Namsaidiaje?

Namsaidiaje?

PetCash

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2012
Posts
1,996
Reaction score
2,017
Toka tufunge ndoa maisha yetu yamekuwa mazuri na simple sana.
Ni mke tunayeelewana na ni mshkaji wangu sana tu.
Tumepeana uhuru mkubwa sana ila pia una mipaka. Kuna mipaka ya kawaida ambayo mwanajamii
yeyote anaielewa na kuna ambayo si muhimu sana ila tumeamua tu kujiwekea
(Kwa mfano kwa sababu mimi ndo mwenye ex tunayewasiliana bado,
mazungumzo yetu hayaruhusiwi kuwa zaidi ya kujuliana hali).


Basi ana rafiki yake(jst friends) wa toka o'level, na familia zao ziliko jirani na ni family friends.
Huyu jamaa alikuwa close sana na wife enzi hizo ila hawakuwahi kwenda zaidi
(Najua kwa sababu hakuna kabla yangu aliyewahi). Ila ukaribu wao ulikuwa unatisha,
kwa mfano one day walienda beach na friends wengine wa jirani
(mtaani kwao wife walikuwa mambo safi kidogo tofauti na nlipokulia mimi). enzi hizo tunaanza kuwa wachumba
wife kanipigia simu niende na nilipofika jamaa alimkiss kidogo kwenye lips. Nikashtuka sana cku hiyo,
nilipomuuliza akasema ni normal na kweli jamaa alimkiss mdada mwingine ambaye boyfriend wake alikuwepo
hivyo hivyo. Basi nikafunguka kumuambia kuwa mambo hayo mi siyawezi na akanisikia. Wife ni mpole kiasi
na kakulia sehemu yenye maadili mazuri ila uzunguuzungu ulikuwa mwingi hata hivyo baadae tukawezana.


Sasa miaka kadhaa mbele ndo mwezi jana, yeye kaolewa(na mimi) na jamaa ana mke. Sasa juzi kati jamaa katoka
edinburg. Wife alipotoka kazini akaniaga anaenda kuwatembelea. Alipokuja home akaja na laptop,
akaniachia akaenda rum sasa mimi nikawa naishangaa(touch screen) na kuitumia nikasahau hata kumuuliza alipewa zawadi,
ni ya kazini ama alinunua. NIkawa tu naitumia hata wife hakuwa na time nayo tena. Sasa wiki iliyopita nakuja gundua
kuwa wife alivyoenda kwa jamaa(ile mwezi jana) aliacha ndoa yake mashakani baada ya siku chache.


Kiukweli ni kwamba laptop alipewa na jamaa kama zawadi ya kuja, jamaa hela alizopewa kwa safari ya Uskoti si nyingi sana
na alileta zawadi mbili tu! pauni 300 mkufu wa mkewe na laptop pauni 450 for my wife!!!!
Sasa mkewe alivyoambiwa hivyo na mmewe akammind, akaondoka usiku kulala kwa wazazi wa mume. Usuluhishi umefanyika wiki
nzima jamaa analala alone ndo mambo yakawa poa, mke akataka laptop wazazi wakambembeleza amwachie(si wanamjua wife).


Sasa huku kwangu mimi na laptop, laptop na mimi, sina nnalolijua na wife anajua hajajishunghulisha nao anaogopa na
hakuniambia chochote. Hiyo wiki jana sasa mke wa jamaa kaniambia shem nna mazungumzo nawe. Nikapitia kwao(mmewe hayupo)
akaniambia yote. Mimi nikataka kumuuliza wife kwa nini alinificha, nikawazaa nikaingiwa na wasiwasi. Kwanza kwa nini
jamaa amnunulie gift expensive kuliko mkewe?Ile laptop nzuri vile y jamaa asiifanye yake?


Basi na mimi nikaamua kunyamaza. Niakaanza kukumbuka vitu vidogovidogo vilivyokuwa vinanitatiza. Kwanza wiki ile
(mwezi jana) jamaa kaondokewa nyumbani na mkewe alikuwa anaenda sana kazini kwa wife
(Nilishamkuta mara2 wakati nampitia wife na mara ya2 ilikuwa ghafla sana kiasi kwamba kwa mbali ni kama hawakutaka niwakute pamoja).
Mke wangu amekuwa mkimya too much hata siku moja tulikuwa tunatoka kazini kila nikianzisha stori
inakufa niakaamua kunyamaza nimuobserve almanusura apitilize nyumba(alikuwa anaendesha).
Siku moja nilimuacha mke akichat naye sebuleni narudi namkuta anafuta machozi fasta! Nilimbana cku hiyo hadi karibu tugombane.
Ni kazi? hapana, nyumbani? hapana wazazi? hapana nimekuudhi? hapana. Ni hormones? hapani Nikamtaja jamaa aliyechati naye
labda kamuudhi akashtuka kidogo then hapana!Nikamkomalia tukaelekea kugombana ikabidi nimuache.


Sasa waungwana nahisi mke wangu anaanza kufall kwa jamaa(Na jamaa vilevile). Natamani kumuuliza wife lakini
1) Sipendi kuonekana mwanaume mwenye wivu kumuingilia wakati tulishadefine mipaka na hajacross...
2) Na kama wanakuwa wapenzi ni kwa nini miaka yote hiyo wako close wasiwe?(No body was stopping them. Na nnajua hawajawahi kuwa hivyo)
3) Nimekomaa sana kumjali na kumtunza mke wangu na yeye pia vilevile na naamini itakuwa ngumu sana kwake kuvuka mipaka,
lakini nafanyaje sasa kumrudisha wakati moyo wake unaenda huko? How do i rescue her before she breaks her heart?
4) Naombeni mnishauri kwa sababu mtu akimpenda mtu hata nipige mikwara kama kweli wakidhamiria kufanya mi naepushaje?
5) Mliishije/Mnaishije kwenye ndoa zenu kuepuka haya?(mnisaidie second year mimi)
 
Dark City .....
kuja huku...mkuu

Mkuu naona unanitakia kesi....huu ni muda wa watu kaka....

Ila vijana wengine wanatia huruma.....Unawezaje kuruhusu mtu mwingine awe na ukaribu wa namna hiyo na mwenzi wako??

Halafu kuna jambo niliapa kutolifanya na kweli Mungu alinisaidia...kama mtu wa bush basi tamfuta kuku wa kienyeji mwenzio...... Haya mambo ya kuchanganya Lawino na Ocol kwenye chungu kimoja ni magumu sana aisee!!

Hapa naona "mbombo ngafu"....

Babu DC!!
 
daaa...
wewe kweli unahitaji ushauri kabla hujakutana na MANYOYA... HorsePower Kaunga gfsonwin
babu @Aspirin ..mkuje huku kushauri jamani.. jahazi lisije zama.

Akutane na manyoya mara ngapi??

Hivi kweli mume au mke analeta kitu kipya kama Laptop na haulizwi kaipata wapi??

Nahisi kama kuna ndoa ambazo watu wanaogopana kama maafande!

Babu DC!!
 
Pole ndugu yangu kwa masahibu hayo! Lakini ninachokiona hapo ni kwamba mwanamke kama ilivyo kwa mwanaume ni dhaifu katika mioyo yetu!! Mkeo tayari ameshafall kwa rafikiye huyo wa zamani. Kaka siyo wazungu sisi ambao huwa wanaweza hizo defined boundaries kwa sisi waafrika kwa kweli we need to have a defined boundaries. Mi nadhani inawezekana washapitiliza katika mahusiano yakawaida na wako katika mapenzi mootomoto. Wakati unaoana hakukuwa na uhakika wa true feelings kwa huyo so called friend, sasa tayari mkeo ameshapata hisia za kumpenda jamaa na anaongezewa upendo hasa kupitia hizo zawadi na ukaribu pamoja na mazoea yamepelekea kufikia mahusiano (if at all they have fallen in).

Ushauri: Jitahidi kuvuruga mahusiano yao tena very soon kunusuru ndoa yako na hii ni kwa kutumia njia yeyote kuwakeep apart hawa wawili hasa hasa kwa kumuweka mkeo ajifeel guilt kwa kuvuruga ndoa ya wenzake (the now ongoing conflict to your friend' marriage should be used as a shield). Lakini kama utaacha mawasiliano na mazoea yaendelee kizungu kama zamani kaka utarudi hapa Jukwaani kutupa habari ya kutengana. Mwanamke akifall huwa harudi nyuma tofauti na wanaume ambao most of the time are unpredictable!! Otherwwisw Pole sana wangu!!
 
Mkuu naona unanitakia kesi....huu ni muda wa watu kaka....

Ila vijana wengine wanatia huruma.....Unawezaje kuruhusu mtu mwingine awe na ukaribu wa namna hiyo na mwenzi wako??

Halafu kuna jambo niliapa kutolifanya na kweli Mungu alinisaidia...kama mtu wa bush basi tamfuta kuku wa kienyeji mwenzio...... Haya mambo ya kuchanganya Lawino na Ocol kwenye chungu kimoja ni magumu sana aisee!!

Hapa naona "mbombo ngafu"....

Babu DC!!

Mi mwenyewe nimeshindwa cha kuzungumza
hapa kuna culture clash kubwa pia
 
Mi mwenyewe nimeshindwa cha kuzungumza
hapa kuna culture clash kubwa pia


Eti mtu anampiga busu mpenzi wako mdomoni na wewe unaangalia na kunywea??

Mbado sana kuelewa haya mambo ya dotcom!!

Babu DC!!
 
Pole ndugu yangu kwa masahibu hayo! Lakini ninachokiona hapo ni kwamba mwanamke kama ilivyo kwa mwanaume ni dhaifu katika mioyo yetu!! Mkeo tayari ameshafall kwa rafikiye huyo wa zamani. Kaka siyo wazungu sisi ambao huwa wanaweza hizo defined boundaries kwa sisi waafrika kwa kweli we need to have a defined boundaries. Mi nadhani inawezekana washapitiliza katika mahusiano yakawaida na wako katika mapenzi mootomoto. Wakati unaoana hakukuwa na uhakika wa true feelings kwa huyo so called friend, sasa tayari mkeo ameshapata hisia za kumpenda jamaa na anaongezewa upendo hasa kupitia hizo zawadi na ukaribu pamoja na mazoea yamepelekea kufikia mahusiano (if at all they have fallen in).

Ushauri: Jitahidi kuvuruga mahusiano yao tena very soon kunusuru ndoa yako na hii ni kwa kutumia njia yeyote kuwakeep apart hawa wawili hasa hasa kwa kumuweka mkeo ajifeel guilt kwa kuvuruga ndoa ya wenzake (the now ongoing conflict to your friend' marriage should be used as a shield). Lakini kama utaacha mawasiliano na mazoea yaendelee kizungu kama zamani kaka utarudi hapa Jukwaani kutupa habari ya kutengana. Mwanamke akifall huwa harudi nyuma tofauti na wanaume ambao most of the time are unpredictable!! Otherwwisw Pole sana wangu!!

Hapa kuna bomu jingine limejificha kizani....

Kama mke wa jamaa kafikia kushtaki kwa shemeji yake...kuna bonge la swap linakuja kwa kasi...lol!!

Babu DC!!
 
ahaha Mi nnachoona hapo ni kuwa hamna cheating wala nini..sema uzungu uzungu umezidi..afu we mwenyewe hujui mambo hayo ahahha ndo inabidi ujifunze sasa...dont change the players change the game... anza kumualika huyo mshkaji hapo home makusudi uone wanavokuwa mbele yako ...mwisho utaelewa ni nini..ila kuhusu cheating sio kweli.wangefanya kwanzia kipindi hicho...hai make sense.
 
Mmmh, hapa pagumu. Ngoja wenye ndoa waongee kwanza.
Mungu akusaidie
 
Pet cash umepotea kweli siku hizi kiongozi!!

Naomba nikwambie haya ila ni machungu lkn dawa
... Hivi hata kumuuliza mkeo laptop kaipata wapi na penyewe uliogopa ili tu usije kugombana nae??
...hivi wewe unaona sawa mkeo kuwa karibu na rafiki yake hata kama anakuumiza??
...hivi wewe unaamini kwamba ulimzibua mkeo kisa tu alimwagika damu siku ya kwanza je unajua kwamba hata vizibo vya mchina vipo??
...sasa usemapo tukupe ushauri wafikiri sisi tutaweza kuvaa viatu vyako ya kwamba ww umeshindwa kuwa mume ndani mwako??
 
Last edited by a moderator:
eti mtu anampiga busu mpenzi wako mdomoni na wewe unaangalia na kunywea??

Mbado sana kuelewa haya mambo ya dotcom!!

Babu dc!!
huu wala sio uzungu ni uzumbukuku!!
Hivi wanaume wengine wamekoma kuwa wanaume etieeee!!
Babuuuu hebu kwanza rudisheni jando jamani kweli huyu ni mwanaume kabisaaa aliyetahiriwa na baba yake??
 
hii sasa ni soo kama vipi kaeni wote mbwatukiane ili iwe poa kuliko mlewe na kujikuta mnapandana kama mwanajf yule baada ya faida wakajikuta wanapandana
 
Back
Top Bottom