?
mimi nadhani Dr slaa anastahili heshima yake mkuu
- Mkuu sana kwani kazi ya Katibu Mwenezi wa chama cha siasa ni nini hasa? Hebu weka wazi hilo kwanza halafu ndio utoe hukumu, Rais wa Jamhuri majuzi amesema wazi kwamba kila analolisema Nape ni lake yeye, sasa hebu tumpe nafasi Nape afanye kazi mpya aliyopewa na CCM, moja ya kazi zake mpya ni msemaji mkuu wa chama, kwa hiyo anapoongea ni chama kinaongea.

- Mwacheni Nape, afanye kazi ya chama chake, maaana kama mantiki yako ni hoja basi ungeanza na Dr. Slaa kwanza, kwani hajamuona Mtikila, anavyowahi kwenye sheria akiwa na ushahidi? Pleaseeee!

William @ NYC, USA.
 
He who passively accepts evil is as much involved in it as he who helps to perpetrate it. He who accepts evil without protesting against it is really cooperating with it.
Martin Luther King, Jr.

QUOTE=Vitendo;1910120]Hapo sio Sawa hata kidogo..Nape hakuchakachua Umri wake kipindi cha kugombea uwenyekiti wa UVCCM taifa...waliochakachua ni wale walokuwa vingiozi wa kipindi hicho kwa kusogeza uchaguzi mbele ili kufanya baadhi ya watu kupoteza sifa za kugombea na kama wewe ni mfuatiriaji Mzuri utakumbuka siku ile ya uchaguzi ,mwenyekiti wa chama alipotoa hotuba ya kufungua mkutanoo mkuu wa chama alisema kuwa "Kama umri wa mtu umezidi hata kwa siku moja,basi mtu huyo hana sifa za kugombea ndani ya UVCCM"..wajumbe waliokuwepo mle wakajua tu hilo dogo linamuendea nape "direct" hasa ukikumbuka kuwa Nape alienguliwa kwa kigezo cha umri.[/QUOTE]
 
Wana JF, nimemsikia jioni hii BBC Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bw. Nape kuhusu kujivua gamba. Ila kwa matamshi anayoyatoa ya kumchafua Ndg. Edward Lowasa siyo ya kiungwana wala kianaume,

Kwanza bora aongee na sisi tusikie mambo ya kuongela jikoni hatutaki. ni yametufikisha hapa tulipo.

Pili nafas yake inaamrushu kuongea na vyombo vya habari hata ila siku. Sasa akiulizwa asijibu ???au akwepe maswali.
 
Dah..,Nape atawasababishia wengi pressure.
Common Nape keep it on hadi walie mwaka huu,wanaotaka kukuziba mdomo watajiju .
 
- Mkuu sana kwani kazi ya Katibu Mwenezi wa chama cha siasa ni nini hasa? Hebu weka wazi hilo kwanza halafu ndio utoe hukumu, Rais wa Jamhuri majuzi amesema wazi kwamba kila analolisema Nape ni lake yeye, sasa hebu tumpe nafasi Nape afanye kazi mpya aliyopewa na CCM, moja ya kazi zake mpya ni msemaji mkuu wa chama, kwa hiyo anapoongea ni chama kinaongea.

- Mwacheni Nape, afanye kazi ya chama chake, maaana kama mantiki yako ni hoja basi ungeanza na Dr. Slaa kwanza, kwani hajamuona Mtikila, anavyowahi kwenye sheria akiwa na ushahidi? Pleaseeee!

William @ NYC, USA.
Yaelekea una uchungu na ?mzee wako kuwemo katika listi mpya ya vibakauchumi a.k.a. Mafisadi. Hebu tueleze Mtikila amewahi mara ngapi kwenye hiyo sheria na ameshapata nini zaidi ya kupoteza tu muda wake? Mtindo wananaoutumia CHADEMA ndiyo muafaka, maana haiwezekani kabisa kutafuta haki kwa kwenda kushtaki kwa muasisi wa uhalifu uliotokea. Kimantiki Majaji, Mahakimu, Polisi, Usalama wa Taifa, na huo usanii mnaouita TAKUKURU (Taasisi ya kuwasaidia na Kuwatetea wala Rushwa) n.k. wanateuliwa na Rais,ambaye kwa bahati mbaya huyu wa sasa ni vigumu kutofautishwa na watuhumiwa! Unategemea haki ipi kwa chombo gani cha sheria cha nchi hii ambapo vyooote ni mali binafsi ya Rais na wanaapishwa kumlinda na kumtetea katika kila jambo hata la kuiangamiza nchi hii hii inayowatunza na kuwanawirisha? Hebu tuambie ile kesi ya madai ya mgombea binafsi ya huyo Mtikila dhidi ya serikali iliishaishaje vile? Labda kwa kuwa uko mbali, iligeuzwa shoo ya maigizo na haki ya kikatiba ya Mtanzania kufinyangwa! Tusidanganyane;lugha wanayoigwaya na kuiogopa kama ukoma hawa vibaka mnaowaita CCM ni moja tu, ya Peoples....Power.
 
- Mkuu sana kwani kazi ya Katibu Mwenezi wa chama cha siasa ni nini hasa? Hebu weka wazi hilo kwanza halafu ndio utoe hukumu, Rais wa Jamhuri majuzi amesema wazi kwamba kila analolisema Nape ni lake yeye, sasa hebu tumpe nafasi Nape afanye kazi mpya aliyopewa na CCM, moja ya kazi zake mpya ni msemaji mkuu wa chama, kwa hiyo anapoongea ni chama kinaongea.

- Mwacheni Nape, afanye kazi ya chama chake, maaana kama mantiki yako ni hoja basi ungeanza na Dr. Slaa kwanza, kwani hajamuona Mtikila, anavyowahi kwenye sheria akiwa na ushahidi? Pleaseeee!

William @ NYC, USA.

Huitaji kumtetea Nape. Maoni na Mitazamo tofauti ni kitu muhimu kwa afya ya kimtazamo ya mwanasiasa. Anachokifanya Nape kinamweka katika vita binafsi na EL na kwakua yeye ni 'Light weight' kwenye siasa hii itamgarimu. Ukiongea naye(narejea post yako uliyodai umewasiliana naye) mwambie afuatilie mambo ya kimsingi na sio watu. Amwache Mwenyekiti na Vikao vya Kimaamuzi vishugulike na watu(Individuals)
 
Wangetueleza ni ufisadi gani walioufanya na waliufanyia wapi,manake hizi porojo za kujivua gamba bila ya kutueleza gamba ni kitu gani bado tunaona usanii mtupu.....
 
Mimi Masikitiko yangu ni Kuwa Hawa watu waligombea na kuahidi mambo lukuki, sasa wameshinda kwa kishindo kama wanavyojisifia!! Sasa mbona kazi hawafanyi? Wanafikiri maisha yanasubiri? Fanyeni Kazi ndugu zangu Hatuna haja na malumbano yenu!! Nchi inaangamia kwa lindi la umasikini!!!Kila mahali ni kero tupu, sasa mnatafuta sifa kunako majukwaa badala ya kuwattumikia wananchi!! Sasa mligombea kutawala ili Iweje? Mwendeleze Mabishano? Mjui hii nchi ipo mikononi mwenu hadi 2015, sasa mnasubiri nini kutufanyia mlichotuahidi?
 
Back
Top Bottom