Nampenda lakini sina maisha

Nampenda lakini sina maisha

Maisha ukiyafikiria kesho utakula nini na utavaa nini huwezi kufanya chochote.
Mchukue huyo mwanamke ishi naye ila zingatia uzazi wa mpango. Jichanganye mtaani, tafuta marafiki wenye familia na watu wazima ambao utakuwa urafiki wa kazi. Tafuta kazi hata ya car wash. Familia ni kipimo kizuri sana cha kuwa na maendeleo.
Huwa iko hivi, unapokuwa na shida akili hufanya kazi haraka sana.
N.B
Ongea na dada yako au ndugu yako yoyote akupe hela ya kupanga miezi 3. Nenda kapange mbali na kwenu. Unaamka asubuhi mtoto anataka kula, mzee hapo lazima utoboe
Ahsante kwa Ushauri Ndugu yangu
 
Ng'ang'ana man usimwache naamin huyo ndo mke wako wa kweli ukimwacha utakuja kuoa kituko na utajuta pambana..... Story yako ina fanana na yangu kabisa
Inshallah Mkuu, Pole Kaka Kama ulikutana na hii situation
 
Mwana una issue kama ya kwangu,tofauti mie npo chuo mwaka wa 3 na tyr ana mtoto,saivi yupo kwao..analea mtoto ila nachofanya saivi najibana hela ya boom nayopata,nalipa ada mwnyew,kodi..khs mavazi kibabe t siku znasogea..nafanya yte kujibana kwa ajili ya kesho na mtu wangu,bht nzuri ye ni msusi mzuri(saloon ya kike) hvyo napambana hadi arudi akute ofisi ishakamilka ili kuwepo uhakika wa elf 2 kwa siku kupatkana+mimi nkjchanganya mtaani after chuo..bdo mwaka mmoja kumaliza..

#usimuache huyo mwanamke pambana nae,kwan anafahamu hali yako..cha mno tafta mtaji ata kdg achome ata chapati,atengeneze uji..trust me kama ana nia,una nia dhabiti pia mtatoboa..

kwa alieko mwanza ancheki kwa hii namba
0622902768*
nina shda na mlango.
 
Mwana una issue kama ya kwangu,tofauti mie npo chuo mwaka wa 3 na tyr ana mtoto,saivi yupo kwao..analea mtoto ila nachofanya saivi najibana hela ya boom nayopata,nalipa ada mwnyew,kodi..khs mavazi kibabe t siku znasogea..nafanya yte kujibana kwa ajili ya kesho na mtu wangu,bht nzuri ye ni msusi mzuri(saloon ya kike) hvyo napambana hadi arudi akute ofisi ishakamilka ili kuwepo uhakika wa elf 2 kwa siku kupatkana+mimi nkjchanganya mtaani after chuo..bdo mwaka mmoja kumaliza..

#usimuache huyo mwanamke pambana nae,kwan anafahamu hali yako..cha mno tafta mtaji ata kdg achome ata chapati,atengeneze uji..trust me kama ana nia,una nia dhabiti pia mtatoboa..

kwa alieko mwanza ancheki kwa hii namba
0622902768*
nina shda na mlango.
Ahsante kwa Ushauri wako Brother, Nitafanya Kazi mawazo yako.
 
Kama unakitanda na godoro Apo mchawi Ni ela ya Kodi tu issue ya chakula hua siyo sababu yamtu kuacha kuoa ukizingatia wewe na uyo Dem Amna penzi la mashaka .. haya Maisha ayana formula

Kama una 27 years now unaweza subutu kuoa mahana ukisubiri Maisha yawe poa utajikuta una turn 35 bila kua na stable financial .. ushauri wangu kilakitu nikujarib just try ukishindwa mungu atajua .. uyo Dem akirudi kwao .. kumrudisha Tena siyo raisi ... kwakua Kuna morari itashuka Sana juu yake then mtapotezeana kizembe..

Ungekuw na umbri chini ya 25 ningekuambia mtafutie nauli arudi but iyo over 25 years Kama unataka kua mwanaume halisi jipige kifua usiogope Kama kweli ni mwanamke ulie dhibitisha anasifa zote zakua mke ..wew weka ndani

Tafuta watu wakusapoti kweny Kodi af Anza mwaka ukiwa mwanaume mpya kabsa .. mungu atakuona tu ..
Mkuu fata ushauri huu, narudia tena mtoa mada fata huu ushauri.
 
wanawake wa kanda ya ziwa wapo vizuri ktk kazi uyo ishi nae ye akatafute kibarua hata kwa mama lishe hawa na we utapata mwanga ukiendelea kubaki ktk comfort zone hutoboi umri wa kuamua huo shauri yako, subiri kazi miaka 40 inakukuta hapo hapo ,we ukiweza pata elfu kumi nae akapata elfu saba mnaishi vizuri tu na kodi mnalipa na chenji inabaki,

Dar nimeishi miaka 20 sasa hakuna mji rahisi kama dar hata usipokua na kazi unaishi vizuri tu kikubwa kujichanganya na wahangaikaji.

kama unaona aibu kutafuta dar utaiona ngumu,back to 2013 nilikua ninaaibu kujichanganya ila nikishapiga kijogoo au konyagi ukinikuta ktk mishe mishe unaweza sema sio mimi. Watu walikua wananifurahia sana maneno yao yalikua na baraka dogo utatoboa tu
 
Shukrani Mkuu, Lakini kabla ya uwepo wake kaka nimesambaza San CV mpaka nazikuta kwenye vifungashio vya vitumbua,

Ingekua kijijini ningetumia Mafunzo ya JKT kuanzisha kilimo Cha mboga mboga
Kama kweli unampenda, usimwache arudi kijijini.

Huko anaweza kwenda kupata hifadhi kwa mwingine na ikawa mwisho Wa mahusiano yenu. Cha msingi komaa na ishu yeyote halali hata kuanzisha Genge ili maisha yenu yasonge mbele.
 
Sorry dogo kwa nitakalo ongea huenda halitakufurahisha lakini linaukweli ndani yake, Kwanza siku hizi kupata mke unayeona anafaa kuwa mke ni bahati Sana hivyo kuachia huyu binti kizembe kizembe unaweza ukajuta huko mbeleni pamoja na kukaa vizuri unakofikiria kiuchumi ambalo ni dhana fikirika, pili dogo tujifunze kunyumbulika tusitegemee vyeti na CV, kama kijana anaweza kutoka mtwara, njombe na maeneo mengine akanza uza maji na biscuti na akawa na hela ya kujikimu na baadae akajenga nyumba na amekuja na mtaji usiozidi elfu 50000/_ hapo hakai kwao SEBUSE wewe unakaa kwenu na una wazazi karibu. Dogo fanya maamuzi magumu kujitegemea maadam huyu binti awe anakupenda kweli na anakusikiliza, siku life limekaa vizuri usimwache lakini
 
Sahihi mkuu, Acha nipambane.. lakini kwa wakati huu nifanye Nini mkuu? Nimtafute nauli au nikomae nae tu?
Komaa nae babu, akili itachanganya na fursa za mtonyo kibao utaziona, ukilegeza akirud mkoa unaweza ukapokonywa kiwepesi tu wenye nia nae.
 
Hii ndio summary ya huu uzi:
Huna hela...
Huna kazi...
Huna makazi yako...
Huna uhakika wa milo mitatu kwa siku...

Unataka uwe na mwanamke ambaye hata kwao hawakutambui...
Unataka umpatie ujauzito huyo mwanamke ili uanzishe familia...

Soma kwa taratibu haya niliyoandika, usisome kwa kutumia akili bali tumia moyo, chukua muda kuyatafakari na uweke jawabu kwenye kila kimojawapo...

Mahali ambapo na Huna, jaribu kutafuta jawabu la jinsi gani Utakuwa na....

Jifunze kitu kimoja, nyumba huwa haisimami bila msingi wa kuibeba, wala mti huwa hausimami pasipo mizizi ya kuuliza...
 
Wakuu Habari za muda huu, niende moja kwa moja kwenye mada.

Hii inanihusu Mimi mwenyewe na hapa Nawaza na kuwazua na sipati jibu sahihi, Nachanganyikiwa.

Mimi Ni kijana mwenye miaka 26, Elimu yangu Ni kidato Cha Sita na pia nilisoma Certificate in Clearing and Forwarding, Naishi Dar kwa Wazazi Ila nakaa chumba Cha nje Cha Peke angu,

Kwa muda Sasa nilikua nikitamani kuwa na familia, Yani mke na mtoto, ukizingatia rafiki zangu karibu wengi Wana maisha Yao na familia zao, niliwahi kuajiriwa lakini kwa Sasa Sina Kazi ya uhakika nadandia tu mishe yeyote itakayokuja mbele yangu.

Sasa Kuna huyu binti, mtoto wa Kanda ya ziwa, mzuri, binti mdogo miaka 20(Asomi) alikua akifanya Kazi za usaidizi za ndani, Muuni nikamuelewa nikaanzisha mahusiano nae, baada ya miezi kadhaa mwajiri wake akayumba Kiuchumi na kumuachisha Kazi.

Binti Hana ndugu mjini, kwao Ni mbali na maisha ya kwao pia wanamuangalia yeye ndio mwokozi wao, Kimsingi binti ananipenda na Mimi pia Nampenda na ndio msichana ninaetamani kuishi nae na kutengeneza familia.

Tatizo linakuja hapa, Mimi Jobless, kula kwa kengele japo sio kila siku kwasababu nikiwa na mishe zangu napenda kujitegemea kuliko kusumbua home, huyu mtoto wa watu nataka kumsaidia, nataka asiwe mbali na Mimi kusudi Mambo yangu yaki tiki niishi nae.

Kwa Sasa nimemuombea hifadhi kwa Dada yangu japo ya siku kadhaa na tayari Nina siku tano tu mbele za kujua hatma yake.

Nawaza nifanye Nini?? Nimtafutie nauli arudi kwao?? Nikae nae kibishi, atakula Nini? Ana mahitaji mtoto wa kike na Mimi Ni hohe have?? Naomba ushauri wakuu.
Natanguliza Shukrani.
Jaribu uone
 
Nyie ndio mnasemaga mnasikilizia mchongo siyo? Komaa Dogo toka nyumbani kisha urudi jioni utajifunza maisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom