matumbo
JF-Expert Member
- Jul 9, 2011
- 7,224
- 3,958
sasa wewe si useme huyo Sugu amefanya nini? mmefanya makosa makubwa kuchagua mbunge kihiyo na adhabu yake ndio hiyo
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi âSuguâ ameonesha falsafa ya kuongoza kwa vitendo baada ya kutoa msaada utakaowezesha kujengwa kwa daraja kwenye Kata ya Itende.
Wananchi wa Itende, walimlilia Sugu kuwa daraja hilo limekuwa kikwazo kwa maendeleo yao, pia linahatarisha maisha ya watu ambao huvuka kila siku.
Daraja hilo, limewekwa miti juu, hivyo kuhatarisha maisha ya watu wanaopita, wakilitumia daraja hilo kama njia yao kuu.
Sugu, aliwatembelea wananchi wa Itende na kutoa fedha taslimu ambazo zitawezesha kujengwa kwa daraja hilo kwa kiwango cha zege.
Hata hivyo, vyanzo vya habari hii havijaweka wazi kiasi ambacho Sugu alikitoa kufanikisha ujenzi huo, isipokuwa vilieleza: âMheshimiwa Sugu ametoa fedha zote zitakazofanikisha ujenzi wa daraja hilo.â
Baada ya kutoa msaada huo, Sugu aliwataka wananchi wa Itende kushirikiana naye katika kuleta maendeleo Mbeya Mjini.
Wananchi wa Itende, walimlilia Sugu kuwa daraja hilo limekuwa kikwazo kwa maendeleo yao, pia linahatarisha maisha ya watu ambao huvuka kila siku.
Daraja hilo, limewekwa miti juu, hivyo kuhatarisha maisha ya watu wanaopita, wakilitumia daraja hilo kama njia yao kuu.
Sugu, aliwatembelea wananchi wa Itende na kutoa fedha taslimu ambazo zitawezesha kujengwa kwa daraja hilo kwa kiwango cha zege.
Hata hivyo, vyanzo vya habari hii havijaweka wazi kiasi ambacho Sugu alikitoa kufanikisha ujenzi huo, isipokuwa vilieleza: âMheshimiwa Sugu ametoa fedha zote zitakazofanikisha ujenzi wa daraja hilo.â
Baada ya kutoa msaada huo, Sugu aliwataka wananchi wa Itende kushirikiana naye katika kuleta maendeleo Mbeya Mjini.