Naleta kwenu wadau,
Yupo dada mmoja ambaye nimetokea sana kumpenda. Ukaribu wetu na kufahamiana kulianza mwaka huu mwezi January. Sasa baada ya kufahamiana kama marafiki kwa muda sasa nimetokea kumpenda na kumuhitaji maishani kama mke wangu. Nina miaka ishirini na nane sasa na ningetamani kuoa mwakani mambo yakienda vyema. Nisingependa kufika 30yrs sijaoa.
Tatizo langu ni moja, huyu binti baada ya kumweleza ukweli alinitamkia waziwazi kwamba ana mtu ambaye wako kwenye mahusiano japokuwa hawapo in good terms lakini wako pamoja. Swali langu ni moja, je niendelee kukaza uzi kwa huyu binti especially at this time akiwa na mahusiano shake? Au niachane nae tuendelee kuwa marafiki tu?
Naomba ushauri wenu wadau
Nawasilisha