Namshauri Nape aache visasi

Namshauri Nape aache visasi

Mhoja

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2010
Posts
207
Reaction score
24
Wana JF, nimemsikia jioni hii BBC Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bw. Nape kuhusu kujivua gamba. Ila kwa matamshi anayoyatoa ya kumchafua Ndg. Edward Lowasa siyo ya kiungwana wala kianaume, kwa sababu mi naamini wanaume kama kuna matatizo huwa wanakaa na kuongea na kuyamaliza au kutoyamaliza na kuchua hatua. Kwa habari za maamuzi ya NEC kama waliazimia kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi ni jambo jema, kinachotakiwa ni kutekeleza maamuzi ya kikao na siyo kila siku bwana mdogo amekuwa akiongea majukwaani jambo hilo hilo badala ya kulitekeleza na kupeleka taarifa kwenye vikao vilivyoagiza kama watuhumiwa wamepima wenyewe au wamekataa. Ugonvwi wake na Lowasa wakati alitaka kugombea uenyekiti wa UVCCM asitumie jukwaa alilopewa kumharibu kisakiolojia adui yake, maandiko yanasema mpende adui yako. Mimi naheshimu sana maamuzi ya NEC ila kinachonishangaza ni uropokaji wa kila siku wa katibu mwenyezi mpaka inakera. Kwa sababu kuna ugumu gani kama barua anasema zimeandikwa lakini mpaka leo bado hawajapewa, ina maana Ofisi ya CCM inakosa mesenja wa kuzipeleka kwa dispatch au kwa EMS? Cha kushangaza kiongozi aliyebaki kuropoka majukwaani ni Nape peke yake, kwa nini wengine wote wapo kimya? Labda kama hayo anayoyaongea awe ametumwa, lakini kama atakuwa ametumwa ajue kuwa waliomtuma watapita kama wengine walivyopita, na anaweza kuja kuhangaika sana baadaye.
Ninachomuomba barua watuhumiwa wapewe kwa mujibu wa taratibu wa kufikisha barua, kama watazijibu, watakaa kimya au lolote watakalolifanya apeleke taarifa kwenye vikao na siyo kila siku kutoa taarifa zingine za chama ambazo hazina maana kwa watanzania.
 
Visasi....!

Hakuna kisasi kwa muharifu. Lugha ya visasi ilitumiwa wakati Kikwete anatafuta Urais, eti kuna watu walionyesha kumuogopa kwa visasi vyake. Lakini kama kweli wewe ni mwizi, tukufute kwa mtindo gani? Au tuendelee kusema ni ajali ya kisiasa wakati tuna hakika kabisa kwamba wewe ni fisadi. Hakuna Kisasi. Hiyo ni haki yao kwa ushetani wao.

Ktk CCM kunaweza kuwa na malengo meeengi kwa maamuzi yale yale! Siamini kama Kujivua gamba kuna lengo moja kati ya Nape na Kikwete na wengineo.
Tusimuhukumu Nape. Kama kweli Barua ni kwenda kwa Lowasa, Chenge na RA basi ni lazima aitumie nafasi ya uenezi vizuri. Lazima watu wanaomuhusudu Lowasa waandaliwe kwa taarifa kama hizo za Nape

Hawa, ki-historia ni 'wahalifu sugu' bahati mbaya kabisa wana wafuasi wasiotaka kuona ukweli. Wao binafsi hawako tayari kuikubali hasara inayotokana na vitendo vyao. Taarifa zinaonyesha kwamba Lowasa na wafuasi wake bado haamini kama hataweza kuwa Rais wa nchi hii. Ni kwa gharama yoyote na akikosa basi anasema tukose wote. CCM wakimwaga mboga, naye atamwaga ugali, wote tufe kwa njaa.

Anachohangaikia ni umaarufu wake urudi. Ataanzisha vituo vya redio na hata TV ili aanze kujisifu kwa vyombo vyake.

Hawa wote waache wapate matusi yote yanayowezekana ili wapate elimu ya matendo yao na iwe elimu kwa wengine.
 
Hakuna visasi hapo.muacheni nape afanye kazi yake.
Huyo kijana ni mjasiri sana.kama unataka kujua nape ni mjasiri kwa kiasi gani ..leo hii nenda kamuulize jk,ni maneno gani nape alimwambia kipindi kile jk anaomba fursa ya kuiwakilisha ccm kwenye urais(kura za maoni ccm 2005).
 
Tatizo Nape hana ujasiri wa kuwataja hao mafisadi wanaotaka waondoke CCM maana hana uhakika wala ushahidi wa ufisadi bali anatumia hoja za watu wengine for cheap popularity, kama anajiamini na ana huakika kuna fisadi ndani CCM awataje japo mmoja basi.

Hawezi kuondoa ufisadi mwa maneno ya propaganda.
 
Ok wakubwa nimewaelewa, nilikuwa nazungumzia ubinadamu zaidi kuwa kama mtu amekosa mwadhibu mara moja. Maadamu mmeeleza anachokifanya Nape siyo bisasi nami sina objection. Aendelee.
 
Wana JF, nimemsikia jioni hii BBC Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bw. Nape kuhusu kujivua gamba. Ila kwa matamshi anayoyatoa ya kumchafua Ndg. Edward Lowasa siyo ya kiungwana wala kianaume, kwa sababu mi naamini wanaume kama kuna matatizo huwa wanakaa na kuongea na kuyamaliza au kutoyamaliza na kuchua hatua. Kwa habari za maamuzi ya NEC kama waliazimia kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi ni jambo jema, kinachotakiwa ni kutekeleza maamuzi ya kikao na siyo kila siku bwana mdogo amekuwa akiongea majukwaani jambo hilo hilo badala ya kulitekeleza na kupeleka taarifa kwenye vikao vilivyoagiza kama watuhumiwa wamepima wenyewe au wamekataa. Ugonvwi wake na Lowasa wakati alitaka kugombea uenyekiti wa UVCCM asitumie jukwaa alilopewa kumharibu kisakiolojia adui yake, maandiko yanasema mpende adui yako. Mimi naheshimu sana maamuzi ya NEC ila kinachonishangaza ni uropokaji wa kila siku wa katibu mwenyezi mpaka inakera. Kwa sababu kuna ugumu gani kama barua anasema zimeandikwa lakini mpaka leo bado hawajapewa, ina maana Ofisi ya CCM inakosa mesenja wa kuzipeleka kwa dispatch au kwa EMS? Cha kushangaza kiongozi aliyebaki kuropoka majukwaani ni Nape peke yake, kwa nini wengine wote wapo kimya? Labda kama hayo anayoyaongea awe ametumwa, lakini kama atakuwa ametumwa ajue kuwa waliomtuma watapita kama wengine walivyopita, na anaweza kuja kuhangaika sana baadaye.
Ninachomuomba barua watuhumiwa wapewe kwa mujibu wa taratibu wa kufikisha barua, kama watazijibu, watakaa kimya au lolote watakalolifanya apeleke taarifa kwenye vikao na siyo kila siku kutoa taarifa zingine za chama ambazo hazina maana kwa watanzania.
Ule mkutano mliofanya pale Ubungo na hela mkapewa na mafisadi ndio matokeo yake ehe?
 
mkuu haya mambo ni siri kubwa lakini kwa mwenye macho ahambiwi tazama, ccm walimkata NAPE , KWENYE UVCCM kama mwenyekiti, wakamtema kwenye ubunge kule ubungo,
ghafla wamemleta kama katibu mwenezi kutoka huko MASASI,
kwa wenye HEKIMA majibu ni haya
MWENYEKITI WA CHAMA HANA UBAVU MBELE YA HAO RACHEL, WAO NDIO INGINI YA YEYE KUWA HAPO MAGOGONI, SASA BASI NANI WAKUWA JANITOR ?

ndio hapo anatafutwa mtu hasiye na huruma na RACHEL, na ni NAPE hafanyi haya kwa masilahi ya taifa anafanya kujipoza nafsi yake maana hawa mmoja wao yaani EL ni adui binafsi kwake,
wasiwasi angu ni pale atakapoliza hiyo kazi yake ya U-JANITOR kwa manufaa yake na mkuu wa kaya,
huyu mimi namuweka kundi la ngiri anasahau mapema sana kifuatacho kwake kwenye mbio za kujiokoa na kukomoana.
KWA NINI ANASHINDWA KUJIULIZA TWO BROTHERS kati ya mkuu wa kaya na EL ilikufa wapi?
Wana JF, nimemsikia jioni hii BBC Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bw. Nape kuhusu kujivua gamba. Ila kwa matamshi anayoyatoa ya kumchafua Ndg. Edward Lowasa siyo ya kiungwana wala kianaume, kwa sababu mi naamini wanaume kama kuna matatizo huwa wanakaa na kuongea na kuyamaliza au kutoyamaliza na kuchua hatua. Kwa habari za maamuzi ya NEC kama waliazimia kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi ni jambo jema, kinachotakiwa ni kutekeleza maamuzi ya kikao na siyo kila siku bwana mdogo amekuwa akiongea majukwaani jambo hilo hilo badala ya kulitekeleza na kupeleka taarifa kwenye vikao vilivyoagiza kama watuhumiwa wamepima wenyewe au wamekataa. Ugonvwi wake na Lowasa wakati alitaka kugombea uenyekiti wa UVCCM asitumie jukwaa alilopewa kumharibu kisakiolojia adui yake, maandiko yanasema mpende adui yako. Mimi naheshimu sana maamuzi ya NEC ila kinachonishangaza ni uropokaji wa kila siku wa katibu mwenyezi mpaka inakera. Kwa sababu kuna ugumu gani kama barua anasema zimeandikwa lakini mpaka leo bado hawajapewa, ina maana Ofisi ya CCM inakosa mesenja wa kuzipeleka kwa dispatch au kwa EMS? Cha kushangaza kiongozi aliyebaki kuropoka majukwaani ni Nape peke yake, kwa nini wengine wote wapo kimya? Labda kama hayo anayoyaongea awe ametumwa, lakini kama atakuwa ametumwa ajue kuwa waliomtuma watapita kama wengine walivyopita, na anaweza kuja kuhangaika sana baadaye.
Ninachomuomba barua watuhumiwa wapewe kwa mujibu wa taratibu wa kufikisha barua, kama watazijibu, watakaa kimya au lolote watakalolifanya apeleke taarifa kwenye vikao na siyo kila siku kutoa taarifa zingine za chama ambazo hazina maana kwa watanzania.
 
Nape hana lolote mafisadi hawafukuzwi kupitia majukwaaa kama vikao vilishaamua Nape anatakiwa atekeleze maazimio kama yeye ndiyo mtekelezaji sio kunanga akina Lowasa kila siku majukwaani huku akiwa hana ubavu wa kuwagusa wala kuwafikishia hizop barua. Hapo Nape analipiza tu visasi wala sio kwamba eti anafanya kazi. Kama kweli ccm inawaondoa mafisadi na kwa kuwa JK ni mhusika mkuu wa igizo kwa nini NEC haikuweka kaimu Mwenyekiti kabisa.
Mana sote tunajua mapato ya kifisadi yamemsaidia JK kuwa rais na kama wanafukuzwa ni wote wanaenda, swali Je, nec ilishatangaza Kaimu Mwenyekiti wa chama??
 
Nape hajui anachokifanya...si ndiye huyu huyu aliyechakachua cheti cha kuzaliwa Ili mradi agombee UVCCM?
 
mkuu tumia maneno rahisi maslahi binafsi
vijana wengi walioko ccm wana stress kuliko wazee maana walijua
watakua watawala lakini kwa jinsi watanzania walivyoa shituka sasa wana force king
kuingia ikulu
Nape hajui anachokifanya...si ndiye huyu huyu aliyechakachua cheti cha kuzaliwa Ili mradi agombee UVCCM?
 
Nape na CCM yao wanafiki tu..anyway waache wafu wazike wafu wao!
 
Tatizo Nape hana ujasiri wa kuwataja hao mafisadi wanaotaka waondoke CCM maana hana uhakika wala ushahidi wa ufisadi bali anatumia hoja za watu wengine for cheap popularity, kama anajiamini na ana huakika kuna fisadi ndani CCM awataje japo mmoja basi.

Hawezi kuondoa ufisadi mwa maneno ya propaganda.

Kwa nyepesi zinazovuma Lumumba ni kuwa Msekwa anasita ile mbaya kuweka mkono kwenye hizo barua. Mukama alijitoa mapema kuwa yeye bado ni mpya, ni mtendaji tu, maamuzi ni Mwenyekiti au Makamu. Kazi sasa nani atamfuata Mwenyekiti kuweka mkono wake ili barua zitolewe.

Mmojawapo katika RACHEL keshaipata draft copy ya hizo barua, anavuta tu pumzi kusubiri barua rasmi.

Hii ngoma tamu sana.

Pamoja na visasi na chuki Nape hawezi kuwataja RACHEL hana ubavu huo, na pia hasemi hizo siku 90 zinaanzia lini na zinaishia lini. Je, zilianza baada ya kikao cha NEC/CC, au zitaanza baada ya kupewa barua?
 
Wana JF, nimemsikia jioni hii BBC Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Bw. Nape kuhusu kujivua gamba. Ila kwa matamshi anayoyatoa ya kumchafua Ndg. Edward Lowasa siyo ya kiungwana wala kianaume, kwa sababu mi naamini wanaume kama kuna matatizo huwa wanakaa na kuongea na kuyamaliza au kutoyamaliza na kuchua hatua. Kwa habari za maamuzi ya NEC kama waliazimia kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi ni jambo jema, kinachotakiwa ni kutekeleza maamuzi ya kikao na siyo kila siku bwana mdogo amekuwa akiongea majukwaani jambo hilo hilo badala ya kulitekeleza na kupeleka taarifa kwenye vikao vilivyoagiza kama watuhumiwa wamepima wenyewe au wamekataa. Ugonvwi wake na Lowasa wakati alitaka kugombea uenyekiti wa UVCCM asitumie jukwaa alilopewa kumharibu kisakiolojia adui yake, maandiko yanasema mpende adui yako. Mimi naheshimu sana maamuzi ya NEC ila kinachonishangaza ni uropokaji wa kila siku wa katibu mwenyezi mpaka inakera. Kwa sababu kuna ugumu gani kama barua anasema zimeandikwa lakini mpaka leo bado hawajapewa, ina maana Ofisi ya CCM inakosa mesenja wa kuzipeleka kwa dispatch au kwa EMS? Cha kushangaza kiongozi aliyebaki kuropoka majukwaani ni Nape peke yake, kwa nini wengine wote wapo kimya? Labda kama hayo anayoyaongea awe ametumwa, lakini kama atakuwa ametumwa ajue kuwa waliomtuma watapita kama wengine walivyopita, na anaweza kuja kuhangaika sana baadaye.
Ninachomuomba barua watuhumiwa wapewe kwa mujibu wa taratibu wa kufikisha barua, kama watazijibu, watakaa kimya au lolote watakalolifanya apeleke taarifa kwenye vikao na siyo kila siku kutoa taarifa zingine za chama ambazo hazina maana kwa watanzania.


- Mkuu sana kwani kazi ya Katibu Mwenezi wa chama cha siasa ni nini hasa? Hebu weka wazi hilo kwanza halafu ndio utoe hukumu, Rais wa Jamhuri majuzi amesema wazi kwamba kila analolisema Nape ni lake yeye, sasa hebu tumpe nafasi Nape afanye kazi mpya aliyopewa na CCM, moja ya kazi zake mpya ni msemaji mkuu wa chama, kwa hiyo anapoongea ni chama kinaongea.

- Mwacheni Nape, afanye kazi ya chama chake, maaana kama mantiki yako ni hoja basi ungeanza na Dr. Slaa kwanza, kwani hajamuona Mtikila, anavyowahi kwenye sheria akiwa na ushahidi? Pleaseeee!

William @ NYC, USA.
 
Nape hajui anachokifanya...si ndiye huyu huyu aliyechakachua cheti cha kuzaliwa Ili mradi agombee UVCCM?

Hapo sio Sawa hata kidogo..Nape hakuchakachua Umri wake kipindi cha kugombea uwenyekiti wa UVCCM taifa...waliochakachua ni wale walokuwa vingiozi wa kipindi hicho kwa kusogeza uchaguzi mbele ili kufanya baadhi ya watu kupoteza sifa za kugombea na kama wewe ni mfuatiriaji Mzuri utakumbuka siku ile ya uchaguzi ,mwenyekiti wa chama alipotoa hotuba ya kufungua mkutanoo mkuu wa chama alisema kuwa "Kama umri wa mtu umezidi hata kwa siku moja,basi mtu huyo hana sifa za kugombea ndani ya UVCCM"..wajumbe waliokuwepo mle wakajua tu hilo dogo linamuendea nape "direct" hasa ukikumbuka kuwa Nape alienguliwa kwa kigezo cha umri.
 
Ni ugomvi wa makundi ndani ya CCM. Usije shangaa wanaonekana wanashangilia muda huu,baada ya mwaka mmoja ndiyo watuhumiwa
 
Jamani toka lini JF ikiwa washabiki wa Lowassa au mimi ndio sijui?
 
tanzania yetu ya nyerere ilishakufa

hii tanzania ya leo kama kenya hivi au nigeria hivi.....

unbelievable
 
Ninachojua Nape ni Katibu mwenezi moja ya kazi yake kuongea sasa we Mhoja hutaki aongee?waachie hoja zao CCM mbona Wanaotajwa hawasemi lolote? Mbona hujamsema Makongoro Nyerere? Au ?
 
Hapa Kikwete ametafuta pakuamishia lawama Nape na Msekwa! Kikwete ni Rafiki wa Lowasa kufa na kupona hawakukutana barabarani kama alivyosema Lowasa, Kinacho waumiza kichwa ni jinsi ya kuokoa CCM wao wameshauriwa na Msomali mmoja kuwa kuwafukuza hao itaipa CCM credit kubwa na kuifufuwa! sijui kama ni kweli au la!

Ujinga waliofanya na ambao CCM wamesahau ni kuwa staili wanayotumia ni kama ile ya Kikwete kwa SAS 2005. Kama CCM walitaka na kama Kikwete amedhamiria kwa dhati hili swala kazi ingemalizwa kilaini kupitia Dola maana ndio wanaoshughulikia Mafisadi na ndio wana-sheria na kuzilinda, sasa iweje CCM iseme leo hao watu ni mafisadi wakati waliwai kukana hapo nyuma? Mbona Kikwete alitumia hadi vyombo vya Dola kuwasafisa hao watu leo watawashikia wapi? Kazi siyo rahisi hivyo maana wanapaswa pia kutwambia Ufisadi waliofanya! na itakuwaje iwapo hao watu hawata shughulikiwa na Dola labda hata walisha forgy na kupoteza ushahidi maana nijuavyo asilimia karibia 80 ya wachunguzi makini waliokuwa wanajua vyema mafaili ya EPA na Richmond wameshakufa hasa wale wa PCCB na Polisi?

Hapa wanafanya mchezo mchafu hawashughulikii mafisadi nakataa, hapa wameanza kampeni za Urais hawa jamaa, kama ni Ufisadi tunataka kusikia NAPE yupo kimia, bali tunataka kusikia Kikwete, Pinda, Luhanjo, Rashid, Hoseah na Mwema ndio wanaongea na kutwambia mikakati na mipango dhidi ya Ufisadi wote uliowai kufanywa, hao ndio watutangazie majina ya watuhumiwa wa Ufisadi na lini wanafikishwa mahakamani siyo kelele za Nape.

Hata hivyo kuna wakati nahisi baadhi ya wanachama wa CCM hawakumuelewa M/kiti wao! hasa aliposema wanavua gamba, maana nyoka akivua gamba bado anakuwa nyoka tu! yamkini anakuwa hatari kuliko awali!

Ila yote hiyo ni kumsafishia njia Mwinyi mdogo ndani ya CCM kama itapona lakini maana ipo ICU
 
Back
Top Bottom