Nampenda lakini sina maisha

Nampenda lakini sina maisha

Sahihi mkuu, Acha nipambane.. lakini kwa wakati huu nifanye Nini mkuu? Nimtafute nauli au nikomae nae tu?
Hiyo nauli ya kanda ya ziwa haipungui elfu sabini,huo ni mtaji kabisa,
 
Kweli Ni Jobless lakini ku fight na fight na yes sikosi mbili tatu, lakini kwa kumuweka ndani mzee ntachemka kabisa... Ahsante kwa ushauri pia
Mambo kama haya huwa hayahitaji ushauri wamtu mwingine fanya unachoamini miaka uliyonayo bado unaogopa jambo dogo hivi naamini utakachoamua ww ndio kitakuwa sahihi
 
Hii ndio summary ya huu uzi:
Huna hela...
Huna kazi...
Huna makazi yako...
Huna uhakika wa milo mitatu kwa siku...

Unataka uwe na mwanamke ambaye hata kwao hawakutambui...
Unataka umpatie ujauzito huyo mwanamke ili uanzishe familia...

Soma kwa taratibu haya niliyoandika, usisome kwa kutumia akili bali tumia moyo, chukua muda kuyatafakari na uweke jawabu kwenye kila kimojawapo...

Mahali ambapo na Huna, jaribu kutafuta jawabu la jinsi gani Utakuwa na....

Jifunze kitu kimoja, nyumba huwa haisimami bila msingi wa kuibeba, wala mti huwa hausimami pasipo mizizi ya kuuliza...
Nimekuelewa mkuu, Ahsante kwa Ushauri
 
Wakuu Habari za muda huu, niende moja kwa moja kwenye mada.

Hii inanihusu Mimi mwenyewe na hapa Nawaza na kuwazua na sipati jibu sahihi, Nachanganyikiwa.

Mimi Ni kijana mwenye miaka 26, Elimu yangu Ni kidato Cha Sita na pia nilisoma Certificate in Clearing and Forwarding, Naishi Dar kwa Wazazi Ila nakaa chumba Cha nje Cha Peke angu,

Kwa muda Sasa nilikua nikitamani kuwa na familia, Yani mke na mtoto, ukizingatia rafiki zangu karibu wengi Wana maisha Yao na familia zao, niliwahi kuajiriwa lakini kwa Sasa Sina Kazi ya uhakika nadandia tu mishe yeyote itakayokuja mbele yangu.

Sasa Kuna huyu binti, mtoto wa Kanda ya ziwa, mzuri, binti mdogo miaka 20(Asomi) alikua akifanya Kazi za usaidizi za ndani, Muuni nikamuelewa nikaanzisha mahusiano nae, baada ya miezi kadhaa mwajiri wake akayumba Kiuchumi na kumuachisha Kazi.

Binti Hana ndugu mjini, kwao Ni mbali na maisha ya kwao pia wanamuangalia yeye ndio mwokozi wao, Kimsingi binti ananipenda na Mimi pia Nampenda na ndio msichana ninaetamani kuishi nae na kutengeneza familia.

Tatizo linakuja hapa, Mimi Jobless, kula kwa kengele japo sio kila siku kwasababu nikiwa na mishe zangu napenda kujitegemea kuliko kusumbua home, huyu mtoto wa watu nataka kumsaidia, nataka asiwe mbali na Mimi kusudi Mambo yangu yaki tiki niishi nae.

Kwa Sasa nimemuombea hifadhi kwa Dada yangu japo ya siku kadhaa na tayari Nina siku tano tu mbele za kujua hatma yake.

Nawaza nifanye Nini?? Nimtafutie nauli arudi kwao?? Nikae nae kibishi, atakula Nini? Ana mahitaji mtoto wa kike na Mimi Ni hohe have?? Naomba ushauri wakuu.
Natanguliza Shukrani.
Huyo ukimuacha aende peke yake kijijini yatakukuta yaliyomkuta kagwa, kule kuna watu wanakula ugali kilo tano na maziwa debe moja kila siku watamshona atakusahau

Ushauri wangu kama unampenda wew fanya mpango tafuta pesa uende nae huko kijijin kwao(kanda ya ziwa) kule kuna mishe nyingi, kama uvuvi,ubebaji mizigo nk.

Unaweza ukanunua hata kaplot kadogo ukakafanya kama bustan and who knows? Baadae unaweza ukapata mtaj mkubwa na ukafanya makubwa zaidi ukiwa na huyo demu wako.
 
Huyo ndio nyota wa mchezo mtafutie kibarua hata kiwandani,Atakusaidia kukupa changamoto ya kupambana.
 
Mkuu ukifikia maamuz ya kumrudisha kwao nichek, aje moshi kuendelea na ajira yake, nina uhitaji na dada wa nyumbanii
 
Mshirikishe Mungu kwanza,karibu tuishi sio nzur kimaadili, lazim ufate taratib km vile kwenda kwa wazaz ili wakukabidh,ukiamua kumchukua bila ruhusa ya wazazi wake, je km ana matatizo huyo bint, je? yakutokea hakuna atakayekuelewa hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuhusu vitu vya ndani tayari ninavyo, Kitanda, Godoro, Sofa na vingine vidogo vidogo, Ishu Ni kwamba tu Sina mchongo wa uhakika wa kunifanya Ni survive na mtoto wa mtu
Siatakula chakula Cha kwenu huku ukipambania upate kaz,shida Nini?unacomplicate maisha mwnyw,mi sikushaur aondoke,ww mtaftie hata lak mbili afanye biashara ndogo ndogo ziwasaidie ukiwa unatafta kaz
 
kama kweli umeamua kujilipua jilipue tuu, ww una had pa kulala kuna wanafamilia walianza kwa kulala kwny baraza hawana pa kulala lkn wapambana mpka kikaeleweka.

muhimu n kuamua kwa dhati, hakuna kinachoshndkana.
 
Nikushauri tu,, hao viumbe ni watu wa hovyo sana... Kama unamchukua ili akupe challenge au akutoe kwenye comfort zone basi utakuwa sahihi,, maana yake lazima akili ikukae sawa..

Ila kama ndio unawaza ndoa,, kila la kheri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom