Nakusudia kumshtaki baba yangu

Nakusudia kumshtaki baba yangu

Pole Sana,inasikitisha
Wazee wengine Kama wamelogwa vile yani
 
Na hapo si mzee tu kuna wadogo zake pia wangeweza kumgeuka pia.
Hapa alibugi.
Unapokuwa na familia unaacha kila kitu na ndugu wote unashirikiana na mkeo kutengeneza maisha ya watoto.
Kosa pia alifanya hapo. Hii ya kuacha hati kwingine na yeye yupo eneo tofauti ni mbaya sana.
 
Sijaona kosa la baba’ko hapo, umeandika mengi ila ukahitimisha kinachokuuma ni 16m tu... itakuwa umeanza kufirisika hivyo unatafuta wa kumbebesha lawama.

Tafuta hela nyingi bwashee, ukizipata tafuta zingine... mwache mzee ale mafao usisahau keshakwambia umlipe gharama za matunzo.

Cheers 🥂
 
Na hapo si mzee tu kuna wadogo zake pia wangeweza kumgeuka pia.
Hapa alibugi.
Unapokuwa na familia unaacha kila kitu na ndugu wote unashirikiana na mkeo kutengeneza maisha ya watoto.
Migogoro ya kifamilia ni mizito sana hasa mzee akiyumba kiuchumi tofauti na alivyokuwa awali lazima uadui utokee kati ya watoto ama mke.
 
Pole sana mkuu, huyu mzee alikutunza vyema wakati hajaanza kufanya huo unaoita upumbavu au alikuwa hivyo tangu zamani?

Je ana mgogoro na mkewe yaani mama yako.?

Umewahi kufuatilia japo kujua chanzo cha yeye kurudi nyuma kiuchumi ni nini.?
Mkuu mzee wangu sitaki kumsema uongo alinitunza vema sana tatzo la uhuni na alipoanza kupata pesa alibadilika sana na hapo ndipo uhuni ulipozidi mpaka mda huu tunafikishana huku na sijui kakamatwaje kwa sasa kawa ni zaidi ya MPUMBAVU ukoo mzima unamshangaa. Yaani Kama nisingesimama kwenye familia basi Hawa madogo wangekuwa wanajiuza na wengine machokoraa hakukuwa na msaada mwingine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sina neno zuri la kutumia zaidi ya kusema nimebahatika kuzaliwa na baba mpumbavu sana, mjinga na asiyejielewa, sina mantiki ya kumdharau baba yangu lakini mpaka hapa nilipofika Sina budi kusema ni mjinga na imefika hatua namchukia kwelikweli Kuna misemo mingi ya wahenga kuhusu wazazi lakini wengine ni gundu, Mimi pia ni baba wa watoto 4 lakini huyu mzazi wangu hafai kuigwa na mzazi yeyote aliye smart.

Stori ni ndefu sana hapa naifupisha kidogo, Huyu baba yangu hana maisha ya dhiki ni mtu mwenye uwezo wa kufanya chochote anachotaka pamoja ya kuwa na miradi hajawahi kuishirikisha familia na hakuna anaejua miradi yake ilipo hata Mimi pamoja na kusikia tu kwa watu sijawahi kumuuliza na wala hilo halijawahi kuwa tatzo kwangu na wadogo zangu.

Tatizo ni hili,Kuna kipindi baba yangu alifirisika alichoka sana kiuchumi, kipindi hicho Mimi nilikuwa vizuri kiuchumi baada ya kumaliza chuo wajomba zangu waliniwezesha nikawa nina miradi ambayo ilikuwa inatoa profit nzuri kipesa na kiutafutaji nilikuwa mkoa tofauti na wazazi na tulikuwa karibu sana kimawasiliano. Siku moja Baba alinipigia simu akiniomba tuongee kwa kina , yalikuwa maongezi marefu lakini kikubwa alikuwa ananiambia amefirisika na gari zote alizokuwa nazo ameuza na alihitaji msaada wangu wa kuinua uchumi wake. Ilibidi nifunge safari kurudi nyumbani kwa wazazi ili tuzungumze vizuri sikutaka kufanya maamuzi nikiwa mbali nikiwa sijui ukubwa wa tatzo.

Na hii ndio ilikuwa mara ya kwanza kuongea na baba yangu kwa kina hakuwahi kunishirikisha kwenye mambo yake yoyote yale, tulizungumza kwa kina na ilikuwa siku nzuri sana kwetu na familia kiujumla tulifika muafaka kwa ustawi wa familia na wadogo zangu ambao walikuwa bado wako shule ambao walihitaji msaada zaidi kufika malengo yao na kwa vile pesa aliyoomba ilikuwa ndani ya uwezo wangu nilimpa mara 2 ya kile alichoomba nikamnunulia na gari la kutembelea, na hapa niseme ukweli pamoja na kwamba nyumbani kulikuwa na magari baba yangu alikuwa hataki kuona watoto tunajua kuendesha lakini kwa vile mjomba alikuwa na gari na mwanae alikuwa anajua aliweza kunifundisha na nikawa najua na sikuwahi kuendesha gari la baba alikuwa haruhusu mpaka anafirisika, Sasa kulingana na ufinyu wangu wa mda kuna nyumba ilikuwa inauzwa huo mkoa anaoenda kuwekeza nikampa pesa zingine ili akamilizie kunilipia na achukue document zote kwa niaba yangu na aninunulie viwanja kadhaa ambavyo tayari nilikuwa kwenye mawasiliano na wauzaji.

Kipindi chote tukawa tunawasiliana na kumuweka karibu na wale wauzaji na nyumba na viwanja ili kuhakikisha anavinunua na kuhusu maendeleo ya miradi yake aliyofungua. Sikujua chochote ndani ya mwaka mzima mpaka pale mdogo wangu aliyekuwa anaingia kidato cha 2 na mwingine cha 4 kunipigia simu kwamba wamefukuzwa shule kwa sababu ya ada Ikabidi nishtuke kumpigia mzee kutaka kujua nini kimetokea maana moja ya makubaliano yetu ni watoto kulipiwa ada, bila matarajio alinijibu kiukali sana na kunitaka nilipe gharama zake za matunzo yangu alivyonilea, ikanibidi nianze kufuatilia kupata hati za nyumba na viwanja nilivomtuma aninunulie kufika pale kwenye nyumba na viwanja vyote vishauzwa na yeye amejenga nyumba nyingine ambayo anaishi na mwanamke mwingine na tayari Wana mtoto mzee kweli ni mhuni lakini sikutegemea atafikia kiwango hiki. Nilihisi kuchanganyikiwa, ilileta mgogoro kidogo kati yangu na yeye lakini niliradhimika kusamehe. Mzigo wa pale nyumbani watoto wa5 wote wako shule private baba yangu akawa hana mda nao tena.

Nikaingia kwenye majukumu mazito na magumu lakini mungu akanifungulia riziki kipato nilichokuwa nakipata kikawa si haba nikapambana nao mpaka wengine leo wako chuo na kuweza kujenga nyumba nzuri zaidi kwa ajili ya familia na nikafungua miradi pale nyumbani ili kuwezesha kupata pesa za matumizi madogo na kujikimu kwa familia, wakuu sikujua lengo la baba kwa kweli yaani alichukua kirikuu akasomba vitu vyote dukani mpaka leo haijulikani alipeleka wapi na mtaji wote wa biashara za mobile money transaction akachukua.

Kinachonifanya nimfungulie kesi ni hiki, nilinunua kiwanja mwaka juzi kwa 16m na yeye akiwa shahidi hati nikaiacha nyumbani kwa mama na mara kadhaa nimekuwa naisahau kuichukua mwezi January naenda kuweka uzio kwenye uwanja wangu nakuta kumeshajengwa, namuuliza aliyepo anasema ameuziwa na baba na hati anatoa ambayo niliyouziwa mimi mwanzoni kumuuliza mama anasema yeye alitunza kwenda kuangalia alipoiweka haipo, na Mimi nina familia nishachoka nitaka nimburuze mahakamani.

Kuna mda inafika kiwango cha uvumilivu kinaisha, ukisikia watu watu wanauana ni mambo Kama haya na hapa ndipo unapoona Kama Diamond hama mda na baba yake hapaswi kulaumiwa Hawa wazee wengine ni WAPUMBAVU mambo mengi nimeamua kufupisha, maana nahisi kumtwanga hata risasi huyu mke wake amerudisha nyuma sana kwenye uchumi wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya ni madhara ya kumtelekeza baba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimemtelekezaje mkuu? Mpaka nilimpa 28m kuboost mtaji wa miradi yake, 30m za kumalizia malipo ya nyumba yangu, 12m za viwanja zote kala mkuu yaani angekuwa sio baba ningekuwa nshamramba risasi.

Acha baba, ulishawahi kumlamba risasi hata njiwa.?
 
Umeongea kwa uchungu sana, Hawa wazee kuna wengine wanafeli sana...

Naomba nikushauri kitu hata mkienda mahakaman nna uhakika hakuna kitu ambacho utarudishiwa kwa namna yoyote ile zaidi ya kupoteza muda
ila kama unao muda wa kufatilia kesi za madai fanya.

Umesema wadogo zako wengine wapo chuo anza kuwaingiza kwenye miradi yako kama ambavyo wajomba zako walikufunza wewe.

Anzisha mradi ambao utakua unalisha familia na kusomesha ambao bado wanahitaji kusomeshwa inaweza isiwe ule mkoa ambako mzee wako yupo au kama huko bas shirikiana na wadogo zako ambao wapo pale bila mzee wako kufaham chochote.

Ushajishusha kwa mzee wako imetosha chakufanya sasa badilisha namna ya kusaidia hao waliobakia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ushauri mwingine tuko pamoja, la kumshitaki mzee aachane nalo kabisa.
Inauma lakini lazima asamehe, lazima. Na avumilie hayo maamuzi ya mzee ya kuwa na mwanamke mwingine, si vyema kwenda deep.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mzee wangu sitaki kumsema uongo alinitunza vema sana tatzo la uhuni na alipoanza kupata pesa alibadilika sana na hapo ndipo uhuni ulipozidi mpaka mda huu tunafikishana huku na sijui kakamatwaje kwa sasa kawa ni zaidi ya MPUMBAVU ukoo mzima unamshangaa. Yaani Kama nisingesimama kwenye familia basi Hawa madogo wangekuwa wanajiuza na wengine machokoraa hakukuwa na msaada mwingine

Sent using Jamii Forums mobile app
"Wengi wape" ila si mara zote huyo ni mzee wako hata kama ana mapungufu ya wazi usiungane na ukoo wako kumsakama kwa ujinga wake na uhuni jaribu kutafuta muda ambao unaweza kuonekana ni muda wa kipuuzi omba appointment naye kisha kirafiki anza kuongea naye ukiamini ni mpumbavu, yaani vaa uhusika kama vile wewe ndiye baba yake.

Jaribu kumuuliza anaona hatima gani na maisha yake pamoja na familia ameamua iwe katika njia hiyo au kuna kitu kipo ndani yake. Huwenda mzee wetu amepata mhuni ambaye amevuruga ufahamu wake na haelewi chanya wala hasi. Usimhukumu kuwa ni mpumbavu wala mjinga ila tafuta chanzo cha upumbavu wake huo ambao amekuwa nao hivi karibuni najua upumbavu wake huwenda ni msukumo kutoka kwa yule ambaye anakaa naye sasa.

Ulipambana na kupata zaidi ya milioni 10 na viwanja ukanunua huku wadogo zako wa5 ukikomaa nao na tena wako private schools. Huoni kama wewe ni mtu ambaye unaweza kumudu mambo mazito na kuyatatua? Wewe inatakiwa mzee wako ndiye akuone mpumbavu kwa yote ambayo kakutendea na umekaa kimya. Hebu onesha mzee kuwa amezaa dume lisilotetereka katika magumu kama hayo aliyokupitisha.

Utadai pesa je asipokuwa nazo atakulipa nini? Najua unaweza kuishi bila hizo pesa ambazo unataka kudai kwa huyo mzee wako. Kama uchumi wako haujatetereka achana na kelele za kifamilia unda himaya yako uwe mfalme katika himaya yako uishi katika misingi yako uache kufuatilia huyo unaeita mpumbavu.
 
Pole sana mkuu, huyu mzee alikutunza vyema wakati hajaanza kufanya huo unaoita upumbavu au alikuwa hivyo tangu zamani?

Je ana mgogoro na mkewe yaani mama yako.?

Umewahi kufuatilia japo kujua chanzo cha yeye kurudi nyuma kiuchumi ni nini.?
Achimbe tena kuhusu mama yake na baba yake ?
Hapana asamehe tu Mungu atampigania atanyanyuka. Kuna vitu si vya kujua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom