Mwananchi B
JF-Expert Member
- May 23, 2013
- 2,050
- 4,602
Ni mwanamke ninaempenda sana namuamini pia nimempa kila kitu ili asione najificha kwa chochote nyuma ya pazia, kama nywila zote isipokuwa za ATMs, namjali sana, kila mda lazima nijue anaendeleaje kwa njia yoyote ile, nampa kila kitu anachohitaji hata kama mda mwingine ni cha kipuuzi, kiufupi namthamini sana kama mtu wa muhimu sana kwangu.
Nimeanza nae mahusiano mda sasa yapata miaka miwili, tupo nae mbali kidogo yaani mikoa tofauti, ila huwa twakutana baada ya mda fulani, na yale mambo nipo kawaida tu, lakini tatizo ni kwamba ni Kama hatambui uwepo wangu, napokosea kidogo tu hata ambapo kosa si langu inakuwa ni shida ni kama mda mwingi nakuwa napimwa Kwa vimaswali vya ajabu ajabu, sasa kimbembe niteleze ulimi au kidole basi itakuwa balaa.
Mda mwingine nikiangalia hata wastani wa ujumbe mfupi ninaotuma na anaonitumia ni hauna uhusiano ni kama ndani ya jumbe 10, basi mbili ndio zake, pia kuna mda tunaongea katika simu yeye anaongea na wengine wa pembeni yake tena anarudi kwangu, nikimwambia basi ni kununiana, nami nikifanya hivyo basi ndio kimbembe, mara oooh hunijali, mara oooh una visichana vyako huko, balaa apige akute simu bize ni balaa, utaulizwa maswali 700, haniamini, sasa sijui tatizo ni nini?
Au nampenda sana? nipunguze mapenzi kwake? Hivi kumpenda sana ni tatizo maana nasikia ukimpenda sana mwanamke anakuona kanya boya? Au nimuache tu? Maana mda mwingine nahisi hanipendi, labda mie ndio napenda sana, kinachoniuma zaidi mda napokosea kidogo ananifananisha na jamaa yake wa zamani ambae hakuwa mwaminifu, na mie sina ujinga huo, huwa natamani kumwambia aniache.
Ila nikikaa hasira zaisha naendelea nae, kiukweli sipendi kabisa kusingiziwa kitu pia sipendi wala kusikia michepuko nayathamini mahusiano yangu na huyu mbidada. Tena kuna mda tukiwa fresh twapiga stori anamsifia, yaani ni kama uwepo wangu kwake ni mdogo sana. Imekaaje hii wakuu?
Nawasilisha
Nimeanza nae mahusiano mda sasa yapata miaka miwili, tupo nae mbali kidogo yaani mikoa tofauti, ila huwa twakutana baada ya mda fulani, na yale mambo nipo kawaida tu, lakini tatizo ni kwamba ni Kama hatambui uwepo wangu, napokosea kidogo tu hata ambapo kosa si langu inakuwa ni shida ni kama mda mwingi nakuwa napimwa Kwa vimaswali vya ajabu ajabu, sasa kimbembe niteleze ulimi au kidole basi itakuwa balaa.
Mda mwingine nikiangalia hata wastani wa ujumbe mfupi ninaotuma na anaonitumia ni hauna uhusiano ni kama ndani ya jumbe 10, basi mbili ndio zake, pia kuna mda tunaongea katika simu yeye anaongea na wengine wa pembeni yake tena anarudi kwangu, nikimwambia basi ni kununiana, nami nikifanya hivyo basi ndio kimbembe, mara oooh hunijali, mara oooh una visichana vyako huko, balaa apige akute simu bize ni balaa, utaulizwa maswali 700, haniamini, sasa sijui tatizo ni nini?
Au nampenda sana? nipunguze mapenzi kwake? Hivi kumpenda sana ni tatizo maana nasikia ukimpenda sana mwanamke anakuona kanya boya? Au nimuache tu? Maana mda mwingine nahisi hanipendi, labda mie ndio napenda sana, kinachoniuma zaidi mda napokosea kidogo ananifananisha na jamaa yake wa zamani ambae hakuwa mwaminifu, na mie sina ujinga huo, huwa natamani kumwambia aniache.
Ila nikikaa hasira zaisha naendelea nae, kiukweli sipendi kabisa kusingiziwa kitu pia sipendi wala kusikia michepuko nayathamini mahusiano yangu na huyu mbidada. Tena kuna mda tukiwa fresh twapiga stori anamsifia, yaani ni kama uwepo wangu kwake ni mdogo sana. Imekaaje hii wakuu?
Nawasilisha