Namba 11:11 or 1111

Namba 11:11 or 1111

Financial Analyst

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2017
Posts
2,123
Reaction score
4,577
Tangia 2017 nilianza kupitia hali ya ukumbusho wa mara kwa mara ili nizione namba 1111 pale zinapokuwa zimetokea au kuwako sehemu. Sio asubuhi, mchana au usiku. Mara nyingi nimekuwa nikiziona katika saa yangu ya mkono, PC au simu (11:11). Sio ishu ya kuangalia muda wakati wote, yani najikuta inanipata hali inayonifanya kuangalia sehemu au simu na kukutana na hizo namba.

Mara nyingi nilichukulia poa hadi ilipofika mwaka huu, nilipoamua kufanya research kwa nini naona hizi namba mara kwa mara.

●Wataalamu wa saikolojia wana claim ni hali tu ya kiakili inayokukumbusha uangalie hiyo namba either kwenye saa kwa sababu kuna jambo la ukumbusho liliwahi kutokea muda huo or katika sehemu yenye namba kama hiyo.

●Watalaamu wa namba (numerologist) wana sema ukiwa unaona hizo namba mara kwa mara ni ukumbusho kuwa unalindwa or guided na presence ya kiroho kati yako.

●Watalaamu wengine wanasema ukiona hizo namba mara kwa mara ni kukumbusha na kualert kuwa uchukue hatua ili ujijenge kiroho, kimwili na kiakili ili ujikinge na madhara na changamoto tofauti zinazokuja.

●Watalaamu wengine wanasema ni nguvu yako ya kiroho inakuonesha opportunity/fursa ya wewe kukuwa kiakili, uwezo wa fikra, uponyaji na upendo na kupanda ngazi za juu za kiroho na kukuonesha upo katika njia sahihi kwa ajili ya mafanikio yako.

●Wengine wanasema ni sign ya presence ya malaika wako inapokuwa nawe, kukulinda na kukuogoza.

Je na wewe umekuwa na hali ya kuona hizo namba au nyingine za kujirudia rudia mara nyingi?

For whatever reason why i am seeing these numbers often, i pray and hope it is of good terms.
 
I SWEAR TO GOD, HILI JAMBO HUWA NALIONA MARA KWA MARA NA HUWA NAJIULIZA SANA AU WALE JAMAA WA UPANDE WA PILI WANANISAKA NINI???!I MEAN FREEMASONS??
Cc Mshana Jr aka platinumz
 
Siku mkiacha kuwaza mauzauza haya mtaendelea, uchawi sijui dini sijui madude gani mkiweka pembeni mtashangaa mafanikio yanavyokuja. Seriously people stop this nonsense, hivi waafrika mna shida gani?
 
Mimi huwa nakutaga 5:55 hii nayo sijui tusemeje tena tangu nipo primary school mpaka sasahivi hadi nashindwa kuelewa kuna siri gani katika hili.
 
Duh ! Umenifikirisha sana maana mimi huwa naangalia zaidi saa kwenye simu ya mkononi na mara nyingi sana hukutana na 22:22. Mpaka nilishajiuliza kwani lazima ikifika saa nne na dk.22 usiku niangalie saa ?
 
Namba zangu za mawasiliano zinaishia na 11111 zote tatu,(tigo, ttcl, Airtel) maana yake nini mm nazitaja kila siku na hiyo kitu usemayo nakutana nayo sana 11:11
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom