Nampongeza Rais, tulisubiri ulianzishe....

Nampongeza Rais, tulisubiri ulianzishe....

Kaka VUTA-NKUVUTE , masikio ya watanzania wote kwa sasa yapo kwa TINDU LISU, hata Uncle Magu yupo masikio wazi kusubiri Tindu ataongea nini, naona Tindu anaiendesha na kuisumbua Serikali sana

Ngoja atoe neno
 
Wote nyie wezi ni kuwatupa tu mmetuibia mno hakuna mabadiliko kupitia ccm hakuna wewe kama mzuri na una nia na nchi hii njoo chadema njoo ukawa ila kama huko sahau
 
Akimalizana na madini ageukie na mbuga zetu za wanyama nako kuna madudu mengi.
 
Mimi VUTA-NKUVUTE alias Mzee Tupatupa, kada nguli wa CCM na 'Shushushu' mstaafu, nampongeza Rais na Mwenyekiti wangu wa CCM Dr. John Pombe Magufuli kwa anachokifanya sasa kuhusu madini. Nampongeza Rais kwa kuanzisha 'vita' hii ya kusaka haki yetu kama Taifa na kupata tunachostahili.

Mhe. Rais, nimekusikiliza vya kutosha bila kutisha. Nakupongeza hasa kwa kuliona tatizo linalozunguka mambo yote haya: ubovu wa Sheria zetu mbalimbali zinazosimamia madini. Hakuna haja ya kunyoosheana vidole kwa wale waliokuwa wakijadili tofautitofauti lakini kwa hoja moja ya ubovu wa sharia.

Mhe. Rais, kuhusu wahusika waliotajwa na Kamati Maalum ya Prof. Osoro leo, ulipaswa kuagiza kwa kutaja majina wahusika wa kuhojiwa. Wametajwa wengi kwenye Ripoti, kwa mazuri na mabaya. Wametajwa wasiotajika na watahojiwa wasiohojika. Madini ni yetu sote. Tutayalinda hadi tone la mwisho la damu yetu kama watanzania. Tulitaka Rais uanze.

Mhe. Rais, umefanya vyema kumkabidhi kazi ya kisheria Nguli wa Sheria, Prof. Kabudi. Yeye anawajua waliokuwa wanafunzi wake bora, imara, waaminifu na walinda maslahi ya nchi. Anawajua waliopo Serikalini na wale walio sekta binafsi. Anawajua waliopo chamani-CCM na wale waliopo upinzani. Kwakuwa hili sasa ni jambo la kitaifa, atawachagua kutoka popote.

Kuwa na 'neutral pool' ya Wanasheria wazalendo ni jambo kubwa na la kupongezwa. Ulinzi wa nchi kiuchumi upo kwenye sheria. Mhe. Rais, ulipaswa kuwataja wakuhojiwa waziwazi: Chenge, Yona, Salula, Mwanyika, Kafumu na kadhalika. Kwakuwa wote ni wanaCCM, nakushauri uwashughulikie pia kichama ili 'kukisafisha' chama.


Tutalinda mali zetu, tulisubiri Rais alianzishe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Kile kipindi cha kupata heshima mtaani kutokana na kutuibia naona kimefika ukingoni. Bado kitambo kidogo kila mtu ataishi kwa mshahara ambao anaufanyia kazi. Sijui Karamagi, Kafumu, Mwanyika kama leo watalala, maana wametajwa mubashara vyombo vya dola viwashughulikie. Kwa uzoefu naona mtemi Chenge atachomoa tu.
 
Nisaidieni kumwelewa Rais wangu jamani; Sheria irudishwe bungeni ijadiliwe upya na wale walioupitisha alafu watolewe nje wale waliokua wanaitaji irudishwe waijadili upwa.

Au Mimi ndo sijaelewa hapa; uTaifa wetu umepotelea wapi?
Anataka akina Kibajaj ndo wajadili hapa ndo namuona Rais anatuchezea akili
 
Kile kipindi cha kupata heshima mtaani kutokana na kutuibia naona kimefika ukingoni. Bado kitambo kidogo kila mtu ataishi kwa mshahara ambao anaufanyia kazi. Sijui Karamagi, Kafumu, Mwanyika kama leo watalala, maana wametajwa mubashara vyombo vya dola viwashughulikie. Kwa uzoefu naona mtemi Chenge atachomoa tu.
Chenge yupo live Bungeni anaongoza Bunge muda huu
 
Kama leo rais anakubali pendekezo la mikataba isiwe siri kwanini bunge lisiwe live ili nasi tuone uwazi huo. ...?
 
Wapinzani bado wanastahili pongezi wanaona mbali japo baadhi yetu hatuoni.Hata raisi alipaswa kuwashukuru sana na kuwatia moyo waendelee kukosoa na kutoa ushauri kwa serikali mana haya yote walishayapigia kelele.
 
Siku mikataba inasainiwa ulimpongeza hivi hivi Rais aliyekuwepo wakati ule. Shame on you
LINI? TOA WEHU WAKO HAPA? NANI ALISHANGILIA?MBONA UNAONGEA AS IF IMESAINIWA MWAKA 2015
 
Naendelea kuunga mkono juhudi zozote za dhati za kulinda rasilimali zetu yakiwemo madini. Na kwa leo Mh Rais nikupongeze wewe mwenyewe. Ukiwa siriaz na ukaunganisha nguvu zetu Taifa litapona na tutaanza kula neema ya rasilimali zetu.

Lakini nachelea kusema isiwe nguvu ya soda na tusiishie kwenye madini. Tunaibiwa sana kila mahali kama Utalii na Gesi, sasa wakati bado chuma ni cha moto twende na kule pia.
 
LINI? TOA WEHU WAKO HAPA? NANI ALISHANGILIA?MBONA UNAONGEA AS IF IMESAINIWA MWAKA 2015
Akili za CCM ni za kipekee, siku hiyo mpaka mlienda kuomba kibali kwa Mahita cha maandamano ya kumpongeza Mhe Rais aliyekuwepo mkuu.
 
hivi mzee tupatupa wa lumumba ndo nani?!isijekuwa mshana
 
Kwa upande mwingine hizi findings za Kamati ya Pili kwa zaidi ya asilimia 90% ziko kwenye hotuba mbalimbali za Mh Mnyika na Dr. W. Slaa. Jipya hapo kwenye kamati ni hilo la Usajili wa Acacia BRELA. Zinalandana sana na hoja na kilio cha Upinzani kwa takriban miaka 15 iliyopita.

Kwa hiyo viongozi wetu na hasa Wabunge wa CCM ni budi sasa mbadilike. Mchango wenu kwenye hasara na wizi huu ni mkubwa sana na wa miaka mingi.

Pia niungane na wengine kutoa rai kuwa yapelekwe Bungeni marejeo ya Katiba JMT. Tufute kifungu cha 46 hasa kumwondolea kinga Rais kutoshtakiwa. Hilo lifanyike sambamba na hatua za kuwaadhibu waliokuwa wasaidizi wao (Mh Mkapa na Mh Kikwete) ambao wametajwa kwenye ripoti hii na nyingenezo za Kibunge. Iwapo hamtawachukulia hatua stahiki na kuwaadhibu Mkapa na Kikwete basi huu utakuwa ni uonevu kwa "dagaa". Nimnukuu Rais Magufuli leo wakati akihitimisha alisema "....hao wadogo mnawaadhibu lakini hawa wakubwa hamuwachukulii hatua....." sasa aishi hayo maneno yake kwa vitendo, hilo tu.
 
Kwa upande mwingine hizi findings za Kamati ya Pili kwa zaidi ya asilimia 90% ziko kwenye hotuba mbalimbali za Mh Mnyika na Dr. W. Slaa. Jipya hapo kwenye kamati ni hilo la Usajili wa Acacia BRELA.

Kwa hiyo viongozi wetu na hasa Wabunge wa CCM ni budi sasa mbadilike. Mchango wenu kwenye hasara na wizi huu ni mkubwa sana na kwa miaka mingi.

Pia niungane na wengine kutoa rai kuwa yapelekwe Bungeni marejeo ya Katiba JMT. Tufute kifungu cha 46 hasa kumwondolea kinga Rais kutoshtakiwa. Hilo lifanyike sambamba na hatua za kuwaadhibu waliokuwa wasaidizi wao (Mh Mkapa na Mh Kikwete) ambao wametajwa kwenye ripoti hii na nyingenezo za Kibunge. Iwapo hamtawachukulia hatua stahiki na kuwaadhibu Mkapa na Kikwete basi huu utakuwa ni uonevu kwa "dagaa". Nimnukuu Rais Magufuli leo wakati akihitimisha alisema "....hao wadogo mnawaadhibu lakini hawa wakubwa hamuwachukulii hatua....." sasa aishi hayo maneno yake kwa vitendo, hilo tu.
Sheria/Katiba huwa hairudi nyuma mkuu.
 
Sheria/Katiba huwa hairudi nyuma mkuu.

Desperate situation demands desperate measures.

Sasa kwa yaliyofanyika awamu ile ya 3 & 4 utarudishaje fedha zilizoibiwa? Utakomeshaji uhuni na ufisadi uliokithiri toka Ikulu mpaka ofisi ya Kitongoji? Na kama utambana Karamagi, Chenge na Yona, je kwanini usimbane Mkapa na Kikwete?
 
Back
Top Bottom