Mhoja
JF-Expert Member
- Aug 13, 2010
- 207
- 24
Wana JF, nimemsikia jioni hii BBC Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bw. Nape kuhusu kujivua gamba. Ila kwa matamshi anayoyatoa ya kumchafua Ndg. Edward Lowasa siyo ya kiungwana wala kianaume, kwa sababu mi naamini wanaume kama kuna matatizo huwa wanakaa na kuongea na kuyamaliza au kutoyamaliza na kuchua hatua. Kwa habari za maamuzi ya NEC kama waliazimia kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi ni jambo jema, kinachotakiwa ni kutekeleza maamuzi ya kikao na siyo kila siku bwana mdogo amekuwa akiongea majukwaani jambo hilo hilo badala ya kulitekeleza na kupeleka taarifa kwenye vikao vilivyoagiza kama watuhumiwa wamepima wenyewe au wamekataa. Ugonvwi wake na Lowasa wakati alitaka kugombea uenyekiti wa UVCCM asitumie jukwaa alilopewa kumharibu kisakiolojia adui yake, maandiko yanasema mpende adui yako. Mimi naheshimu sana maamuzi ya NEC ila kinachonishangaza ni uropokaji wa kila siku wa katibu mwenyezi mpaka inakera. Kwa sababu kuna ugumu gani kama barua anasema zimeandikwa lakini mpaka leo bado hawajapewa, ina maana Ofisi ya CCM inakosa mesenja wa kuzipeleka kwa dispatch au kwa EMS? Cha kushangaza kiongozi aliyebaki kuropoka majukwaani ni Nape peke yake, kwa nini wengine wote wapo kimya? Labda kama hayo anayoyaongea awe ametumwa, lakini kama atakuwa ametumwa ajue kuwa waliomtuma watapita kama wengine walivyopita, na anaweza kuja kuhangaika sana baadaye.
Ninachomuomba barua watuhumiwa wapewe kwa mujibu wa taratibu wa kufikisha barua, kama watazijibu, watakaa kimya au lolote watakalolifanya apeleke taarifa kwenye vikao na siyo kila siku kutoa taarifa zingine za chama ambazo hazina maana kwa watanzania.
Ninachomuomba barua watuhumiwa wapewe kwa mujibu wa taratibu wa kufikisha barua, kama watazijibu, watakaa kimya au lolote watakalolifanya apeleke taarifa kwenye vikao na siyo kila siku kutoa taarifa zingine za chama ambazo hazina maana kwa watanzania.