Naliona anguko la mbunge wa Mbeya Mjini

Naliona anguko la mbunge wa Mbeya Mjini

dah kuna watu yaan wanalipwa kwa kupost thead za ccm na kupondea comment za chadema japo zina maslai kwa wananchi polen sana ndo madhara ya kuendekeza tumbo
 
Unaelekea ulirithishwa mikoba ya gizani ya Sheikh Yahya Hussein kabla hajafariki. Haya tuambie unaona nini kuhusiana na magaidi ambao hawatarudi mjengoni 2015.

Umeandika sawasawa mkuu, hata mimi iki kitu nakiona, na sio Sugu tu, na wengine wengi wa CHADEMA hawatarudi 2015 pale bungeni.
 
mi naishi block t,jiran na makao ya Sugu na Mary Mwanjelwa,kiukweli sion tofauti ya Sugu na Mpesya,wote chenga tu..

Majina mengine haya jamani....!! sugu nd'o nini...?? Kweli anayetegemewa kutunga sheria za nchi anaitwa sugu....??!! Nd'o maana wakoloni mambo leo wameteka njia zetu zote za uchumi..!
 
Kibwete na wenzio mkajipange tena sana tuu! Mengi yamefanyika chini ya mbunge wetu sugu katika kuhakikisha fedha ya wanambeya inatumika ipasavyo kutuletea maendeleo kitu ambacho mpesya na serikali yake mbovu ya ccm walishindwa kukifanya! Bado tutamuhitaji sugu
 
Naungana na mtoa mada kwa matusi yake yy na msigwa sidhani kama watarudi
 
mkuu mi natokea Mbeya maeneo ya Samora Secondary ? Na sina ushabiki ila sielewi labda uniambie ilitakiwa afanye nini zaidi ya aliyoyafanya au toa mfano wa jimbo ambalo linafaa kuwa mfano wa kuigwa ukilitofautisha na lilipokuwa chini ya Mpesya ?

sasa wewe si useme huyo Sugu amefanya nini? mmefanya makosa makubwa kuchagua mbunge kihiyo na adhabu yake ndio hiyo
 
dah kuna watu yaan wanalipwa kwa kupost thead za ccm na kupondea comment za chadema japo zina maslai kwa wananchi polen sana ndo madhara ya kuendekeza tumbo

kwa hiyo wote tupende itikadi yako ndo uamini hatulipwi?
 
DUH!....kama kweli abadilike na kama co kweli acheni propaganda za kijibwa mwehu.
 
bt pia mtoa mada kajifunze kuandika inaonekana matumizi ya R na L tatizo kwako.
 
Majitu mengne sijui ya wapi badala ya kuangalia miaka 50 wamepata nini eti sugu hajafanya kitu kwel unafikiri kwa kutumia makalio
 
Mimi ni mpita njia tu lakini haya matusi! Sio hoja ni matusi hayavumiliki. Mh. Sugu upo juu na utaendelea kuwa Raisi wa wana Mbeya na siyo Mbeya Mjini tu. Huyu mtoa lugha chafu,kashfa,dhihaka nadhani leo ni May mosi ungeanza kwa kutueleza Nampesya alifanya nini katika uongozi wake hadi wananchi wakaamua kumtupilia mbali? Niendelee tu kutoa Rai kuwa wanajamii forum hawapigi wote kura manake ni watu wa mikoa tofauti, hivyo ili lengo lako likamilike nenda Uyole nenda Mbeya mjini ukatoe hyo elimu kwa hao Vijana waliochoka na chama chako kwa zaidi ya 50yrs uone matokeo yake, kama JK kule alipigwa mawe na ulinzi wote huo alionao? Wewe mbwa kachoka usiye na hata chembe ya mbwa wa kukulinda? Si wataku**ra? Angalia Mkuu kaenda kuomba msamaha kule kwa matendo ambayo anawafanyia watanzania [kodi za watanzania] ulinzi wote wa nchi umehamia Mbeya unajua kwanini? Mbeya hawana hizo elimu za kuungaunga lakini hadi yule mwenye hali ya chini anajua baya na zuri. Ukitaka kuamini sugu jembe? Vurugu zilizotokea mbeya! Wamachina na bodaboda juu ya serikali yao ikumbukwa baada ya vyombo vya usalama kushindwa akiwamo mkuu wa mkoa, vijana walisikika wakipiga kelele, "tunamtakaaaaa? Rais wetuuu{sugu}. Serikali ilimpigia simu akiwa bungeni na kumlipia garama za usafiri alipofika mbeya tu hakuwa na mabomu wa maji ya kuwasha isipokuwa alitumia Psychological Techniques ku compromise solution. Akili ndogo sana. Ingekuwa ni huyo unayemtaka ungekuta walikufa wengi.
 
Hata kadi ya ccm siijui inafananaje wasiwasi wako tu sipo huko unapofikiria ila kwa sababu ccm ndo wanafanya usilale shauri yako,nambie uzaifu up wa viungo au wa kitu gani jipambanue siyo unaandika vipande vidogo kama mazoea mitomingi.
sasa wewe ni mwongo kabisa, hata kadi ya ccm hujui inafananaje!?
 
Kaka kama kunamtu Mbeya asiye na ushabiki ukiongea naye atakupa clear picha.



Sugu akusanya milioni 8 mfuko wa elimu
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’, ameendelea kuzoa mafanikio kupitia mfuko wake wa elimu.
Sugu, alianzisha Mfuko wa Elimu Mbeya (MBETF) kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wasiojiweza kwenye Jimbo la Mbeya Mjini waweze kusoma bila matatizo kuanzia sekondari mpaka vyuoni.
Sugu2013.jpg

Sugu%20MBETF.jpg

Kwa mujibu wa Sugu, ameweza kukusanya kiasi cha shilingi 8,350,000 kutoka kwa makampuni mbalimbali ambayo yamejitolea kuuwezesha mfuko huo kutimiza malengo yake.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Facebook, Sugu ameandika kuwa Coca Cola Mbeya, imetoa shilingi 5,000,000, Lafarge-Mbeya Cemente shilingi 2,000,000 na Kampuni ya Mbeya Tanzania (TBL) shilingi 1,000,000.
Aliyataja makampuni mengine yaliyochangia kuwa ni Benki ya CRDB-Mbeya shilingi 200,000, Mwamikomo Store shilingi 150,000 na Access Computers waliotoa kompyuta moja kwa ajili ya ofisi ya MBETF, iliyopo Kata ya Nzovwe, Mbeya.
Sugu ameandika: “Mimi Joseph Mbili, Mbunge wa Mbeya Mjini na Mwenyekiti wa Mfuko wa Elimu Mbeya (Mbeya Education Trust Fund) pamoja na bodi yetu ya wadhamini, tunapenda kutoa shukurani zetu za dhati kwa makampuni hayo kwa kuchangia mfuko wetu.”
Aliongeza: “Ewe mwana Mbeya na rafiki wa Mbeya popote ulipo, tafadhali changia mfuko wa elimu ili tufikie malengo ya kupeleka sekondari watoto wasio na uwezo wapatao 360 kwa mwaka huu 2013. Akaunti yetu ni 01J50421214700 CRDB BANK Mwanjelwa Branch kwa jina la Mbeya Education Trust Fund.”
 
Naungana na mtoa mada kwa matusi yake yy na msigwa sidhani kama watarudi

ma2si yepi yanayochukza kwa m2 kati kuambiwa mpumbavu au mbwa, au 2si la Lusinde, 2si la Al-Shabab, Gaidi Nchembe na wapumbavu wengine?
 
Mheshiwa sugu ni miongoni mwa wabunge waliochaguliwa kwa kishindo kiasi kwamba wananchi walifulika eneo la kuhesabia kura kulazimisha matokeo yatangazwe halaka na ikawa hivyo sugu akawa mbunge.tangu aingie bungeni impact yake kwenye jimbo lake la uchaguzi haijaonekana na pengine imefika mahala baadhi ya watu wameanza kufikiria tofauti juu ya mbunge huyo na pengine kusema wazi kuwa hana anachofanya zaid ya kubishana bungeni kwa mambo ambayo hayana msaada kwa jimbo lake la uchaguzi.kikubwa kinachosubiliwa mbeya mjini ni uchaguzi mkuu ili wakaazi wa mbeya waamue vinginevyo na uzuri wa watu wa mbeya wanachagua mtu si chama kwa hiyo itategemea sugu atapambana na nani toka vyama vingine ktk uchaguzi mkuu ujao.

Join Date : 20th April 2013
Posts : 183
Rep Power : 338
Likes Received8
Likes Given3
[h=2]
icon1.png
yale yale ya wanajamvi wa 2013[/h]
 
Nimeamini CHADEMA kinawasumbua kweli, wabunge wangapi wa CCM watarudi ndugu? wasiojua hata wanamwakilisha nani bungeni, wamebaki kutetea maslahi ya watu binafsi, chama na serikali. AMKA USINGIZINI Ndugu.
 
Back
Top Bottom