SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,240
- 4,270
Kabla ya kuanzishwa kwa mtindo mpya wa usajili wa magari, magari yote nchini yalisajiliwa kwenye makao makuu ya kila mkoa. Kwa hiyo namba zilitumia jina la mji mkuu, mathalani kama ni Arusha, namba zilianza na AR, kama ni Moshi MS nk.Ili kuandikisha magari mengi zaidi herufi za miji zilinyambuliwa kama vile ARA MSA nk. Moshi kulikuwa na MSB ambayo ilizua utani maarufu wa Mchaga Si Binadamu.Sijui watu wangezua utani gani kama Arusha ingekuwa na namba ARV..........