.
Kwangu mimi Rostam, Sitta, Lowassa, Chenge, Mwakyembe na wengine wote ni vyanzo muhimu vya habari na kwa Tanzania Daima wana nafasi sawa kihabari. Msimamo wangu huo uko bayana na kimsingi hatufungamani na upande wowote.
.
Nilikataa tangu mapema kujiingiza katika vita ya ufisadi inayopiganwa na akina Sitta na akina Mwakyembe kwa sababu nimejiridhidhs kwamba ni vita ya kitapeli.
KIBANDA KWA HILI TUKO PAMOJA ! sema tu, nimekuelewa na ninatayarisha nakala ya kutetea na kuuelewesha umma unamaanisha nini! just simple logic is needed!
Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, anafanya kazi part-time kwenye magazine inayomilikiwa na Edward Lowassa inaitwa UMOJA. Pia Kibanda amekuwa anatoa habari za kumbeba Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge kwenye Tanzania Daima mara nyingi. Kwa kupokea maagizo na malipo kutoka kwa Lowassa na Rostam Aziz, Kibanda pia amekuwa akiandika habari na makala nyingi za kuwakashifu Samuel Sitta, Harisson Mwakyembe, Bernard Membe na John Magufuli.
Tanzania Daima ni moja ya magazeti yanayotumiwa na fisadi Rostam Aziz kutetea ufisadi mbalimbali, ikiwemo malipo kwa Dowans kwa nguvu zote. Wanaitumia Tanzania Daima kwa kuwa gazeti linaaminika kuwa ni huru na ni rahisi ku-brain wash watu kuliko kutumia Mtanzania/Rai ambayo Watanzania hawayasomi tena sasa baada ya kugundua kuwa yanamilikiwa na Rostam.
Cha kushangaza ni kuwa mmiliki wa Tanzania Daima, Freeman Mbowe, anaachia tu gazeti lake litumiwe na mafisadi kupitia kwa Kibanda kuangamiza nchi.
[/B][/COLOR]
Kabla hujashangaa, jiulize kama Freeman Mbowe anaweza kuwa mfuasi mzuri wa Dk. Slaa!
Ni kwamba Slaa yuko peke yake, akizungukwa na wasanii kama Mbowe na Zitto Kabwe. Mbowe hawezi kuwa safi, hata kwa OMO. He is a business man, and that says it!
CHADEMA wanatakiwa waanzishwe gazeti lao, TV yao na Redio yao. Tanzania Daima is hijacked.
You can't trust Mbowe, I am sorry.......
Pole sana Kibanda! Umesahau kitu kimoja... Kusoma ni jambo moja na kuelewa ni jambo jengine! Baadhi ya wasomi wetu wa kileo, upeo wao ni mdogo sana, kwa sababu wao wanataka kuamini kile walichokwishaamini hivyo basi anaweza kusoma paragraph moja tu, akahitimisha habari nzima na kutoa hukumu zake. Hapo ndipo wanapozusha na hawaambiliki!!
Hivi kama wao ni wakweli na wana-kumbukumbu basi watuambie ni KWANINI MWALIMU ALIKUWA HAMTAKI SS? Na kama SS si mbinafsi na mwenye kupenda kujitenga alikuwamo katika G55!! Na kama kweli yeye SS ni mwenye uchungu na nchi na hana uchu wa madaraka na kupenda sifa KWANINI JENGO LA SPIKA LIJENGWE JIMBONI MWAKE NA SI DODOMA ina maana alitaka USPIKA - UKAMUZU BANDA!?)
Jarida la UMOJA halimilikiwi na Lowassa. Mimi si mtu wa kufanya kazi kwa mtu kwa kujificha hata siku moja. Wewe ni ndugu yangu kwa nini uwapotoshe Watanzania wanaosoma thread hii. Ni vyema ukiwaeleza udhaifu wangu wa kweli. Kama ningekuwa ninatawaliwa na fedha nisingekuwa Tanzania Daima leo. Kosa langu ni kuruhusu mijadala huru katika Tanzania Daima.
Nitakuwa ninakwenda kinyume cha dhamira yangu nikianza kuzuia habari zinazowahusu akina Lowassa, Rostam, Chenge na wengine kama wanavyofanya wahariri wengine. Nimekataa kuwa mnafiki kujifanya nawapiga vita watu fulani fulani na wakati huo huo nikikutana na watu hao mafichoni. Namshukuru Mungu nimekuwa mhariri katika kipindi ambacho kikundi fulani chenye nguvu katika media kilipoamua kutumia media na kututumia sisi waandishi kuwafunga midomo wengine na kuwachafua wengine.
Wakati waandishi wa habari wengi wakipiga kampeni za kumuunga mkono Kikwete mwaka 2005 hata kuliunga mkono kundi la mtandao ambalo moja ya sera zake zilikuwa ni kuwachafua akina Dk. Salim, Sumaye, Malecela etc baadhi yetu tulisimama kidete kupinga kosa hilo la kuwachafua wengine kwa sababu ya urais. Nitakuwa mpumbavu iwapo nitakubali leo hii kikundi cha watu wengine wawachafue wengine kwa sababu tu ya urais wa mwaka 2015. Kosa hilo nimelikataa.
Ni jambo jema kwamba Mbowe anazijua siasa za nchi hii, anawajua vyema ninyi akina informer na anaujua unafiki wenu. Wewe mwenyewe alikuwa akuajiri mwaka 2005 lakini kwa tamaa zako za fedha ukaenda kwa mwajiri mwenye pesa. Laiti kama familia ya Mbowe ingekuwa ni ya kusikiliza majungu na uzushi wa akina informer ingenifukuza kazi zamani. Wasomaji wa Tanzania Daima endeleeni kusoma gazeti hili na ikibidi andikeni hata makala za kupinga mitazamo yangu na ya wengine kwani huo ndiyo uhuru wa habari. Siogopi challenges za kukosolewa, kupingwa na hata kuzushiwa. Niko thabiti, namshukuru Mungu