Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,508
- 830,009
Si mbaya kwakweli kuwa na nyumba ndogo kama ukiona shemeji hakutoshelezi mahitaji, japo kuna wengine wameingia huko kutokana na stress za ndoa na migogoro lakini wengine ni tamaa tu na kutoridhika na mmoja!
Nyumba ndogo zina utamu wake, lakini pia zina nguvu na ushawishi wa ajabu kabisa. Kuna wengine wamenogewa kabisa na kuhamishia majeshi yote nyumba ndogo ama kuoa kabisa.
Jihadhari rafiki kuwa makini usije kuangukia huo mtego. Utajuta majuto yote na hutapata wa kukusaidia.
Ni nyumba ndogo chache zenye akili hekima na tafakuri! Anajua vema uwepo na umuhimu wa nyumba kubwa hivyo hukusaidia kuijenga kwakuwa anatambua fika kule kukiharibika hata huku amani huwa ndogo.
Kuna wenye bahati mbaya walinaswa kwenye nyumba ndogo za hivyo na kunogewa kabisa (sometimes madawa yakitumika). Nyumba ndogo hizi zina nia ya kuharibu ama sometimes ni uchoyo tu na ubinafsi. Kipindi uko kwake kwako umeaga uko semina uko kazini, uko safarini uko na washkaji nk nk, anajua uongo wote uliokuwa ukidanganya.
Leo hii unataliki mkeo halali wa ndoa na kwenda kuishi na bi mdogo. MY FRIEND UMEKWISHA! Utamdanganya nini mwizi? Utakuwa umejipeleka mwenyewe kifungoni kwenye gereza la kujitakia. Utapekuliwa wallet, utapekuliwa simu, utapekuliwa nguo! Utafuatiliwa kazini, utachaguliwa marafiki na utapangiwa muda wa kurudi nyumbani na hata muda wa kutoka weekend. Furaha yako itageuka fadhaa
Nikukumbushe tu rafiki cheza kwa step
NB : Nyumba ndogo nyie ndio msingi imara wa ndoa nyingi, bebeni kwa weledi hili jukumu huku mkitambua fika kwamba SIKIO ni SIKIO tuu kamwe haliwezi kuzidi KICHWA
Sent using Jamii Forums mobile app
Nyumba ndogo zina utamu wake, lakini pia zina nguvu na ushawishi wa ajabu kabisa. Kuna wengine wamenogewa kabisa na kuhamishia majeshi yote nyumba ndogo ama kuoa kabisa.
Jihadhari rafiki kuwa makini usije kuangukia huo mtego. Utajuta majuto yote na hutapata wa kukusaidia.
Ni nyumba ndogo chache zenye akili hekima na tafakuri! Anajua vema uwepo na umuhimu wa nyumba kubwa hivyo hukusaidia kuijenga kwakuwa anatambua fika kule kukiharibika hata huku amani huwa ndogo.
Kuna wenye bahati mbaya walinaswa kwenye nyumba ndogo za hivyo na kunogewa kabisa (sometimes madawa yakitumika). Nyumba ndogo hizi zina nia ya kuharibu ama sometimes ni uchoyo tu na ubinafsi. Kipindi uko kwake kwako umeaga uko semina uko kazini, uko safarini uko na washkaji nk nk, anajua uongo wote uliokuwa ukidanganya.
Leo hii unataliki mkeo halali wa ndoa na kwenda kuishi na bi mdogo. MY FRIEND UMEKWISHA! Utamdanganya nini mwizi? Utakuwa umejipeleka mwenyewe kifungoni kwenye gereza la kujitakia. Utapekuliwa wallet, utapekuliwa simu, utapekuliwa nguo! Utafuatiliwa kazini, utachaguliwa marafiki na utapangiwa muda wa kurudi nyumbani na hata muda wa kutoka weekend. Furaha yako itageuka fadhaa
Nikukumbushe tu rafiki cheza kwa step
NB : Nyumba ndogo nyie ndio msingi imara wa ndoa nyingi, bebeni kwa weledi hili jukumu huku mkitambua fika kwamba SIKIO ni SIKIO tuu kamwe haliwezi kuzidi KICHWA
Sent using Jamii Forums mobile app