DELETED ACCOUNT
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 9,805
- 15,470
Sikatai. Chama ni zaidi ya Ahoua ila Simba mpya ilibidi ijengwe na sipendekezi kurudi nyuma maana itaendelea kupata shida kufunga ukurasa wake. Ni kama ilivyochukua muda kupata ujasiri wa kumuacha Zimbwe, bila kumuacha ingeendelea kusajili wachezaji mbadala na kusingizia hawatoshi kumbe zimwi la uwepo wake linafunika fursa ya kupata wachezaji wapya.Kwa uwezo wa wachezaji waliopo Simba kwa sasa na ukamuongeza mchezaji kama CHAMA anaweza kukupa kitu cha ziada chenye thamani zaidi kwenye mechi.
Ni tatizo hilo hilo lipo timu ya taifa. Mbona wenzetu wanaibua wachezaji wapya kila siku na ndiyo hao hao tunawakimbilia na kuwasifia, kwa nini na sisi tusipate ujasiri huo?