Nampenda mchumba wangu wa zamani

Nampenda mchumba wangu wa zamani

Head teacher

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2012
Posts
1,796
Reaction score
413
Najuta kuolewa na mwanamume nisiye mpenda. Ni stori ndefu lakini kwa kifupi...nilikuwa na boyfriend wangu tuliyependana sana. Tulipanga kuoana na barua ya posa alishaleta kwetu. mchumba wangu muda huo alikuwa anasoma chuo kikuu na mimi nilikuwa form six. Baadae nilisikia kuwa mchumba wangu ana mahusiano na binti mmoja ambapo baadae ikasemekana alimpa mimba na kisha kuzaa mtoto wa kiume. Nilipo muuliza alikana kutembea na mwanamke huyo na alikataa kuwa mtoto si wake. Lakini kadiri siku zilivyoenda palionekana kila dalili kuwa mtoto ni wake kwani walifanana sana. Kwa hasira nikaamua kumwacha nami nikatafuta mwanamume nizae naye kulipiza kisasi. Ingawa ulikuwa uamuzi mgumu kwangu nikazaa na mvulana mmoja ambaye kusema ukweli sikumpenda kama mchumba wangu. Nikiwa mjamzito yule mchumba wangu aliniomba tuendelee na mahusiano kwa lengo lile lile la kuoana. Mchumba angu hakujali sana kile kitendo cha kupata mimba. Na tuliendelea uhusiano wetu kama kawaida ila safari hii nikiwa na waume wawili tena wanaofahamiana.
Mwanamume huyu wa sasa kwa kuhofia kunyang'anywa mke alipeleka barua fasta kwa wazazi na taratibu za kufunga ndoa zilianza mara. Mpaka sasa nimefunga ndoa kanisani na mwanamume huyu nisiyempenda na nina watoto wawili. Mchumba angu aliamua kumuoa yule mwanamke na amezaa naye jumla ya watoto watatu ila hajafunga ndoa akidai ananisubiri mimi niamue lini tutaoana, huku akijua nimefunga ndoa. Kwani naye anasema hampendi mwanamke anayeishi naye. Kwa upande mwingine wazazi na ndugu wa mchumba wangu hawampendi mke wake , wakati wazazi na ndugu zangu hawampendi mume wangu. Hivyo nipo dilema. Lakini ukweli ni kwamba mimi ninampenda zaidi sana mchumba wangu wa zamani na hapa nilipo nina mimba yake na ninatarajia kujifungua hivi punde. Natarajia baada ya kujifungua nianze ukurasa mpya na man of my dream........ Kama kuna ushauri wowote nitashkuru sana
 
Najuta kuolewa na mwanamume nisiye mpenda. Ni stori ndefu lakini kwa kifupi...nilikuwa na boyfriend wangu tuliyependana sana. Tulipanga kuoana na barua ya posa alishaleta kwetu. mchumba wangu muda huo alikuwa anasoma chuo kikuu na mimi nilikuwa form six. Baadae nilisikia kuwa mchumba wangu ana mahusiano na binti mmoja ambapo baadae ikasemekana alimpa mimba na kisha kuzaa mtoto wa kiume. Nilipo muuliza alikana kutembea na mwanamke huyo na alikataa kuwa mtoto si wake. Lakini kadiri siku zilivyoenda palionekana kila dalili kuwa mtoto ni wake kwani walifanana sana. Kwa hasira nikaamua kumwacha nami nikatafuta mwanamume nizae naye kulipiza kisasi. Ingawa ulikuwa uamuzi mgumu kwangu nikazaa na mvulana mmoja ambaye kusema ukweli sikumpenda kama mchumba wangu. Nikiwa mjamzito yule mchumba wangu aliniomba tuendelee na mahusiano kwa lengo lile lile la kuoana. Mchumba angu hakujali sana kile kitendo cha kupata mimba. Na tuliendelea uhusiano wetu kama kawaida ila safari hii nikiwa na waume wawili tena wanaofahamiana.
Mwanamume huyu wa sasa kwa kuhofia kunyang'anywa mke alipeleka barua fasta kwa wazazi na taratibu za kufunga ndoa zilianza mara. Mpaka sasa nimefunga ndoa kanisani na mwanamume huyu nisiyempenda na nina watoto wawili. Mchumba angu aliamua kumuoa yule mwanamke na amezaa naye jumla ya watoto watatu ila hajafunga ndoa akidai ananisubiri mimi niamue lini tutaoana, huku akijua nimefunga ndoa. Kwani naye anasema hampendi mwanamke anayeishi naye. Kwa upande mwingine wazazi na ndugu wa mchumba wangu hawampendi mke wake , wakati wazazi na ndugu zangu hawampendi mume wangu. Hivyo nipo dilema. Lakini ukweli ni kwamba mimi ninampenda zaidi sana mchumba wangu wa zamani na hapa nilipo nina mimba yake na ninatarajia kujifungua hivi punde. Natarajia baada ya kujifungua nianze ukurasa mpya na man of my dream........ Kama kuna ushauri wowote nitashkuru sana

endeleeni kugegedana tuu...mkioana tuu utamu wa kugegedana utapotea....mke au mume wa mtu mtamu ndio maana wasema bado wampenda......alafu nyie wanawake wabaya...so jamaa utambambikia mtoto lol
 
Mistakes zenu nyie watatu.., zitawagharimu victims wawili ambao hawana makosa (watoto wenu na mke wa rafiki yako..)

Acheni utani na roho za watu na maisha ya watoto kama mnaona mmependana na huyo mwenzako tafuta talaka kwa mume wako na rudi kwa huyo jamaa yako, sio kuendelea na uzinzi ambao mwisho wake ni mateso kwa wengine...

Lakini kumbuka, ingawa huyo jamaa ametoa ahadi ya kukuoa KUMBUKA..

wisdompromise1024.jpg
 
Hukumpenda ukazaa nae?Tulia hapo hapo, kama ungekuwa unampenda mchumba wako wa zamani ungevumilia hata mapungufu yake
 
Hiyo ipo sana dada... Wengi wanapanda altareni si kwa kuwa wamependana,bali, matatizo mbalimbali kama yako hayo,wengine kwa kuwa na elimu ndogo,kazi isiyolipa,na mengine kama hayo..
Stori yako inatufundisha mengi. Huyo jamaa alicheat,na hakukueleza ukweli,we nawe ulikasirika,ambapo sasa ni hasira- hasara..
Kifupi,umefanya dhambi kuwa na mahusiano nje ya ndoa hadi kubeba mimba..
Ahadi za kanisani,na maneno ya Padre au Mchungaji wako unayakumbuka,kama"..alichokiunganisha Mungu mwanadamu asiki...."
Unakumbuka kisa cha Prince Charles na Princess Diana? Sina zaidi.
 
Subiri kuungua tu je unakumbuka usemi ya kuwa mpo wangapi?
We endelea!
 
Nikikuita mjinga sjui nitakuwa nimekosea.
Una watoto wawili na bado akili yako inayumbishwa na moyo. Mpumbavu hujali nafsi yake tu watoto anasahau.
Hivi hao watoto wako wawili unataka wahangaike kwa sababu ya moyo wako kwa mtu mwingine?

Mwanaume gani huyo mjinga atakayekubali kuishi na mke aliyevunja ndoa yake, akaja na watoto wake 2 kujumlisha na wa kwake wanakuwa watano!!

Akili yako inakwenda mbele au kurudi nyuma?
 
The shit is getting tough now...lolz
But one thing i can say is a leopard cannot change its spot..sorry to say but you are a bitch in marriage wardrobe..
And better the devil you know than the devil you dont...ishi na huyo uliyenaye unawezaje kudhani mchumbako wa zamani anakupenda kuliko huyu wa sasa wakati alishakusaliti?....mnafanya mapenzi yaonekane kazi ya kijinga sana aisee..lolz!!
 
Nikikuita mjinga sjui nitakuwa nimekosea.
Una watoto wawili na bado akili yako inayumbishwa na moyo. Mpumbavu hujali nafsi yake tu watoto anasahau.
Hivi hao watoto wako wawili unataka wahangaike kwa sababu ya moyo wako kwa mtu mwingine?

Mwanaume gani huyo mjinga atakayekubali kuishi na mke aliyevunja ndoa yake, akaja na watoto wake 2 kujumlisha na wa kwake wanakuwa watano!!

Akili yako inakwenda mbele au kurudi nyuma?

yaani hebu njoo uchukue zawadi yako umemaliza kila kitu,watoto wa mitaani sio wote ni yatima wengine wanatokana na upuuzi kama wa huyu mwanamke anajifikiria yeye tu(ubinafsi) anasahau hao watoto wasio na hatia
 
Mtaka yote kwa Pupa Hukosa yote! Unachezea shilingi chooni mda si mrefu utakosa yote akili ndo itakukaa uzuri!

Ukitembea na mume wa mtu katuuu usiyaamini maneno yake kuwa ATAMUACHA MKEWE NA KUWA NA WEWE!!!!! Hizo story tu! Ngoja ujikute umemuacha mumeo afu yeye atakuwa anakupiga sound tu, wala hamuachi mkewe kamweee!

Kama anakupenda saanaaa kwanini alizaa na huyo dada in the first place? Uridhike na mgegedo sasa ukitaka kujifanya abunuwasi ndio yatakukuta!
 
yaani hebu njoo uchukue zawadi yako umemaliza kila kitu,watoto wa mitaani sio wote ni yatima wengine wanatokana na upuuzi kama wa huyu mwanamke anajifikiria yeye tu(ubinafsi) anasahau hao watoto wasio na hatia

Yaani hafai kabisa kuwa mke! Masikini hao watoto ni kama wanasubiri zahma muda wowote.

Zawadi sisahau lol!
 
25 kwani vp

ndo maana unashindwa kufanya maamuzi ya busara ukidhani we bado mtoto wakati umeshakomaa kabisa,kilichokuharakisha kuingia kwenye ndoa ndo uvumilie sio kukaa unatolea waume za watu macho,tena umkome mume wa mtu kama ndoa yako imekushinda usivunje na ya mwenzio, we umeolewa lakini kiguu na njia kutafuta umbea kwamba wakwe hawampendi mke wa hawala yako badala ya kutafakari maisha yako na watoto hapo baadae itakuaje kama sio kihelehele kinachokusumbua ni nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom